TRANSFORM JUSTICE INTO PASSION 2009 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: i KITUO CHA HUDUMA ZA SHERIA ZANZIBAR Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kiliazishwa mnamo mwaka 1992. Ni moja ya Asasi isiyokuwa ya kiserikali ambayo ni ya kujitolea, inayojitegemea na ni asasi ambayo si ya kibiashara. Lengo kuu la Kituo ni kutoa huduma za sheria kwa watu wote wasiojiweza wakiwemo; maskini, wanawake, watoto na watu wenye ulemavu Zanzibar. Mbali na lengo hilo Kituo pia kimeanzishwa kwa madhumuni ya kueneza elimu ya sheria kwa kuandika na kutoa machapisho mbalimbali ya sheria. Hii ni moja ya njia za kuhakikisha kuwa wazanzibari wote wanapata elimu ya msingi inayohusiana na masuala ya sheria hasa katika kujuwa hali zao, ili kujenga jamii ambayo inaheshimu, Utawala wa Sheria, Utawala Bora na kuheshimu, kulinda na kutekeleza misingi ya Haki za Binadamu Zanzibar. Malengo ya Kituo Kituo kinafanya kazi za kisheria zikiwemo; uwakilishi Mahakamani, na usuluhishi wa migogoro kwa kuzingatia maslahi ya watu wasiojiweza na maskini. Pia Kituo kinafanya kazi ya kunatoa elimu ya kisheria kwa jamii ili kuongeza uelewa wa masuala ya sheria na Haki za Binaadamu kwa kupitia semina, makongamano, na mijadala inayohusiana na masuala ya kisheria ili kuwawezesha watu kutoka sehemu tofauti kujadili sera za kisheria na kimaendeleo. Kituo pia kinaandaa mikutano ya kitaalamu kwa ajili ya kutoa mafunzo kutoka sekta tofauti katika jamii ya Zanzibar. Shughuli za Kituo Malengo ya kituo yanatimizwa kwa kutekeleza shughuli zifuatazo:1. Ushauri wa Kisheria; 2. Mafunzo ya Wasaidizi wa Sheria; 3. Mafunzo ya Haki za Binaadamu; ii Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 4. Utoaji wa Haki; 5. Majarida, Vitabu na Vipeperushi; 6. Vipindi vya Redio; 7. Vipindi vya Televisheni; na 8. Program za Mafunzo wa Wahitimu wa Sheria. Dira ya Kituo Azma ya kituo ni kuhakikisha kwamba kila mzanzibari, hasa watu maskini, wanawake, watoto, watu wenye ulemavu na makundi yote katika jamii wanaelewa vizuri haki zao za msingi za kisheria na kanuni za Haki za Binaadamu na pia waweze kuzidai ili kujenga jamii iliyojengwa kwenye msingi ya utawala wa sheria, utawala bora na kuheshimu misingi ya haki za binaadamu. Dhamira ya Kituo Kituo kimekusudia kuongeza uelewa wa jamii juu ya haki zao na wajibu kwa kutoa elimu ya sheria na Haki za Binaadamu, utafiti wa maswala ya kisheria, kuendesha semina, warsha, mikutano, na kutoa ushauri wa msaada wa kisheria. Muundo wa Kituo Kituo cha Huduma za Sheria kimesajiliwa chini ya Sheria za Zanzibar. Kinaendeshwa na Bodi ya Wadhamini ambayo wajumbe wake kwa sasa ni: Prof. Chris Maina Peter Profesa wa Sheria, Chuo Kikuu cha Dar es Salaam na ni Wakili wa Mahakama Kuu Ya Tanzania (Kaimu Mwenyekiti). Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: iii Bi. Safia Masoud Khamis Mwanasheria wa Serikali, Afisi ya Mkurugenzi mwendesha Mashtaka, Zanzibar(Mjumbe). Bi. Josefrieda Pereira Mhadhiri Chuo Kikuu cha Taifa Zanzibar ± SUZA(Mjumbe) Bw. Iss-haq I. Shariff Mkurugenzi Mtendaji, Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar, Katibu wa Bodi ya Wadhamini. Wafanyakazi wa Kituo Kwa sasa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kina wafanyakazi wa kada mbali mbali wapatao 14. Kumi wapo katika ofisi yake ya Unguja na Wanne wapo katika ofisi ya Pemba iliyopo Chake Chake. Maadili ya Kituo Watu wote wanaoshiriki katika shughuli za Kituo ni lazima wawe ni watu wenye dhamira nzuri kwa watu wote katika masuala yote yanayohusiana na Kituo, na hawaruhusiwi kutumia huduma pamoja na jina la Kituo kwa ajili ya maslahi yake binafsi, kisaisa, kidini, au jambo lolote ambalo liko nje ya malengo ya Kituo. iv Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Anwani Unaweza kuwasiliana na Kituo kwa anuani ifuatayo:Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar S.L.P. 3360, Kibokoni(Mkabala na Skuli ya Maandalizi ya Kidutani) Zanzibar. Simu:+255(024) 223 3784. Faksi+255(024) 223 4495. Afisi ya Pemba: S.L.P. 18 Chake Chake Pemba. Simu:+255(024) 2452 936 Barua Pepe: zlsc@hudumazasheria.or.tz Tovuti: www.hudumazasheria.or.tz Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: v DIBAJI Moja ya lengo kuu la Kituo cha Huduma za Sheria ni kutoa msaada wa kisheria bila ya malipo. Hivyo, kazi hii ilianza kutekelezwa mara tu baada ya kuanzishwa kwa Kituo kwa kutumia Wanasheria wa Serikali. Idadi ya watu wenye kuhitaji huduma hii ilikuwa ikiongezeka kila kukicha, na hivyo uhaba wa huduma hizo ulianza kuonekana baada ya kuongezeka kwa idadi ya watu wa Zanzibar na wazanzibari walio wengi kuanza kupata uelewa juu ya haki zao na hivyo kujitokeza kwa wingi kutaka huduma. Hapo ndipo Kituo kilipoanza kutafuta njia mbadala ya kukidhi haja hiyo na kuona kuwa upo umuhimu wa kupanua huduma za msaada wa kisheria mjini na vijijini. Hivyo basi Kituo kilibuni utaratibu wa kuweka Wasaidizi wa Sheria katika sehemu zote za Zanzibar ili kurahisisha upatikanaji wa huduma hiyo. Hivyo mnamo mwaka 2007 Kituo kilianzisha rasmi mpango huo. Mpaka sasa, Kituo kimeweza kuwaajiri Wasaidizi wa Sheria wasiopunguwa hamsini(50) ambao wamesambazwa katika majimbo yote ya uchaguzi yaliyoko Unguja na Pemba. Wasaidizi hao wamepatiwa elimu ya msingi inayohusiana na masuala ya sheria pamoja na kupata maelekezo kutoka kwa maafisa mipango wa Kituo juu ya utoaji wa msaada wa kisheria. Licha ya hayo Kituo pia kimeona iko haja ya kutayarishia Wasaidizi hawa muongozo ambao utakuwa unawaongoza katika utekelezaji wa majukumu yao ya kazi. Umuhimu wa muongozo huu ni kuwa umejaribu kugusia nyanja zote ambazo ni muhimu katika kuhakikisha Utawala wa Sheria unakuwepo nchini ikiwemo; Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984, na Katiba ya Jamhuri wa Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977 pamoja na misingi mikuu na kanuni muhimu zilizomo ndani yake kama vile Utawala wa Sheria, Uhuru wa Mahakama, Haki na wajibu wa Binaadamu(raia), Utawala Bora, Mihimili mikuu ya Serikali pamoja na kazi zake. Pia muongozo huu umejaribu kufafanua sheria tofauti zikiwemo Sheria za Kazi, Sheria za Ardhi, Sheria za Makosa vi Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: ya Jinai na Makosa ya Madai, Sheria za Vikosi vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Sheria za Uchaguzi za Zanzibar, Sheria ya Mzanzibari pamoja na Sheria ya Usajili wa Vitambulisho vya Mzanzibari, Sheria za Tawala za Mikoa na Sheria ya Kumlinda Mwari na Mtoto mwenye Mzazi Mmoja. Katika kuhakikisha wasaidizi wa sheria wanafanyakazi katika mazingira mazuri, Kituo kimewatambulisha rasmi wasaidizi hao wa sheria katika sehemu zote husika za kiserikali pamoja na kuwapatia vitendekea kazi vyote muhimu zikiwemo Katiba zote mbili. Mwisho Kituo kinachukua fursa hii ya kuwashukuru wale wote walioshiriki katika kuandaa muongozo huu kwa nia moja au nyingine kwa kutumia muda wao, ujuzi pamoja na fikra zao ili kuhakikisha muongozo huu umechapishwa katika hali ya kufahamika kwa watu wote. Watayarishaji husika wa muongozo huu ni Bwana Yahya Khamis Hamad na Abdulhakim Issa. Wengine walioshiriki katika kuufanyia marekebisho ni Prof. Haroub Othman, Bw. Ishaq Shariff, Bi. Naima Azzan pamoja na Said Hassan Said na Bi Fatma Abdalla Hassan. Bila ya kusahau Kituo kinatoa shukrani zake kwa wafadhili wake kwa kuweza kukisaidia Kituo katika kuendesha kazi zake nao ni Danish International Development Agency(DANIDA), Finland International Development Agency(FINIDA), Swedish International Development Agency(SIDA). Shukrani za pekee ziwaendee Sigrid Rausing Trust kwa kuweza kufadhili mpango huu wa wasaidizi wa sheria kwa muda mrefu. Mwishoni tungependa kuwashukuru kwa namna ya pekee Shirika la Friedrich Ebert Stiftung(FES) la Ujerumani na hasa Mkurugenzi wake Mkazi Bw. Peter Haeussler kwa kukubali kufadhili uchapishaji wa Mwongozo huu na pia Bi. Angela Ishengoma ambaye bila ya kuchoka amekuwa akituhimiza kumaliza kazi hii na kuisimamia hadi kufikia mwisho wake. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: vii Wote kwa pamoja wamechangia kwa kiasi kikubwa katika kuleta karibu huduma ya sheria kwa wananchi wa kawaida wa Zanzibar na hasa wale ambao hawawezi kumudu kulipia huduma muhimu za mawakili. Prof. Chris Maina Peter Kaimu Mwenyekiti Bodi ya Wadhamini Kituo Cha Huduma za Sheria Cha Zanzibar Tarehe 2 Novemba, 2009 viii Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: NAMNA YA KUUTUMIA MUONGOZO HUU Muongozo huu ni kwa ajili ya ufundishaji wa Wasaidizi wa Kisheria Zanzibar. Lengo la Muongozo huu ni kumuwezesha Msaidizi wa Kisheria baada ya kukamilika kwa mafunzo haya aweze kukabiliana na masuala mengi yanayotokea katika jimbo analoishi yanayohusiana na Sheria, kwa kuwashauri wananchi waliopatawa na matatizo au wenye migogoro njia gani bora ya kutumia katika kutatua mgogoro au mzozo waliokuwa nao. Kwa kuwa Wasaidizi wa Kisheria sio watu wenye msingi wa mafunzo ya sheria, au kama wamepata mafunzo ya kisheria ni kwa hatua ya cheti tu, mafunzo haya yanategemea kufanyika kwa awamu tano katika kipindi cha mwaka mmoja. Hivyo, Muongozo huo umegawika katika misingi hiyo ya kufuata awamu ambazo Wasaidizi wa Kisheria watafundishwa. Awamu hizi zimepewa jina la Sura, hivyo kuna Sura ya 1 hadi ya 5. Lakini kutokana na kuhofia kuwachosha walengwa na pia katika jitihada ya kujaribu kuwafundisha sheria walengwa katika kila awamu baadhi ya mada imebidi zigaiwe katika awamu zaidi ya moja ili walengwa waweze kufaidika zaid na mafunzo haya. Kwa mfano, mada ya Katiba imegawanywa katika sehemu tatu ambazo zitafundishwa katika awamu tatu za mwanzo. Hali kadhalika pia Sheria nazo zimegawanywa na zitafundishwa katika awamu tofauti kulingana na umuhimu wa Sheria ipi ifundishwe mwanzo, na pia kwa kuzingatia mtiririko wa mada zenyewe. Ni matumaini yetu kuwa msomaji ataweza kuutumia vyema muongozo huu na pia utakuwa ni hazina ya taaluma katika kuwashauri watu wengine ambao wana matatizo ya kisheria. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: ix YALIYOMO Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar_______________ i Dibaji_________________________________________ v Namna ya Kuutumia Muongozo Huu_________________ viii Yaliyomo_______________________________________ ix Vifupisho______________________________________ xvi SURA YA KWANZA____________________________ 1 Sehemu ya Kwanza___________________________ 1 1.1.0 Mpango wa Usaidizi wa Kisheria___________ 1 1.1.1 Dhana ya Sheria________________________ 1 1.1.2 Dhana ya Usaidizi wa Kisheria____________ 2 1.1.3 Sifa za Wasaidizi wa Kisheria_____________ 2 1.1.4 Kazi za Usaidizi wa Kisheria______________ 3 1.1.5 Changamoto Juu ya Mpango Wenyewe______ 4 1.1.6 Haja ya Kuwepo Mpango wa Usaidizi wa Kisheria____________________________ 5 1.1.7 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar na Wazo la Kuwepo Usaidizi wa Kisheria______ 7 1.1.8 Nafasi ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Katika Usaidizi wa Kisheria_______________ 8 1.1.9 Vitendea Kazi vya Wasaidizi wa Kisheria____ 9 Sehemu ya Pili_______________________________ 10 1.2.0 Katiba za Nchi na Misingi Muhimu Iliyomo__ 10 1.2.1 Utangulizi_____________________________ 10 1.2.2 Maana ya Katiba________________________ 10 1.2.3 Katiba ni Sheria Mama___________________ 11 1.2.4 Historia Fupi na Misingi Muhimu ya Kikatiba_ 12 1.2.4.1 Historia Fupi_____________________ 12 1.2.4.2 Misingi Muhimu ya Kikatiba________ 13 Sehemu ya Tatu_____________________________ 15 1.3.0 Sheria Mbali Mbali_____________________ 15 1.3.1 Sheria ya Tawala za Mikoa_______________ 15 x Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 1.3.2 1.3.3 1.3.4 1.3.1.1. Mamlaka ya Mikoa_______________ 15 1.3.1.2 Mamlaka ya Wilaya_______________ 16 1.3.1.3 Mamlaka ya Shehia_______________ 16 Sheria ya Jinai_________________________ 18 1.3.2.1 Nini Kosa la Jinai________________ 18 1.3.2.2 Tofauti kati ya Makosa ya Jinai na Makosa ya Madai________________ 19 1.3.2.3 Ufunguaji wa Kesi ya Jinai_________ 19 1.3.2.4. Makosa ya Jinai_________________ 19 1.3.2.5 Makosa ya Kujamiana_____________ 22 1.3.2.5.1 Kubaka_________________ 22 1.3.2.5.2 Uvunjaji wa Heshima na Udhalilishaji wa Kijinsia___ 23 1.3.2.5.3. Makosa yanayowahusu Watoto23 1.3.2.6 Masharti ya Msingi Kuhusu Dhima au Hatia Katika Makosa ya Jinai________ 24 1.3.2.6.1 Kutojua Sheria____________ 24 1.3.2.6.2 Kutojua Ukweli___________ 25 1.3.2.6.3 Uwezo wa Kuzuia Mali_____ 25 1.3.2.6.4 Kutokuwa na Akili Timamu_ 26 1.3.2.6.5 Ulevi___________________ 26 1.3.2.6.6 Umri Mdogo_____________ 26 Sheria ya Kuwalinda Wari na Watoto wa Mzazi Mmoja_________________________ 27 1.3.3.1 Matunzo ya Watoto_______________ 28 Sheria Juu ya Kazi za Polisi_______________ 29 1.3.4.1 Polisi na Upelelezi Katika Makosa ya Jinai___________________________ 29 1.3.4.2 Upelelezi wa Makosa ya Jinai_______ 30 1.3.4.3.Polisi na Uwezo wa Kumkamata Mtu_ 30 1.3.4.4 Namna ya Kumkamata Mshukiwa na Haki zake_______________________ 32 1.3.4.5 Muda wa Mtu Kuhojiwa___________ 33 1.3.4.6. Namna ya Upekuzi_______________ 34 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: xi 1.3.5 Kanuni za Kutumikia Jamii______________ 35 SURA YA PILI________________________________ 37 Sehemu ya Kwanza__________________________ 37 2.1.0 Katiba na Mgawanyo wa Madaraka________ 37 2.2.0 Utawala wa Sheria______________________ 39 2.2.1. Maana ya Utawala wa Sheria_____________ 39 2.2.2. Usawa Mbele ya Sheria_________________ 40 2.2.3. Umuhimu wa Utawala wa Sheria__________ 41 2.3.0 Muundo na Kazi za Mihimili Mikuu________ 42 2.3.1 Serikali ya Mapinduzi Zanzibar____________ 42 2.3.2 Mahakama____________________________ 43 2.3.2.1 Uhuru wa Mahakama_____________ 47 2.3.2.3 Umuhimu wa Uhuru wa Mahakama__ 48 2.3.2.4 Vyombo Vyenye Mamlaka ya Kimahakama____________________ 48 2.3.2.4.1 Mahakama ya Ardhi_______ 49 2.3.2.4.2 Mahakama ya Kumlinda Mlaji___________________ 49 2.3.2.4.3 Mahakama y aKudhibiti Kodi ya Nyumba_________ 50 2.3.2.4.4 Mahakama ya Kazi________ 50 2.3.3 Baraza la Wawakilishi___________________ 50 2.3.3.1 Kazi ya Baraza la Wawakilishi______ 50 2.3.3.2 Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi__ 51 2.3.3.3 Uongozi wa Baraza_______________ 51 2.3.3.4 Kamati za Baraza la Wawakilishi____ 52 Sehemu ya Pili______________________________ 53 2.4.0 Sheria Mbali Mbali_____________________ 53 2.4.1 Sheria ya Madai________________________ 53 2.4.1.1 Ufunguzi wa Kesi za Madai_________ 55 2.4.1.2 Hatua za Ufunguaji na Uendeshaji wa Kesi za Madai____________________ 56 2.4.1.3 Ukomo wa Ufunguzi wa Kesi ya Madai_58 xii Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 2.4.2 Sheria ya Mikataba_________________ 59 2.4.2.1 Maana ya Mkataba________________ 59 2.4.2.2 Aina ya Mkataba__________________ 60 2.4.2.3 Masharti ya Mkataba_______________ 61 2.4.2.4 Sifa za Mikataba__________________ 61 SURA YA TATU_______________________________ 63 Sehemu ya Kwanza__________________________ 63 3.0 Haki za Binadamu______________________ 63 3.1 Chanzo cha Haki za Binadamu____________ 63 3.2 Sheria za Kimataifa na Haki za Binadamu___ 64 3.2.1 Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa 1945_ 64 3.2.2 Tangazo la Haki za Binadamu la 1948___ 65 3.2.3 Mkataba wa Kimataifa Juu ya Haki za Kiraia na Kisiasa____________________67 3.2.3.1 Chombo cha Utekelezaji________68 3.2.4 Mkataba wa Kimataifa Juu ya Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni____ 68 3.2.4.1 Chombo cha Utekelezaji______ 69 3.3 Mikataba ya Kikanda_____________________ 69 3.3.1 Mkataba wa Afrika Juu ya Haki za Binadamu na Haki za Watu wa 1981____70 3.4 Haki za Binadamu ni Haki za Kisheria?______ 71 3.5 Katiba na Historia Fupi ya Haki za Binadamu Zanzibar_______________________________ 71 3.6 Misingi ya Haki za Binadamu______________ 73 3.6.1 Haki za Kutambuliwa na Kuthaminiwa__ 73 3.6.2 Haki za Usawa_____________________ 74 3.6.3 Haki ya Hifadhi ya Maisha___________ 74 3.6.4 Haki ya Kutoteswa au Kuadhibiwa Kinyama__________________________ 74 3.6.5 Uhuru wa Maoni na Kupata Taarifa____ 75 3.6.6 Uhuru wa Imani na Kuabudu__________ 75 3.6.7 Uhuru wa Kujikusanya_______________75 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: xiii 3.6.8 Uhuru wa Kufanya Kazi na Kupata Ujira_75 3.6.9 Uhuru wa Mtu Kwenda Atakako_______76 3.6.10 Uhuru wa Faragha__________________76 3.7 Wajibu wa Raia_________________________ 76 3.8 Katiba na Utawala Bora___________________77 3.8.1 Misingi Muhimu ya Utawala Bora______78 Sehemu ya Pili________________________________81 3.9.0 Sheria Mbali Mbali______________________ 81 3.9.1 Sheria za Ardhi_________________________ 81 3.9.1.1 Sheria ya Matumizi ya Ardhi________ 81 3.9.1.1.1 Maana ya Ardhi___________ 81 3.9.1.1.2 Umiliki wa Ardhi__________ 82 3.9.1.1.3 Masharti ya Haki za Kuhodhi na Kutumia Ardhi_________ 82 3.9.1.1.4 Kukatishwa kwa Haki za Matumizi ya Ardhi________ 83 3.9.2 Sheria za Uhaulishaji Ardhi_______________ 84 3.9.2.1Sheria ya Uhaulishaji Mali Sura 150-__ 84 3.9.2.1.1 Kipi Kinahaulishika________ 85 3.9.2.1.2 Nani Anaweza Kuhaulisha/ Kuhaulishiwa_____________ 85 3.9.2.1.3 Aina za Uhaulishaji_________86 3.9.2.1.4 Haki/ Wajibu wa Muhaulishaji /Muhaulishiwa____________ 86 3.9.2.2 Sheria ya Uhaulishaji Ardhi Namba 8 ya 1994__________________ 87 3.9.2.2.1 Bodi ya Uhaulishaji Ardhi___ 87 3.9.2.2.2 Utaratibu wa Kuomba Ridhaa ya Bodi____________88 3.9.2.2.3 Masharti ya Ombi__________ 88 3.9.2.2.4 Sababu za Kutotoa Idhini/Ridhaa ya Kuhaulisha_ 89 3.9.3 Sheria ya Usajili wa Ardhi_________________ 89 3.9.3.1 Umuhimu wa Kusajili Ardhi_________ 91 xiv Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: SURA YA NNE_________________________________ 92 Sehemu ya Kwanza___________________________ 92 4.0 Sheria Mbali Mbali_________________________ 92 4.1 Sheria ya Mzanzibari________________________ 92 4.1.1 Nani Mzanzibari?______________________ 92 4.1.2 Uzanzibari wa Kuomba_________________ 93 4.2 Sheria ya Usajili wa Wazanzibari Wakaazi______ 93 4.3 Sheria ya Uchaguzi_________________________ 95 4.3.1 Mgawanyo wa Majimbo________________ 95 4.3.2 Uandikishaji Wapiga Kura______________ 96 4.3.3 Uteuzi wa Wagombea Urais, Uwakilishi, na Udiwani__________________________ 96 4.3.4 Kampeni za Uchaguzi__________________ 99 4.3.5 Upigaji Kura_________________________ 99 4.3.6 Kuhesabu Kura_______________________ 100 4.3.7 Kujumlisha Kura______________________ 100 4.3.8 Kutangaza Matokeo____________________ 100 Sehemu ya Pili_______________________________ 101 4.4.0 Sheria za Idara Maalum za SMZ_____________ 101 4.4.1 Kikosi cha Valantia_______________________ 102 4.4.1.1 Uwezo na Haki za Valantia___________ 102 4.4.2 Kikosi cha Kuzuia Magendo________________ 103 4.4.3 Jeshi la Kujenga Uchumi___________________ 105 4.4.4 Kikosi cha Zimamoto na Uokozi_____________ 107 4.4.5 Chuo Cha Mafunzo_______________________ 108 4.4.5.1 Masuala ya Afya___________________ 109 4.4.5.2 Wakaguzi wa Chuo__________________109 4.4.5.3 Upokeaji wa Wanafunzi na Nidhamu____110 4.4.5.4 Haki za Wanafunzi__________________112 4.4.6 Tume ya Utumishi ya Idara Maalum___________113 SURA YA TANO________________________________ 114 5.0 Sheria Mbali Mbali__________________________ 114 5.1 Sheria za Kazi_______________________________114 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: xv 5.2 Sheria ya Ajira_______________________________ 114 5.2.1 Mkataba wa Ajira________________________114 5.2.2 Matumizi ya Sheria na Haki za Msingi_______ 116 5.2.3 Viwango na Haki za Waajiriwa_____________ 117 5.2.4 Haki za Waajiriwa_______________________ 117 5.2.5 Hatua za Kinidhamu na Adhabu____________ 118 5.2.6 Usimamizi wa Sheria_____________________ 118 5.3 Sheria ya Mahusiano Kazini_____________________119 5.3.1 Haki za Msingi__________________________ 119 5.3.2 Mapatano na Makubaliano ya Pamoja________ 120 5.3.3 Migogoro ya Kazi________________________120 5.4 Sheria ya Usalama na Afya Kazini________________121 5.4.1 Usimamizi wa Usalama na Afya____________ 122 5.4.2 Uteuzi wa Wawakilishi wa Usalama na Afya Kazini__________________ 122 5.4.3 Masharti ya Usalama, Afya na Ustawi_______ 123 5.4.4 Haki na Wajibu wa Waajiriwa______________125 5.5 Sheria ya Fidia ya Wafanyakazi__________________125 5.5.1 Fidia Kutokana na Maumivu_______________ 126 5.5.2 Fidia kwa Wachumaji Karafuu______________127 5.5.3 Fidia kwa Wanamichezo___________________128 5.5.4 Madai ya Fidia___________________________128 5.5.5 Maradhi Yanayotokana na Ajira_____________130 5.6 Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii______________130 5.6.1 Michango Katika Mfuko____________________131 5.6.2 Mafao Yanayotolewa na Mfuko______________131 Vitabu vya Marejeo________________________________133 xvi Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: ACHPR AR CPT DANIDA DPP ECOSOC FES FINIDA ICCPR ICESCR IDS JKU KMKM KVZ n.k. P.A.C. PGO S.L.P. VIFUPISHO African Charter on Human and Afisi ya Rais Christian Professionals of Tanzania Danish International Development Agency Director of Public Prosecutions Economic and Social Council Friedrich Ebert Stiftung Finland International Development Agency International Covenant on Civil and Political Rights International Covenant on Economic, Social and Cultural Rights Institute of Development Studies Jeshi la Kujenga Uchumi Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo Kikosi cha Valantia Na Kadhalika Public Accounts Committee Police General Orders Sanduku la Posta Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: xvii SIDA SMZ SUZA TANU TEC UDHR UN ZLSC ZSTC Sweden International Development Agency Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar State University of Zanzibar Tanganyika African National Union Tanzania Episcopal Conference Universal Declaration of Human Rights United Nations Zanzibar Legal Services Centre Zanzibar State Trading Corporation Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 1 SURA YA KWANZA Sehemu ya Kwanza 1.1.0 Mpango wa Usaidizi wa Kisheria Mpango wa usaidizi wa kisheria ni mpango unaolenga kuwapata watu ambao sio wanasheria lakini wanauelewa fulani juu ya mambo ya sheria, kuwatayarisha kwa kuwafanyia mafunzo na iwapo wataonekana wanafaa watafanya kazi ya kuisaidia jamii katika kuinua ufahamu wa mambo ya kisheria. 1.1.1 Dhana ya Sheria Sheria ni mfumo wa kanuni ambao huwekwa na Baraza la Wawakilishi au Taasisi nyingine yoyote iliyopewa jukumu hilo. Kila mtu aliyemo ndani ya nchi wakiwemo watunga sheria wenyewe, hutakiwa kuufuata mfumo huo. Zipo Sheria za aina mbili: (a). Sheria za Umma( public law). Hizi ni zile sheria zinazoweka masharti kuhusu mahusiano baina ya mtu binafsi na dola au jamii kwa ujumla. Mfano ni Katiba, Sheria za Jinai, Sheria ya Mwendendo wa Jinai n.k. (b). Sheria za Mahusiano binafsi( Private Law). Sheria hizi zinaweka masharti yanayokusudia kudhibiti mahusiano ya mtu na mtu katika maisha ya kila siku. Mfano ni sheria za mikataba, madhara, ndoa, mila, mirathi, n.k. Kutokana na makundi haya mawili pia tunaweza kutofautisha sheria katika namna nyingine mbili: (a). Sheria zinazoweka masharti kuhusu haki na wajibu mfano ni sheria za jinai, sheria za madhara, n.k 2 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: (b). Sheria zinazoweka utaratibu wa kufuatwa katika utoaji haki. Mfano ni Sheria ya mwenendo wa Jinai, na Sheria ya Mwenendo wa Madai. 1.1.2 Dhana ya Usaidizi wa Kisheria Tunapozungumzia Usaidizi wa Kisheria, mawazo yanayopaswa kujengeka kwanza ni juu ya uelewa mdogo wa mambo ya kisheria kwa watu wa kawaida na ugumu uliopo(kuzingatia uhaba wa wanasheria na gharama za huduma wanazotoa) katika kuwapata wanasheria hasa kufanya kazi ya kuhudumia jamii. Kwa kuzingatia hayo Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ndio kimekuja na wazo la kuanzisha huduma za Usaidizi wa Kisheria. Kimantiki, Usaidizi wa Kisheria ni huduma za Kisheria ambazo zitatolewa na watu wenye uelewa maalum wa kisheria, ingawa wao wenyewe sio wanasheria. Watu hawa wataitwa Wasaidizi wa Kisheria. Watu ambao watafanya kazi za Usaidizi wa Kisheria ni watu ambao watateuliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kutoka katika kila jimbo na kupewa mafunzo maalum ya mambo ya sheria ambayo yatawawezesha kufanya kazi za Usaidizi wa Kisheria. 1.1.3 Sifa za Wasaidizi wa Kisheria Watu ambao wanafaa kuteuliwa kwa ajili ya kazi ya Usaidizi kisheria ni watu ambao wameamua kuitumikia jamii na wameweka juhudi zao katika kuhakikisha jamii inapiga hatua za kimaendeleo. Wasaidizi wa Kisheria wanapaswa wawe ni watu waaminifu na ni vyema wawe tayari wamejijengea heshima na kukubalika katika jamii kutokana na uaminifu wao na msimamo wao katika kusaidia jamii. Pia wawe ni watu wenye kuheshimu haki za binadamu, na wawe na elimu isiyopungua kidato cha nne(Form IV). Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 3 Watu wa aina hiyo, baada ya kuteuliwa na kupata mafunzo maalum yanayohitajika, ndio wanapaswa kufanya kazi za Usaidizi wa Kisheria. Watu hao sio lazima wawe na elimu ya mambo ya sheria, kabla ya mafunzo watakayopewa. Kinachohitajika ni mtu mwenye uwezo wa kuelewa mambo, mwenye ridhaa ya kuitumikia jamii na awe yupo tayari kujifunza kwa ajili hiyo. Pia wasiwe ni watu ambao wamejikita sana katika masuala ya siasa ili watu wasishindwe kutumia huduma zao kwa kuhofia misimamo yao kisiasa. 1.1.4 Kazi za Usaidizi wa Kisheria Kazi za Usaidizi wa Kisheria ni muhimu sana katika jamii. Upeo wa kazi za Usaidizi wa Kisheria unaanzia kwa juhudi za makusudi za Msaidizi wa Kisheria kuamsha hisia za wanajamii ili waweze kuona haja ya kujua haki zao. Baada ya Jamii au wanajamii kuhamasika na kupenda kujua haki zao, ni kazi ya Msaidizi wa Kisheria kuwa tayari wakati wo wote kutoa mafunzo juu ya taaluma ya sheria. Na pale endapo kuna mtu ameonyesha kuwa na tatizo juu ya suala lolote linalohusu haki yake kisheria, au ana tatizo juu ya hatua za kuchukua katika kufuatilia upatikanaji wa haki yake, basi ni jukumu la Msaidizi wa Kisheria kuhakikisha kuwa anamsaidia mtu huyo kadiri inavyowezekana, kulingana na tatizo liliopo. Mara nyingi Msaidizi wa Kisheria anategemewa kumuelekeza mtu mwenye tatizo la kisheria mahali ambapo anaweza kupata ufumbuzi wa tatizo lake, iwe Mahakamani au kwenye taasisi au mtu mwingine mwenye mamlaka ya kiutendaji au mwenye uwezo wa kulishughulikia tatizo lake moja kwa moja, kwa mfano wakili( advocate). Msaidizi wa Kisheria pia ana nafasi kubwa ya kuweza kuisaidia jamii husika kwa ujumla kwa kuelekeza jambo ambalo jamii inaweza kufanya ili iondokane na tatizo la kisheria ambalo lipo katika jamii. Kwa sababu hii ni muhimu sana Msaidizi wa kisheria awe anatoka katika jamii anayoitumikia ili awe na uelewa mzuri zaidi wa mambo yanayohusu jamii husika na mazingira yake. 4 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Kwa ujumla kazi za Msaidizi wa Kisheria ni pamoja na:(i). Kutoa elimu ya sheria kwa umma katika njia tofauti. Lengo ni kupigania kuongeza uelewa wa sheria( Legal Literacy) katika jamii; (ii). Kuwaelekeza watu sehemu ambazo wataweza kwenda na kupata ufafanuzi wa matatizo ya kisheria; (iii). Kusaidia utatuzi wa migogoro ya kisheria kwa njia ya ushauri; (iv). Kuwashajiisha wana-jamii kujenga utashi wa kujua haki zao na namna ya kuziendea au kuzishughulikia (v). Kufuatilia matokeo mbali mbali ya ukiukwaji wa haki za binadamu na kutoa taarifa kituo cha Huduma za Sheria; (vi). Kutoa ushauri unaohitajika katika jamii; na (vii). Kutoa taarifa kwa kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar juu ya kazi zao. Msaidizi wa Kisheria anategemewa kuwa ni kichocheo cha jamii kuelewa mambo ya msingi kuhusu sheria na namna inavyofanya kazi katika jamii. Elimu hiyo inategemewa pia kuwawezesha wanajamii kujenga ujasiri wa kudai haki zao baada ya kuzielewa. 1.1.5 Changamoto Juu ya Mpango Wenyewe Sensa ya Watu na Makaazi ya 1988 inaonyesha kuwa mnamo 1988 idadi ya Watu Zanzibar ilikuwa ni 640,675. Miaka kumi na nne baadae mnamo 2002, sensa imeonyesha kuwa idadi ya watu imeongezeka na kufikia 981,754. Watu 593,031 kati ya hao ± takribani nusu ya watu wote wanaishi vijijini. Hali halisi ya maisha ya Watu wanaoishi Vijijini Zanzibar ni masikini na wengi wao wana elimu duni au wamekosa elimu kabisa. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 5 Idadi kubwa ya watu wasiojua kusoma wala kuandika wanaishi Zanzibar vijijini. 1.1.6 Haja ya Kuwepo Mpango wa Usaidizi wa Kisheria Zanzibar ni nchi changa inayoendelea. Sifa moja kubwa ya nchi kama Zanzibar ni kuwa na mazingira yanayobadilika mara kwa mara kutegemea mabadiliko yanayotokea katika jamii. Baadhi ya mabadiliko hayo chimbuko lake ni jamii yenyewe, lakini yapo pia mabadiliko yanayozikumba nchi changa kama athari ya moja kwa moja ya mambo yanayotokea sehemu nyingine duniani. Kama ilivyo katika jamii nyingine, mabadiliko yote haya tunayoyataja yana nafasi na athari zake katika jamii ya Wazanzibari. Kila jamii ina namna maalum ya mambo yake yakiwemo mahusiano kati ya watu wake, matarajio yao na pia matatizo yao. Katika kuhakikisha kuwa jamii ina maendeleo endelevu ni lazima kila jamii iwe na taratibu zake za kisheria na zisizo za kisheria. Kwa sababu taratibu hizi ndio zinahusu maisha ya watu ya kila siku, basi ni dhahiri kuwa uelewa wa taribu hizo ni muhimu kwa maisha ya kila mtu. Taratibu zinazohusu maisha ya watu zipo za aina nyingi; nyingine ni rahisi kwa mtu wa kawaida kuzielewa, lakini nyingine ni kinyume chake. Taratibu nyingine, na hasa zile za kisheria, zinahitaji watu wenye elimu ya kisheria kuweza kujua haki ya mtu katika mazingira fulani, lakini pia kuweza kujua ni namna gani anaweza kuipata haki ambayo tayari amefahamu kuwa anayo. Mengi kati ya mambo ya kisheria yanahitaji upeo wa juu wa uelewa ili mtu aweze kuyafahamu, na hasa kuweza kuyafanyia kazi. Kwa mantiki hii, ni wazi kuwa wengi wa Wazanzibari na hasa wanaoishi vijiji ambao elimu zao zimeishia msingi na kati, au wamekosa elimu kabisa, sio rahisi kuweza kuelewa ufundi wa Kisheria na kuweza kujua haki zao au namna ya kuzipata. Tatizo linakuwa ni kubwa 6 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: zaidi pale ambapo haki ambayo mtu huyo anapaswa kudai imeshikiliwa na watendaji wa vyombo vya umma ambao wana uelewa na ufundi zaidi ya ule wa watu wa kawaida. Hali inakuwa ni mbaya zaidi katika nchi kama Zanzibar ambayo ni changa katika medani za kidemokrasia. Itakumbukwa kuwa mikakati ya upanuzi wa wigo wa kidemokrasia na utawala bora ilianza kuwekwa bayana Tanzania(ikiwemo Zanzibar) mnamo 1992. Katika hali kama hii Mzanzibari wa kawaida angeweza kutegemea msaada wa kitaalamu wa kisheria ili aweze kujua:(i). Sheria inasemaje kuhusu haki, kama anayo; (ii). Ni vipi anaweza kupata haki hiyo. Lakini ni Wazanzibari wangapi hasa wanaoishi vijijini na ambao wamegubikwa na umaskini, wanaweza kumpata mtaalamu wa kisheria wa kuwapa angalau kwa ushauri. Na wale ambao wamebahatika kujua kuwa wanayo haki katika mazingira fulani, ni wangapi kati yao wanaweza kumlipa wakili wa kuwasaidia katika kupigania haki zao. Jibu rahisi kwa maswali yote haya ni kuwa haiwezekani kwa hali halisi za Wazanzibari walio wengi kumudu kulipia huduma za Kisheria. Mpango wa Usaidizi wa Kisheria umebuniwa makusudi na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar( Zanzibar Legal Services Centre) ili kukidhi matakwa ya Wazanzibari walio wengi(hasa walioko vijijini) ya kufunua zaidi uelewa wao wa mambo ya sheria na kuwasaidia katika kuyapatia ufumbuzi matatizo yao ya kisheria, angalau kwa kuwaelekeza namna ambazo haki zao zinaweza kupatikana. Lengo halisi la Kituo cha Huduma za Sheria katika mpango huu, ni kusaidia kujenga jamii yenye mwamko zaidi wa deokrasia na utawala unaoedeshwa kwa mujibu wa sheria. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 7 1.1.7 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar na Wazo la Kuwepo Usaidizi wa Kisheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar ni Jumuiya isiyo ya Serikali na ambayo imesajiliwa kutoa huduma bila faida yoyote binafsi kama Jumuiya. Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kina malengo makubwa manne:(i). Kutoa elimu ya mambo ya sheria kwa umma ili kuinua uelewa wa watu juu ya haki na wajibu wao kwa mujibu wa sheria; (ii). Kufanya utafiti na kusaidia kufanyika kwa utafiti katika mambo ya kisheria Zanzibar; (iii). Kusaidia kutoa huduma za kisheria na ushauri wa kisheria hasa kwa watu wenye maisha duni ikiwa ni pamoja na kuwawakilisha mahakamani na katika ngazi nyingine za mazungumzo ya kisheria, na pia kutoa huduma za ushuhuda unaotakiwa kufanyika kwa mujibu wa sheria; na (iv). Kuendesha makongamano, warsha na semina kwa lengo la kuwakutanisha wataalamu wa fani tofauti kujadili na kufanya maamuzi juu ya sera kwa lengo la kuinua taaluma ya sheria, na pia kuanisha na kusimamia mipango ya kielimu kwa lengo la kuelimisha mtu mmoja mmoja na vikundi vya watu ambao watafaidika na elimu itakayopatikana na hivyo kufanya maisha ya watu kuwa ni bora zaidi. Katika kutafakari majukumu haya ambayo Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kimejipangia na kwa kuzingatia uelewa mdogo wa watu wa Zanzibar(hasa walioko vijijini) juu ya mambo ya kisheria, Kituo kimeamua kuanzisha huduma hii ya Usaidizi wa Kisheria Zanzibar 8 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 1.1.8 Nafasi ya Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar Katika Usaidizi wa Kisheria Mpango huu wa Usaidizi wa Kisheria umebuniwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar. Tumeona hapo nyuma kuwa miongoni mwa malengo ya Kituo ni kuinua uelewa wa Sheria katika jamii na kutoa msaada wa huduma za kisheria. Kwa maana hiyo, Mpango huu wa Usaidizi wa Kisheria umeandaliwa na Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar katika kutekeleza malengo yake kama taasisi. Katika kutekeleza Mpango huu, Kituo tayari kimejizatiti kutafuta watu wanaofaa kufanya kazi za Usaidizi wa Kisheria kulingana na sifa zilizotajwa sehemu nyingine hapo juu. Kituo kitateuwa mtu mmoja kutoka kila jimbo kwa majimbo yote 50 ya Uchanguzi Zanzibar. Wale watakaobahatika kuteuliwa watapata mafunzo ya msingi ya sheria ambayo yatawawezesha kufanya kazi ya Usaidizi wa Kisheria. Mafunzo hayo, ambayo kwa awali yatatolewa kwa wiki mbili mfululizo yatadhaminiwa na Kituo cha Huduma za Sheria, Zanzibar. Baada ya mafunzo hayo, watarudi kwenye majimbo yao kwa ajili ya kuanza kazi zao za Usaidizi wa Kisheria. Katika siku za awali Wasaidizi wa Kisheria watafanya kazi zao chini ya uongozi wa karibu zaidi wa Kituo. Kituo kitateuwa watu miongoni mwa Wanasheria wazoefu na kuwapangia muda wa kuwatembelea Wasaidizi wa Kisheria waliopo kazini ili kuweza kujua matatizo yao na kuwasaidia. Baada ya kipindi cha miezi mitatu ya kwanza Kituo kitaandaa mafunzo mengine ya Wasaidizi wa Kisheria. Lengo ni kuweza kutathimini utendaji wao, na wao wenyewe kuwapa nafasi ya kujipima iwapo elimu waliyoipata imeweza kusaidia katika kupunguza matatizo ya jamii. Pia wataweza, kwa njia ya kubadilishana uzoefu, kuona endapo kuna matatizo au makosa Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 9 ambayo yalijitokeza katika utendaji wa shughuli zao, kwa lengo la kuyatafutia ufumbuzi. Shughuli zote hizo zitafanyika chini ya uongozi na Udhamini wa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar. Kutokana na tathmini ambayo itafanywa baada ya kipindi hicho cha miezi mitatu ya awali ya kazi ya Usaidizi wa Kisheria, Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar kitazingatia ni msaada au huduma gani muhimu inahitajika wakati huo ili kuendeleza mpango huu wa Usaidizi wa Kisheria hapa Zanzibar. 1.1.9 Vitendea Kazi vya Wasaidizi wa Kisheria Mafunzo yatakayoendeshwa kwa Wasaidizi wa Kisheria yameandaliwa makusudi na mahususi ili kuwajengea uwezo wa kufanya kazi wanazohitajika kuzifanya. Mafunzo yenyewe yanaendeshwa kwa kutumia muungozo wa sheria mbali mbali uliotarishwa kwa ajili hiyo pamoja na sheria mbali mbali. Muongozo huo unaelezea kwa lugha rahisi mambo ya msingi ambayo mtu ambaye hana elimu ya sheria ataweza kuelewa kuhusu sheria za nchi na kazi zake katika jamii. Mbali ya kuzungumzia dhana ya sheria kwa ujumla makala hizi zinazotoa mafunzo ya msingi ya kazi ya Usaidizi wa Kisheria. Makala hizi zimezingatia na kuelezea sheria mbali mbali juu ya mambo yanayoonekana ni muhimu zaidi katika jamii ya Wazanzibari. Makala hizi zilizotayarishwa kwa ufupi sana zitakuwa ni vitendea kazi vya msingi kwa Wasaidizi wa Kisheria. Pia zipo makala nyingine juu ya baadhi ya mada hizo hizo ambazo zimetayarishwa kwa urefu zaidi kutoa mwanga wa upeo mkubwa zaidi kwa Wasaidizi wa Kisheria na watu wengine ambao wanapenda kujua zaidi kuhusu taaluma ya kisheria. 10 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Sehemu ya Pili 1.2.0 Katiba za Nchi na Misingi Muhimu Iliyomo 1.2.1 Utangulizi Kwa mujibu wa Ibara ya 2(1) ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, na kifungu cha 1 cha Katiba ya Zanzibar 1984, Zanzibar ni sehemu ya Jamhuri ya Muungano. Kiutawala kuna mambo ndani ya Zanzibar yanayoendeshwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano, na yapo mambo yanayoendeshwa kwa mujibu wa Katiba ya Zanzibar. Kwa maana hiyo, ili mtu aweze kuelewa vyema utawala wa Kikatiba kwa Zanzibar anapaswa aelewe kuhusu maamrisho muhimu ya Katiba zote mbili. 1.2.2 Maana ya Katiba Katiba ni taratibu za msingi zinazotumika kuweka masharti juu ya mahusiano ya watu na mambo yao muhimu katika kundi au jamii Fulani. Katiba inaweza kuwa ya familia, kikundi cha ngoma, klabu ya mpira, jumuiya isiyo ya serikali, chama cha siasa, katiba ya nchi, n.k. taratibu za msingi kabisa ambazo kikundi cha watu iwe nchi, chama cha hiari, n.k, kimejiwekea katika kuhakikisha kuwa kundi hilo linaendelea kuwepo na malengo yake yanapatikana. Ikitokea kuwa kundi la watu wenye Katiba wanabadilisha mwelekeo au malengo yake, basi katiba ya kundi hilo inapaswa kubadilika ili kuhakikisha mambo yanayokusudiwa kufanyika yanafanywa kwa mujibu wa Katiba. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 11 Kutokana na utangulizi huo tunaweza kuelezea kuwa Katiba ya nchi maana yake ni maamrisho maalum ya msingi yenye nguvu za kisheria yanayounda vyombo au ngazi tofauti za kiutawala ambazo ni muhimu katika kuendesha nchi, na kuziwekea kazi zake na pia kuweka taratibu muhimu za kufuatwa katika utendaji kazi wa vyombo hivyo na taratibu nyingine muhimu kuhusu maisha ya watu. Ni yale masharti au maamrisho ya msingi tu ambayo yanategemewa kuingia katika sheria ya nchi. Maarisho mengine yanayopaswa kutungiwa sheria yanatungiwa sheria nyingine kulingana na matakwa ya nchi au jamii inayohusika. Hali hii inatokana na sababu halisi kuwa haiwezekani masharti au maamrisho yote yanayohitajika kuendesha nchi yawekwe katika kitabu kimoja tu kinachoitwa Katiba. Lazima ziwepo sheria nyingine. 1.2.3 Katiba ni Sheria Mama Katiba ni sheria, kwa maana kuwa ina nguvu za kisheria. Lakini nguvu za kisheria ambazo Katiba inazo ni tafauti na nguvu za kisheria ziliopo katika sheria nyingine. Tumeona hapo juu kuwa Katiba ya nchi ndio inaunda vyombo au tasisi muhimu katika kuendesha utawala wa nchi, pia inaelezea kazi za vyombo hivi na mipaka yake, na pia taratibu za msingi za kufuatwa katika utendaji kazi wa vyombo hivyo. Kwa maana hiyo, taasisi muhimu zinazotumika kuendesha nchi huwa zipo kwa mujibu wa Katiba na kufanya kazi zake kwa mujibu wa masharti ya Katiba. Na endapo chombo au taasisi yoyote imefanya jambo au kazi nje ya uwezo ilionao kwa mujibu wa Katiba, au imefanya kitu bila kufuata taratibu zilizowekwa kwa mujibu wa Katiba, basi jambo hilo au kazi hiyo iliyofanywa kinyume na Katiba itakuwa ni batili kwa kiasi ambacho maamrisho ya Katiba yamekiukwa. Na hivyo ndivyo ilivyo hata kwa Sheria zinazotungwa na Bunge au Baraza la Wawakilishi. Endapo Sheria zinakiuka mipaka ya kikatiba basi Sheria hizo zinaweza kutangazwa na Mahakama kuwa ni batili kwa kiasi 12 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: mamlaka za kuendesha nchi nguvu zao na pia uhalali wa matendo yao kunategemea maamrisho ya Katiba. 1.2.4 Historia Fupi na Misingi Muhimu ya Kikatiba 1.2.4.1 Historia Fupi Baada ya kuelewa maana ya Katiba na hadhi yake, Msaidizi wa Kisheria anapaswa kujua historia na maamrisho muhimu yaliyomo ndani ya katiba zetu mbili, Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, na Katiba ya Zanzibar, 1984. Tanzania ni jina lililopatikana baada ya kuunganisha Jamhuri mbili(Jamhuri ya Tanganyika na Jamhuri ya watu wa Zanzibar). Muungano huo ulifanyika tarehe 26/04/1964. Wakati wa Muungano, Tanzania Bara(Wakati huo ikiitwa Tanganyika) ilikuwa inaendeshwa kwa mujibu wa Katiba ya Jamuhuri ya Tanganyika ya 1962 na Zanzibar ilikuwa na Sheria ya Katiba ya 1964( Constitutional Decree). Hata hivyo hizi hazikuwa Katiba za kwanza katika historia ya nchi hizi mbili. Katiba ya kwanza ya Tanganyika ilikuwa ni Katiba ya Tanganyika 1961, na kwa upande wa Zanzibar, kabla ya Mapinduzi matukufu ya 1964 ilikuwepo Katiba ya Uhuru ya mwaka 1963. Kufuatia Muungano wa Tanganyika na Zanzibar mnamo 1964, ilipitishwa Katiba ya Mpito ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania(i.e. Tanzania Interim Constitution) ya 1965. Katiba hiyo iliitwa ya mpito kwa sababu tokea mwanzo ilikusudiwa kutumika kwa muda tu wakati Katiba ya kudumu ya Jamhuri ya Muungano inatayarishwa. Hatimae jopo la Wataalamu kutoka Tanzania Bara na Zanzibar ambao walipewa kazi ya kubuni Katiba mpya walimaliza kazi yao, na mnamo mwaka 1977 Katiba ya Kudumu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ilipitishwa. Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 13 (pamoja na kufanyiwa marekebisho mara kwa mara) ndio ambayo inatumika hivi sasa katika kuendesha mamlaka ya Jamhuri ya Muungano. Kwa upande wa Zanzibar, pamoja na kutumika kwa Katiba ya Jamhuri hapa Zanzibar kwa mambo yanayosimamiwa na Mamlaka za Jamhuri ya Muungano, kuna mambo ambayo yalihitaji kuwepo Katiba ya Zanzibar. Mnamo mwaka 1979 Zanzibar ilifuta ile Sheria ya Katiba ya 1964 na kuweka Katiba ya Zanzibar ya 1979 kutokana na mabadiliko mengi(kijamii kiuchumi na kisiasa) yaliyojitokeza Zanzibar baada ya kupitisha hiyo Katiba ya Zanzibar ya 1979, Zanzibar iliamua kupitisha katiba nyingine. Wazo hili lilitekelezwa mnamo 1984 ambapo Katiba ya Zanzibar 1984 ilipitishwa rasmi. Pamoja na marekebisho ambayo yamewahi kufanywa mara kwa mara kwenye Katiba hiyo, Katiba ya Zanzibar ya 1984 ndio ambayo inatumika hivi sasa katika kuanzisha na kuendesha mamlaka za Zanzibar, ikiwa ni sehemu ya Tanzania. 1.2.4.2 Misingi Muhimu ya Kikatiba Katika sehemu hii tunaangalia, ingawa kwa ufupi, yale mambo ambayo maamrisho yake yanapatikana katika Katiba zetu mbili, yaani Katiba ya Jamhuri ya Muungano 1977(kama ilivyorekebishwa) na Katiba ya Zanzibar 1984(kama ilivyorekebishwa). Tunapozungumzia maamrisho au maamuru ya kikatiba huwa tunamaanisha aidha vyombo muhimu vilivyoundwa kikatiba na upeo au mipaka ya nguvu zao za utendaji, kwa upande mmoja, au kwa upande mwingine, huwa tunazungumzia taratibu za msingi za kikatiba( basic constitutional principles) ambazo zinatumika kuendesha mamlaka za nchi. Katika sehemu hii tunazungumzia kwa kifupi taratibu hizi za msingi. Taratibu zenyewe ni juu ya:- 14 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: (i). Haki za Binadamu na Wajibu wa Raia; (ii). Mgawanyo wa Madaraka; (iii). Utawala wa Sheria; na (iv). Uhuru wa Mahakama. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 15 Sehemu ya Tatu 1.3.0 Sheria Mbali Mbali 1.3.1 Sheria ya Tawala za Mikoa Sheria ya Tawala za Mikoa(Namba 1) ya 1998 ndiyo Sheria ya Zanzibar inayosimamia ugawaji wa Zanzibar katika mamlaka ndogo ndogo za kuitawala kadri ya mikoa, wilaya na mamlaka nyingine. Chini ya Kifungu cha 3 cha Sheria ya Tawala za Mikoa, Rais wa Zanzibar, kwa kushauriana na Rais wa Jamhuri ya Muungano, ndiye mwenye madaraka ya kuigawa Zanzibar katika mamlaka ndogo ndogo za kiutawala kadiri ya mikoa, wilaya na mamlaka nyingine za kiutawala kama atakavyoona inafaa. 1.3.1.1. Mamlaka ya Mikoa Rais wa Zanzibar ana madaraka chini ya Kifungu cha 4(1) cha Sheria ya Tawala za Mikoa, kumteua Mkuu wa Mkoa kwa kila Mkoa uliopo ndani ya Zanzibar. Kazi za Mkuu wa Mkoa zimeelezwa chini ya kifungu cha 5 cha Sheria ya Tawala za Mikoa kuwa ni:(i). Kuangalia, kusimamia na kusaidia katika utendaji wa shughuli za Serikali ndani ya Mkoa wake; (ii). Kuhakikisha kuwa Sera, mipango na maelekezo ya Serikali yanafuatwa; (iii). Kusimamia amani na utawala wa Sheria katika Mkoa wake kwa kushirikiana na vyombo vya ulinzi; na (iv). Kuhakikisha kuwa nyenzo za Serikali(ambazo ni vifaa au mali na Watu) zinatumika ipasavyo kwa maendeleo ya kiuchumi na kijamii. 16 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Aidha katika kuhakikisha hali ya amani na usalama katika Mkoa wake, Mkuu wa Mkoa ana uwezo wa kumkamata na kumuweka kuzuizuini mtu yeyote au kuamrisha Polisi kwa maandishi kumkamata mtu yeyote na kumuweka kizuini, endapo kuna ushahidi kuwa mtu huyo anavunja amani au anaelekea kusababisha uvunjaji wa amani na utulivu na kwamba hali hiyo haiwezi kuzuilika mpaka mtu huyo ambaye ni sababu ya uvunjifu huo wa amani na utulivu amekamatwa na kuwekwa kizuizini. Chini ya Kifungu cha 6(2) na (3) mtu ambaye atakamatwa kwa amri ya Mkuu wa Mkoa ana haki ya kuelezwa sababu za kukamatwa na kuwekwa kizuizini. Pia, kwa vyovyote vile mtu huyo hatawekwa kizuizini kwa muda wa zaidi ya masaa 48 mfululizo bila kufikishwa mahakamani. 1.3.1.2 Mamlaka ya Wilaya Kwa mujibu wa Kifungu cha 4(2) cha Sheria ya Tawala za Mikoa 1998, Rais wa Zanzibar atateua Mkuu wa Wilaya katika kila Wilaya ya Zanzibar. Mkuu wa Wilaya atatekeleza ndani ya Mkoa wake yale majukumu ambayo Mkuu wa Mkoa anayatekeleza chini ya Sheria. (Kifungu 6(5) na 7 vya Sheria Namba 1 ya 1998). 1.3.1.3 Mamlaka ya Shehia Kwa mujibu wa Sheria Namba 1 ya 1998, mbali ya mamlaka ya Mikoa na Wilaya limetafsiriwa kwenye Kifungu cha 2 cha Sheria hii kuwa ni eneo lote ambalo hapo awali lilikuwa ni eneo la Tawi la Chama cha Mapinduzi au eneo jengine lolote ambalo litatengwa na mamlaka kwa ajili hiyo. Hata hivyo haikuelezwa ni mamlaka gani yenye madaraka ya kufanya utengaji huo. Chini ya kifungu 15 cha Sheria ya Tawala za Mikoa, Wakuu wa Mikoa(wakishauriwa na Wakuu wa Wilaya) ndio watawateuwa masheha. Sheha atateuliwa miongoni mwa watu wa shehia inayohusika. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 17 Kazi za Masheha ni:(i). Kutekeleza Sheria, sera, amri na maelekezo yote ya Serikali kwa ajili ya kuhakikisha utekelezaji wa Sheria na utunzaji wa amani; (ii). Kusululisha na kutatua matatizo yote yanayojitokeza katika jamii kwa kutumia busara, desturi, silka na mila za watu wa eneo linalohusika; (iii). Kuweka kumbu kumbu kuhusu usajili wa ndoa, talaka, vizazi na vifo, vibali vya ngoma, vyeti vya kusafirishia mazao, mifugo mkaa na vyenginevyo kama itakavyoelekezwa na taasisi husika; (iv). Kudhibiti uhamiaji wa watu katika Shehia yake; (v). Kupokea taarifa ya mikutano yote ya hadhara katika eneo lake; na (vi). Kufanya mambo mengine yote ya halali kama ambavyo ataagizwa na Mkuu wa Wilaya yake(Angalia Kifungu 17(1)). Katika kutenda shughuli zake, kila sheha anao uwezo wa kumwita mtu yeyote, na endapo mtu huyo atakataa, anao uwezo wa kutoa hati ya wito ili mtu huyo afike mbele yake au atoe taarifa inayohitajiwa na Sheha. Endapo mtu aliyepewa hati ya wito wa Sheha anakataa kwenda, Sheha anaehusika atapeleka taarifa hiyo kwenye Kituo cha Polisi ambacho kitampeleka mtu huyo kwa Sheha. Hata hivyo, mtu yeyote ambae amekataa wito wa Sheha atakuwa ametenda kosa na akipatika na hatia atatozwa faini isiyozidi Tshs. 10,000. Kwa mujibu wa Kifungu cha 17(7), katika kazi zake Sheha atawajibika kwa Mkuu wa Wilaya yake. Ili mtu aweze kuteuliwa kuwa Sheha ni lazima awe na sifa zifuatazo: (i). awe Mzanzibari; (ii). awe ni mtu mwenye kuheshimika; 18 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: (iii). awe ni mtu mwenye tabia nzuri; (iv). awe na umri usiopungua miaka 40; (v). awe amepata elimu ya msingi na anajua kusoma na kuandika kiswahili na/au Kiingereza; na (vi). awe ameishi kwenye Shehia hiyo kwa muda usiopungua miaka 15. 1.3.2 Sheria ya Jinai Sheria ya Jinai Namba 6 ya 2004 inashughulikia masuala yote yanayohusu makosa ya jinai. Makosa yaliyomo ndani ya Sheria hiyo yamewekwa pamoja na kuifanya Sheria hii kuwa wa kuongoza makosa ya jinai 1.3.2.1 Nini Kosa la Jinai Kosa la jinai maana yake ni makosa yaliyomo ndani ya Sheria hii. Makosa haya yanapofanywa mtu aliyefanya kosa huwa anaadhibiwa na Serikali, ingawa aliyemkosea si Sirekali bali ni raia wa kawaida au chombo chenye hadhi ya kuweza kusimama kisheria. Serikali kwa kupitia polisi hufanya upelelezi kuhusiana na tuhuma zilizoripotiwa polisi kuhusiana na makosa haya ya jinai. Polisi inapogundua kwamba tuhuma hizo ni za kweli humshtaki Mahkamani yule aliyetuhumiwa kutenda kosa. Kesi huendeshwa na Waendesha Mashtaka walioteuliwa na Mkurugenzi wa Mashtaka. Mahakama nayo kwa kufuata taratibu zake husikiliza kesi kwa misingi ya kisheria na baadae humhukumu mtu aliyefanya kosa. Hukumu inaweza kuwa ni faini, kutumikia chuo cha mafunzo, au kuitumikia jamii. Faini hupokelewa Mahakamani, bali kutumikia chuo cha mafunzo na kuitumikia jamii husimamiwa na Idara ya Chuo cha Mafunzo kama tutakavyoona tutakapozugumzia Idara Maalum. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 19 1.3.2.2 Tofauti kati ya Makosa ya Jinai na Makosa ya Madai Tofauti kubwa iliyopo kati ya makosa ya jinai na madai ni kwamba katika kosa la jinai Serikali ndiyo inayoshtaki kwa niaba ya muathirika wa tendo la jinai, wakati katika kesi ya madai mdai mwenyewe ndie anayeshtaki. Pia adhabu katika kesi ya jinai huwa ni kifungo, faini au kutumikia jamii, lakini katika kesi ya madai mtu huwa anadai fedha, kitu, mali au fidia ya jambo fulani. 1.3.2.3 Ufunguaji wa Kesi ya Jinai Kesi ya jinai hufunguliwa na Serikali dhidi ya mtu anayetuhumiwa kutenda kosa la jinai. Mtu aliyeathirika na kitendo hicho au mtu aliyeshuhudia tendo hilo likitendeka ana wajibu wa kuripoti tukio hilo katika kituo cha polisi, na polisi hulishughulikia suala hilo katika hatua zifuatazo: (i) huchukua maelezo ya walalamikaji/mlalamikaji; (ii) huchunguza ukweli wa lalamiko hilo; (iii) humkamata mtu anayetuhumiwa kutenda kosa hilo; na (iv) humpeleka Mahakamani na kumfungulia shtaka mtu huyo; 1.3.2.4. Makosa ya Jinai Makosa ya jinai yanaweza kugaiwa katika aina mbali mbali kutegemeana na maudhui yanayozungumzwa. Yapo makosa ya jinai ambayo mtuhumiwa anaweza kukamatwa bila ya mkamataji kuwa na hati ya kukamatia; makosa haya ni yale yanayotendeka waziwazi kama wizi, ujambazi, mauaji nk. Pia yapo yanayohitaji hati ya kukamatia ili uweze kumkamata mtuhumiwa kwa mfano kosa la kula njama, udanganyifu, nk. Kwa yale makosa yasiyohitaji hati ya kukamatia hata mtu wa kawaida anaweza kumkamata mtuhumiwa na kumuweka chini ya ulinzi. Lakini anatakiwa amkabidhi haraka iwezekanavyo kwa vyombo vinavyohusika. Vile vile makosa ya 20 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: jinai yapo yanayopewa dhamana na yasiyopewa dhamana. Makosa yasiyopewa dhamana ni kama kuua kwa makusudi, uhaini na ujambazi wa kutumia silaha. Katika Sheria ya jinai makosa ya jinai yamegaiwa katika makundi mbali mbali. Makundi hayo ni kama yafuatayo: (i). Makosa yanayohusiana na uhaini au yaliyo dhidi ya Serikali ambayo yamo ndani ya Sehemu ya 7; (ii) Makosa yanayohusiana na uhusiano na nchi za kigeni ambayo yamo ndani ya Sehemu ya 8; (iii). Makosa yanayohusiana na kufanya mikusanyiko isiyohalali, fujo na makosa mengine yanayohatarisha amani ambayo yamo ndani ya Sehemu ya 9; (iv). Makosa ya rushwa, utumiaji mbaya wa ofisi za umma na makosa yanayohusiana na uchumi yamo ndani ya Sehemu ya 10; (v). Makosa yanayohusiana na utoaji wa haki Mahakamani, kama vile kutoa maelezo ya uongo, kupandikiza ushahidi, kuwafanya mashahidi waseme uongo, n.k. ambayo yamo ndani ya Sehemu ya 11; (vi). Makosa yanayohusu kukimbia kutoka katika vyombo vya Sheria na kuwazuia maafisa wa Mahakama kufanya kazi zao ambayo yamo ndani ya Sehemu ya 12; (vii). Sehemu ya 13 imeainisha makosa mengine dhidi ya Serikali kama udanganyifu, uzembe kazini, kutotii amri halali na kusababisha hasara kwa Serikali; (viii). Sehemu ya 14 inahusiana na makosa yanayokwenda kinyume na dini; (ix). Sehemu ya 15 inahusiana na makosa ya kujamiiana ambayo yatazungumzwa baadae; Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 21 (x). Sehemu ya 16 inahusiana na makosa ya ndoa na majukumu ya nyumbani; (xi). Sehemu ya 17 inahusiana na makosa dhidi ya afya ya jamii, pamoja na karaha zinazotokea katika jamii; (xii). Sehemu ya 18, 19, 20 na 21 inahusiana na makosa ya mauaji, na yale yenye kuhatarisha maisha au afya; (xiii). Sehemu ya 22 inahusiana na makosa yanayofanywa na vigengi vya wahalifu; (xiv). Sehemu ya 23 inahusiana na makosa ya uzembe na dharau iliyokithiri; (xv). Sehemu ya 24 inahusiana na makosa ya kuingilia katika mwili wa mtu mwingine; (xvi). Sehemu ya 25 inahusiana na makosa ya utekaji nyara na uzuiaji wa uhuru wa mtu; (xvii).Sehemu ya 26, 27, 28, 29, 30, 31 na 32 zinahusiana na makosa ya wizi, ujambazi, unyanganyi, uvunjaji wa majumba, utapeli, udanganyifu na kupokea mali za wizi; (xviii). Sehemu ya 33 inahusiana na makosa yanayotokana na mali; (xix). Sehemu ya 34, 35, 36, 37, 38, 39, 40 na 41 zinahusiana na makosa ya kughushi, sarafu, makosa yanayotokana na komputa, haki ya biashara, pamoja na rushwa; na (xx). Sehemu ya 42, 43, na 44 zinahosusiana na kosa la kujaribu kutenda kosa, kushiriki katika njama za kufanya kosa na mtu aliyeshiriki katika kufanya makosa. 22 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 1.3.2.5 Makosa ya Kujamiana Sheria ya makosa ya kujamiiana ambayo sasa ni sehemu ya Sheria ya Jinai Namba 6 ya 2004 imejaribu kuwalinda wanawake na watoto kutokana na makosa hayo. 1.3.2.5.1 Kubaka Kosa hili hufanyika pale mwanamme anapomuingilia mtoto wa kike au mwanamke katika mazingira yafuatayo: (i). bila ya ridhaa ya mwanamke ikiwa mwanamke huyo si mke wake; (ii). kwa ridhaa ya mwanamke ikiwa ridhaa hiyo inatokana na utumiaji wa nguvu na vitisho, na ikiwa mwanamke huyo yupo katika hofu ya kuuawa au kuumizwa; (iii). kwa ridhaa ya mwanamke ikiwa mwanamke huyo yupo katika kifungo kisichokuwa halali; (iv). kwa ridhaa ya mwanamke wakati mwanamme anajua kwamba mwanamke hayupo timamu au yupo katika hali ya ulevi unaotokana na pombe, madawa au chenginecho alichopewa na mwanamme huyo au mtu mwengine; (v). kwa ridhaa ya mwanamke ikiwa amefanywa aamini kwamba mwanamme huyo ni mume wake; na (vi). ikiwa ipo ridhaa au hapana endapo mwanamke atakuwa chini ya umri wa miaka 18 isipokuwa kama ni mkewe. Katika kuthibitisha kubaka uingizaji wa uume unatosha, na si lazima kuwepo kwa manii au vitu vingine. Pia si lazima kuwepo kwa ushahidi wa kupinga kubakwa- kama vile michubuko ya mwilini siyo ya lazima katika kuthibitisha au kutothibitisha kuwa mwanamke aliridhia au la. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 23 Sheria pia imeweka kosa la kubaka kwa kikundi(mdondo) na imeeleza kwamba kila mtu aliyefanya au kusaidia ubakaji huo atachukuliwa kuwa amebaka, na atahukumiwa bila ya kuangalia kitendo gani alifanya katika ubakaji huo au kama ni mwanamme au mwanamke. 1.3.2.5.2 Uvunjaji wa Heshima na Udhalilishaji wa Kijinsia Sheria imeweka kuwa ni kosa la uvunjaji wa heshima kwa mtu kutumia maneno, sauti, ishara, au kuonyesha kitu akiwa na nia kionekane au kisikilizwe na mwanamke au mtoto wa kike au kumuingilia kwenye faragha yake kwa madhumuni ya kumkashifu. Pia imeweka kosa la udhalilishaji wa kijinsia pale mtu: (i). anapomkashifu kijinsia kwa kutumia nguvu; (ii). anapomdhalilisha kijinsia kwa kutumia maneno au vitendo vinavyopelekea aibu; (iii). anapotumia sauti, ishara, au kuonyesha kitu au kiungo kwa kumkashifu mtu; na (iv). kutoa maneno/ujumbe unaoashiria ngono kwa mtu mwenye mamlaka, ikijumuisha sehemu ya kazi. Kesi inayohusu udhalilishaji wa kijinsia lazima ifunguliwe si zaidi ya siku 180 tokea kosa lilipotendeka. 1.3.2.5.3. Makosa yanayowahusu Watoto Sheria pia imewalinda watoto kwa kuweka wazi makosa yanayowahusu kama vile kuwatorosha, kuwanajisi na kuwalawiti watoto. Mtu atakayemtorosha mtoto adhabu yake ni kifungo cha miaka 3, na yule atakayemnajisi au kumlawiti mtoto wa kike au kiume adhabu yake ni kifungo cha maisha(sawa na mtu aliyebaka). Pia Sheria imeainisha kuwa ni kosa kumuingilia kimwili mtu mwenye akili taahira, na inakataza wanaume na wanawake kuingia katika ukahaba. 24 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Ili kulinda utu wa waathirika wa makosa ya kujamiiana Sheria imeweka kuwa ni kosa kwa mtu kumtaja yule aliyeathirika na makosa haya. Pia imeiipa uwezo Mahakama kuamuru kuwa mkosaji alipe fidia kwa muathirika kwa kadri mahakama itakavyoona inafaa. 1.3.2.6 Masharti ya Msingi Kuhusu Dhima au Hatia Katika Makosa ya Jinai Sehemu hii inazungumzia baadhi ya masharti ya msingi katika sheria kuhusu dhima au kinga katika makosa ya jinai( responsibility/ liability). 1.3.2.6.1 Kutojua Sheria Moja kati ya dhana za msingi kabisa katika utawala wa sheria ni jinai asionekane kuwa na hatia. Dhana hii inaondoa uwezekano wa mtu kushtakiwa kwa kosa la jinai na kuleta hoja yenye kukubalika kuwa yeye binafsi hajui sheria; na kwa hivyo, alikuwa hajui kuwa alichokuwa anatenda ilikuwa ni kosa la jinai. Jibu la msingi kwa hoja kama hiyo inapotokea ni kuwa kwa sababu jambo ambalo mtu amefanya au ameacha kufanya ni kosa kwa mujibu wa sheria basi jambo hilo litabaki kuwa ni kosa hata kama mtendaji kosa alikuwa hajui kuwa ni kosa. Miongoni mwa hekima zilizotumika katika kuweka sharti hili la kisheria ni kuwa kama sheria ingeruhusu kuwa kutojua sheria ni kinga. Kila mtu anayepelekwa Mahakamani angekuwa na jibu moja kubwa ingewaangukia waendesha mashtaka kuthibitisha kuwa alikuwa anajua kuwa ana kosa. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 25 Kwa mujibu wa Sheria za Zanzibar dhana hii ya kutojua sheria imeelezewa kwenye kifungu cha 7 cha Sheria ya Jinai Namba 6 ya 2004. 1.3.2.6.2 Kutojua Ukweli Kisheria mtu ambaye ametenda au ameacha kutenda jambo lolote,ambalo ni kosa, katika hali ambayo anaamini(ingawa ni kwa makosa) kuwa hakufanya kosa. Mtu huyo hatokuwa na hatia kwa tendo hilo alilofanya au kuacha kufanya. Kwa mfano: Jaalia ni kosa la jinai kuwinda katika msitu wa hifadhi wa Jozani. Selemani amepatikana anawinda katika eneo hilo la msitu. Katika utetezi wake Selemani ameeleza kuwa hakuwa akijua kuwa tayari ameingia katika eneo la msitu wa hifadhi, na kwa hakika hapana jambo lolote linaloashiria kuwa tayari ameshaingia katika msitu wa hifadhi. Kwa mujibu wa Sheria Selemani hatokuwa na hatia. Lakini Selemani hatoweza kutumia utetezi kuwa hakuwa anajua kuwa inakatazwa kisheria kuwinda katika msitu huo kwa sababu utetezi huo haukabiliki kama tulivyokwishaeleza hapo juu. 1.3.2.6.3 Uwezo wa Kuzuia Mali Dai halali la mali linajitokeza pale ambapo mtu mmoja anamdai mwingine kitu chochote chenye thamani, na yule anayedaiwa hajalipa ama amekataa kulipa au ameshindwa kulipa. Katika hali kama hii mtu anayedai anaweza kuzuia mali yoyote ya mtu anayedaiwa au kufanya jambo jengine kuhusiana na mali yoyote ya mtu anaemdai. Kufanya hivyo, haitokuwa kosa la jinai na utakuwa ni utetezi wa kutosha. Vinginevyo, kama si kutokuwepo kwa dai hilo angekuwa amefanya kosa la jinai. 26 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 1.3.2.6.4 Kutokuwa na Akili Timamu Katika kuhakikisha kuwa utetezi wa kutokuwa na akili timamu hautumiwi vibaya na watu waliofanya makosa, sheria imeweka msimamo kuwa kila mtu anachukuliwa kuwa ni mwenye akili, na kwamba ataendelea kuchukuliwa hivyo mpaka pale atakapothibitika tu kuwa ana matatizo ya akili. Hapa inamaanisha kuwa endapo mtu atadai kuwa katika kipindi au tukio fulani alikuwa hana akili timamu, basi jukumu linabaki kuwa ni lake la kuthibitisha kuwa wakati wa tukio yeye hakuwa na akili timamu. Hivyo basi, mtu hatokuwa na hatia ikiwa alipofanya kosa hakuwa na akili timamu na imethibitika kuwa wakati anafanya kosa hilo ama: (i) hakujua anachokifanya, au(ii) hakujua kuwa hakutakiwa kufanya hicho alichofanya kutokana na ugonjwa wa akili. Kwa maana nyingine ni kuwa ugonjwa wa akili sio kinga ya mtu kutopatikana na hatia ya kosa la jinai mpaka pale ambapo ugonjwa huo wa akili umeleta moja kati ya athari mbili zilizoelezwa hapo juu. 1.3.2.6.5 Ulevi Kiujumla kufanya makosa ukiwa umelewa sio kinga ya kutopatikana na hatia ya kosa la jinai. Hata hivyo, katika mazingira fulani mlevi anaweza asiwe na hatia ya kosa alilofanya. Hali yenyewe ni pale ambapo kwanza kutokana na ulevi mtu huyo ama ± (i) hakujua anachokifanya, au(ii) hakujua kuwa hakutakiwa kufanya jambo alilofanya. Pili awe ama ± (i) ulevi huo amekunywa bila ya ridhaa yake, au(ii) kutokana na ulevi huo amekuwa hana akili kabisa (mwenda wazimu) wakati huo wa kutenda kosa(kifungu cha 13). 1.3.2.6.6 Umri Mdogo Zipo hali tatu zinazoelezea kipingamizi cha umri mdogo juu ya kupatikana na hatia kwa mwenye kutenda kosa. Hali zenyewe ni: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 27 (a). Mtoto mwenye umri chini ya miaka 12 ± huyu anatambuliwa kisheria kuwa hana kabisa uwezo wa kutenda kosa la jinai; (b). Mtoto kati ya umri wa miaka 12 na 14 ± huyu kiujumla hawezi kutenda kosa la jinai, isipokuwa endapo wakati wa kutenda kosa alikuwa anajua kuwa hakutakiwa kufanya jambo alilofanya. Hivyo, atakuwa na hatia ya kosa alilofanya; na (c). Mtoto mwanamme chini ya umri wa miaka 14 anachukuliwa kisheria kuwa hana uwezo wa kumuingilia kimwili mwanamke. 1.3.3 Sheria ya Kuwalinda Wari na Watoto wa Mzazi Mmoja Sheria hii Namba 4 ya 2005 imepitishwa kwa lengo la kuwalinda wari kutokana na kupata mimba, na kuwalinda watoto waliozaliwa nje ya ndoa ili wapate matunzo mazuri. Tafsiri ya mwari kwa mujibu wa sheria hii ni mwanamke asiyeolewa ambaye ana umri katika ya miaka 18 na 21 na hajawahi kuzaa. Sheria imeweka wazi kwamba ni kosa kwa mwari kupata mimba kwa makusudi au kwa hiari yake na kosa likithibitika atalazimika kuitumikia jamii kwa kipindi cha miezi 6 ambacho kitaanza baada ya kujifungua. Lakini mwari hatochukuliwa kuwa amepata mimba kwa hiari ikiwa mimba hiyo inatokana na kubakwa(ikiwa kubakwa huko kumeripotiwa au la) au ikiwa tendo hilo la ngono lililosababisha mimba amelifanya kwa kutezwa nguvu au kwa namna ambayo alitenda bila ya kuwepo ridhaa yake. Mtu yeyote atakayethibitika na kosa la kumpa ujauzito mwari atahukumiwa kutumikia chuo cha mafunzo kwa muda usiopungua miaka 3 na usiozidi miaka 5. Mtu huyo pia atatakiwa atoe matunzo kwa mtoto aliyezaliwa. Lakini ikiwa aliyefanya kosa hilo ni mwanafunzi wa kiume mwenye umri usiozidi miaka 18 atalazimika kuitumikia jamii kwa kipindi kitakachoamuliwa na Mahakama. 28 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Wakati akiitumikia jamii kwa kipindi hicho atasimamishwa masomo na atarejea masomo yake baada ya kukamilisha kipindi hicho. Sheria hii pia inamlinda mtoto wa kike mwenye umri usiozidi miaka 18 ambaye amepata mimba kutokana na kukosa elimu. Sheria inaeleza kwamba mwanafunzi wa kike mwenye umri chini ya miaka 18 atakapogundulika kuwa ni mjamzito atasimamishwa masomo mara moja, lakini atarejea kwenye masomo mwaka unaofuata baada ya kujifungua. Kwa upande wa mwari aliyepatikana na ujauzito na yeye pia atasimamishwa masomo mara moja, lakini atarejea kwenye masomo baada ya kutumikia jamii kama alivyoamriwa. Lakini mamlaka ya elimu inaweza kumzuia mwari asijiunge na masomo ikiwa hajajirekebisha tabia yake. 1.3.3.1 Matunzo ya Watoto Mwari yeyote, mtoto wa kike, mwanamke aliyeachwa au mwanamke ambaye hajaolewa lakini amepata mimba au amejifungua mtoto nje ya ndoa, anaweza kufungua kesi ya madai katika Mahakama ya Wilaya kudai matunzo ya mtoto kutoka kwa mtu anayedhaniwa kuwa ni baba wa mtoto au aliyemsababishia ujauzito kabla ya mtoto hajazaliwa au wakati wowote kabla ya mtoto hajatimiza miaka 18 au kuweza kujitegemea mwenyewe. Kwa madhumuni ya kumpata baba wa mtoto, mtu yeyote atakayekubali kuwa ni baba wa mtoto au mhusika wa mimba hiyo aidha kwa kauli yake au vitendo vyake basi hatoruhusiwa kulikana jambo hilo na anaweza kushtakiwa kwa ajili ya kutoa matunzo, isipokuwa kama atathibitishia Mahakama kwamba yeye si baba wa mtoto. Lakini hapa ifahamike wazi kwamba ingawa mtu huyo atapaswa kutoa matunzo lakini mambo ya mirathi hayaguswi na Sheria hii na yatashughulikiwa kwa mujibu wa Sheria za mirathi. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 29 Sheria pia imeweka kuwa ni lazima kwa mwari aliyepata mimba amtaje mtu aliyempa mimba. Akikataa atalazimika kuitumikia jamii kwa miezi 3. Lakini ikiwa atatoa jina la uongo kwa makusudi atatumikia jamii kwa miezi 6. Mahakama imepewa uwezo wa kumpa mtu aliyehusika na uja uzito au baba wa mtoto amri ya kutoa matunzo kwa mtoto huyo hadi atimize umri wa miaka 18. Hata hivyo, haki ya kutoa matunzo itasimama pale mama atakapoolewa na mtu huyo. 1.3.4 Sheria Juu ya Kazi za Polisi Kazi za msingi za polisi katika usimamizi wa utekelezaji wa Sheria zimeelezewa kwenye Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai. Pia zipo Sheria ndogo ndogo, zinazoweka utaratibu wa utendaji wa kazi za polisi. Sheria hizi ndogo ndogo zinaitwa Police General Orders (PGO). Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai(Namba 7) ya 2004 na hizo Amri za Utendaji wa shughuli za Kipolisi ndio zinaainisha utaratibu mzima wa kufuatwa na watendaji wa Jeshi la Polisi hasa katika kupambana na makosa ya jinai. Sehemu hii inazungumzia mambo ya msingi yaliyomo katika maamrisho ya Sheria hizi. 1.3.4.1 Polisi na Upelelezi Katika Makosa ya Jinai Baada ya kazi za uendeshaji wa kesi za jinai kwa upande wa Zanzibar kuwekwa ndani ya shughuli zinazofanywa na Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka( Director of Public Prosecutions- DPP), Jeshi la Polisi limebaki na kazi kubwa moja ya kufanya uchunguzi au upelelezi juu ya makosa ya jinai. Hata hivyo, ingawa uendeshaji wa kesi za jinai mahakamani ni kazi ya Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka(DPP), Jeshi la Polisi bado linasaidia kufungua na kuendesha kesi mahakamani kwa baadhi ya kesi za jinai katika mahakama za ngazi za chini. Sababu za msingi ni kuwa Afisi ya Mkurugenzi wa Mashtaka bado ni mpya na hadi sasa haina 30 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: watumishi wa kutosha kuendesha kesi za jinai katika mahakama zote za Zanzibar.Shughuli za msingi ambazo Jeshi la Polisi wanapaswa kuzifanya na namna wanavyopaswa kuzifanya inaelezewa hapa chini. 1.3.4.2 Upelelezi wa Makosa ya Jinai Chini ya kifngu 74(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai, Polisi ni moja wapo ya vyombo vyenye mamlaka ya kuzuia makosa na kufanya upelelezi wa makosa ya jinai. Upelelezi unaweza kufanywa pia na chombo kingine chochote chenye mamlaka ya kuchunguza aina maalum za kesi. Vile vile, Mkurugenzi wa Mshtaka anaweza kumteua Afisa yeyote kufanya upelelezi wa kesi katika makosa ya jinai. Katika kufanya upelelezi Afisa wa Polisi anaweza kumkamata mtu anayehusika, kumhoji, kumpekua, kumuweka kizuizini na kumshitaki mahakamani kwa mujibu wa sheria hii inavyoeleza. 1.3.4.3. Polisi na Uwezo wa Kumkamata Mtu Kumkamata mtu ni moja kati ya mambo yenye athari za moja kwa moja ya kuingilia uhuru wa mtu kwenda anakotaka ambao unalindwa na Katiba ya Zanzibar na pia Katiba ya Jamhuri ya Muungano. Kwa mujibu wa Katiba hizi, mtu anaweza kuingiliwa katika uhuru wake huo kwa mujibu wa Sheria. Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai ni moja ya Sheria ambazo zinaweka masharti yanayoweka mipaka ya uwezo wa Polisi kumkamata mtu katika shughuli zao za upelelezi. Chini ya Kifungu cha 21(2) cha Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai kinatamka kuwa isipokuwa katika hali zilizoelezwa chini ya Kifungu 21(1), mtu yeyote hatakamatwa isipokuwa kama kukamatwa kwake kumeidhinishwa kwa hati ya kukamatia Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 31 iliyototlewa na Mahakama yenye uwezo na mamlaka hayo. Hali zilizoelezwa kwenye kifungu 21(1), zinazoruhusu mtu kukamatwa na Polisi bila ya kuwepo hati ya mahakama, ni:(i). Mtu ambae amehusishwa na kosa ambalo limeainishwa kwenye Jewali la kwanza ya Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai, au mtu ambaye malalamiko ya msingi yametolewa dhidi yake, au taarifa ya kuminika imetolewa dhidi yake au tuhuma ya msingi imetolewa dhidi yake; (ii). Mtu ambaye anafanya uvunjaji wa amani mbele ya polisi; (iii). Mtu yeyote ambaye ameingilia utendaji wa kazi za Polisi, au ametoroka au amejaribu kutoroka katika ulinzi halali; (iv). Mtu ambaye atapatikana na kitu chochote ambacho kinatuhumiwa kimsingi kuwa kinahusika na uvunjaji wa sheria; (v). Mtu ambaye anatuhumiwa, kutoroka katika utumishi wa Jeshi au Idara Maalum; (vi). Mtu ambaye amekutwa mahali usiku katika hali ambayo kimsingi inatia mashaka kuwa ametenda kosa au anajaribu kutenda kosa; (vii). Mtu ambaye amefanya kosa nje ya Zanzibar(na kukimbilia Zanzibar), jambo ambalo pia ni kosa kwa mujibu wa sheria ya Zanzibar inayohusika na kurudisha wahalifu mahali walipotenda kosa, Zanzibar inawajibu wa kumkamata mtu huyo na kumhifadhi; (viii). Mtu ambaye, bila ya sababu ya msingi, atapatikana na zana za kuvunjia nyumba; (ix). Mtu yeyote ambaye alitiwa hatiani na kuachiwa chini ya masharti ya Kifungu 343 na akavunja masharti ya Kifungu hicho au masharti ya Sheria ndogo ndogo zilizotungwa chini ya Kifungu hicho; au 32 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: (x). Mtu ye yote ambaye ataamini kuwa hati ya kukamatiwa imetolewa dhidi yake. Endapo mtu amekamatwa(kwa mujibu wa vifungu tulivyotaja hapo juu) bila ya hati ya kukamatia askari anayemkamata anatakiwa kumueleza mtu huyo kuwa anayo haki ya kupata dhamana, ikiwa kosa alilokamatiwa halina kizuizi cha utoaji dhamana. Pia askari huyo atamsaidia mtu anayemkamata kupata wadhamini wanaohitajika. 1.3.4.4 Namna ya Kumkamata Mshukiwa na Haki zake Wakati wa kumkamata mtu anayeshukiwa/ anayedhaniwa kutenda kosa, askari Polisi au mtu mwingine anayekamata atamgusa mshukiwa anayemkamata sehemu yoyote ya mwili wake au atamuwekea mtu huyo kizuizi cha kwenda atakako. Hata hivyo, njia hizi hazitatumika kwa mtu ambaye amejisalimisha mwenyewe kwenye ulinzi wa Polisi. Ila, endapo mtu anaekamatwa anapinga kukamatwa kwake, Polisi anayehusika anaweza kutumia nguvu zozote zinazohitajika kumkamata mtu huyo, na siyo zaidi(Vifungu 13(1) na(2), na 16). Askari ambaye anatekeleza amri ya kumkamata mtu anatakiwa ajitambulishe kwanza kwa mtu anayetaka kumkamata; na amweleze kosa alilofanya hadi kufikia kukamatwa. Askari huyo pia anatakiwa amweleze mtu anayemkamata haki yake ya kubakia kimya anapoulizwa na kwamba kama ataamua kutoa maelezo basi maelezo yake yanaweza kutumika kama ushahidi katika kesi yake. Atamueleza pia kuhusu haki yake ya kuwepo Wakili wake au rafiki mwengine yeyote wakati anapohojiwa; na pia kumueleza kuhusu haki zake za kupewa dhamana, hasa endapo ukamataji umefanywa bila ya hati ya kukamatia(Kifungu 30(1) hadi(4). Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 33 Mtu ambae amekamatwa hatashikiliwa kwa muda wa zaidi ya masaa 24 kabla hajapelekwa mahakamani au kuachiliwa(Kifungu 28), isipokuwa iwe ni siku ya mapumziko ambapo Mahakama haifanyi kazi. 1.3.4.5 Muda wa Mtu Kuhojiwa Kuna wakati maalum unafaa kwa mtu aliekamatwa na Polisi kuhojiwa. Muda huo umeelekezwa chini ya kifungu 33(1) cha Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai. Kwa mujibu wa maamrisho ya kifungu hicho mtu ambaye amewekwa kizuizini kuhojiwa ndani ya muda wa masaa manne kuanzia wakati ambapo mtu huyo ametiwa kwenye kizuizi. Katika kutathmini muda huo, muda ambao mtuhumiwa amepewa kuzungumza na Wakili wake au mtu mwingine yeyote, hautahesabiwa. Hata hivyo muda wa msingi wa masaa manne unaweza kurefushwa katika hali mbili zifuatazo:(i) Endapo kutokana na mazingira ya kesi yenyewe, mpelelezi anaomba kuwa mahojiano ya msingi hayawezi kumalizika kwa muda wa hayo masaa manne, muda huo unaweza kuongezwa lakini usizidi masaa manane. (ii) Endapo kabla ya kumalizika masaa manne ya msingi, au kabla ya kumalizika muda wa nyongeza, mpelelezi ameomba na kupewa amri ya mahakama chini ya kifungu 33 cha Sheria ya Mwenendo wa Kesi za Jinai ili aweze kukamilisha upelelezi kwa muda wowote unaohitaji. Kwa mujibu wa taratibu hizi askari hatakiwi kumhadaa, kumdhalilisha au kutumia nguvu dhidi ya mtuhumiwa wakati wa kumhoji. Mtu yeyote ambaye yuko kizuizini na amehojiwa kinyume na utaratibu anaweza kudai fidia mahakamani 34 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 1.3.4.6. Namna ya Upekuzi Chini ya Sheria ya Mwenendo wa kesi za Jinai, upekuzi upo wa aina mbili(1) Upekuzi kwa ajili ya kumkamata mtuhumiwa wa uhalifu, na(ii) Upekuzi kwa ajili ya kupata kitu kwa ajili ya ushahidi katika kesi ya jinai. Upekuzi kwa ajili ya kumkamata mtuhumiwa wa uhalifu unafanywa kwa mujibu wa vifungu vya 14,15 na 17. Kwa mujibu wa maamrisho ya vifungu hivi, endapo inaaminika kuwa mtu anayetuhumiwa kwa kosa la jinai, itakuwa ni halali kwa askari mwenye uwezo wa kukamata au amri ya kumkamata mtu huyo. Na katika kufanya hivyo, anaweza kumtaka mtu yeyote mwenye nyumba ambayo mtuhumiwa yumo amruhusu kuingia na kumkamata mtuhumiwa. Endapo atakataliwa ruhusa ya kuingia ndani anaweza kuvunja sehemu yeyote ya jengo na kuingia ndani ili kuweza kumkamata mtuhumiwa. Upekuzi kwa ajili ya kupata kitu ambacho kinahitajika kwa ushahidi katika kesi unafanywa kwa mujibu wa vifungu vya 145, 147, 148 na 149. Chini ya Kifungu cha 145, hati ya upekuzi kwa ajili ya kupata kitu ambacho kinaweza kuwa ni ushahidi katika kesi ya jinai inaweza kutolewa na mahakama baada ya mahakama kuthibitisha kwa kiapo kuwa kuna matumaini ya kupata ushahidi huo katika jengo fulani, au chombo au kitu au mahali popote. Hati ya upekuzi chini ya kifungu hiki inatolewa kwa polisi. Hati hii inampa polisi aliyepewa uwezo wa kuingia(kwa ruhusa ya mwenye nyumba au kwa kuvunja) ndani ya nyumba, chombo au mahali palipotajwa na kufanya upekuzi. Wakati wa upekuzi, askari aliyepewa amri ya kupekuwa anatakiwa awaite watu wawili au zaidi ili kushuhudia upekuzi huo. Upekuzi utafanywa mbele ya watu hao ambao watashuhudia zoezi lote hilo. Baada ya upekuzi, askari anayefanya upekuzi atatayarisha orodha ya vitu vyote vinavyohitajika ambavyo vimepatikana katika upekuzi Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 35 huo, Orodha hiyo itasainiwa na askari aliyepekua na pia hao watu walioshuhudia. Watu ambao wanapekuliwa nao wana haki ya kumpekua askari anayefanya upekuzi kabla ya upekuzi huo kuanza. Pia, wakati wote wa upekuzi na ukamataji askari wanatakiwa wachunge heshima ya mtu wanayemkamata. 1.3.5 Kanuni za Kutumikia Jamii Kanuni hizi zimetungwa chini ya Sheria ya Mwenendo wa Makosa ya Jinai Namba 7 ya 2004 na zimeanza kutumika tarehe 1 Februari 2006 zikiwa na lengo la kuweka utaratibu wa namna gani wale watu wanaohukumiwa kwa makosa madogo madogo wataweza kuitumikia jamii badala ya kwenda chuo cha mafunzo. Makosa madogo ni yale makosa ambayo adhabu yake haizidi kifungo cha miaka 2. Kabla ya Mahakama kutoa amri ya kutumikia jamii kwanza inatizama mazingira na tabia ya mshtakiwa, pia inaweza kumtaka mshtakiwa alete wadhamini ambao watahakikisha kwamba ataitumikia jamii. Kazi atakayofanya mshtakiwa haitozidi miezi 12 na muda wa kazi hautozidi saa 8 kwa siku. Mshtakiwa atakuwa chini ya usimamizi wa afisa atakayetajwa katika amri hiyo. Mahakama itataja aina ya kazi ambayo mshtakiwa ataifanya, na ikiwa mshtakiwa atashindwa kufanya kazi aliyopangiwa Mahakama inaweza kuibadilisha amri hiyo, kumtoza faini isiyozidi shilingi laki tatu, kuifuta amri hiyo na kutoa hukumu ambayo ingepaswa kutolewa kwa kosa hilo. Ikiwa anayetumikia jamii ni mtoto masharti ya kumlinda mtoto dhidi ya kazi za hatari na zenye kuathiri afya lazima yafuatwe. 36 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Ikiwa mshtakiwa anayetumikia jamii atahukumiwa kwenda chuo cha mafunzo kwa kosa jingine, Mahakama itasimamisha amri ya kutumikia jamii na itaweka muda wa kwenda chuo cha mafunzo ambao angetakiwa atumikie hapo awali. Lakini Mahakama itazingatia muda ambao ameshaitumikia jamii. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 37 SURA YA PILI Sehemu ya Kwanza 2.1.0 Katiba na Mgawanyo wa Madaraka Kifungu cha 4 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977(Kama ilivyorekebishwa kwa Sheria Namba 15 ya 1984), na kifungu 5A ya Katiba ya Zanzibar 1984(kama ilivyorekebishwa kwa sheria Namba 2 ya 2002) zinaweka masharti yanayofanana yanayoainisha dhana ya Mgawanyo wa Madaraka. Kila moja kati ya vifungu hivyo vinazungumzia mgawavyo wa Madaraka kati ya mamlaka tatu. Mamlaka hizi ni:(i). Mamlaka ya kiutendaji; (ii). Mamlaka ya kutunga Sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma; na (iii). Mamlaka ya kutekeleza utoaji haki. Kwa upande wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mamlaka ya kiutendaji ni Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mamlaka ya kutunga Sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma ni Bunge la Tanzania, na mamlaka ya kutekeleza utoaji haki ni Mahakama ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Kwa upande wa Zanzibar mamlaka ya kiutendaji ni Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Mamlaka ya kutunga Sheria na kusimamia utekelezaji wa shughuli za umma ni Baraza la Wawakilishi, na Mamlaka ya kutekeleza utoaji haki ni Mahakama ya Zanzibar. Mgawanyo wa madaraka(au mamlaka) una madhumuni ya kugawa, kutofautisha na kutenganisha aina kubwa tatu za mamlaka katika kuendesha nchi. Lengo ni kuona kuwa kuna mgawanyo wa mamlaka baina ya vyombo au mihimili mikubwa mitatu ya kendesha nchi. 38 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mambo matatu ndio yanakusudiwa katika dhana hii ya mgawanyo wa Madaraka. Mambo yenyewe ni:(i). Kwamba kila muhimili mmoja wa dola udhibiti na ufanye kazi ya aina moja tu katika mamlaka hizi tatu. Yaani, Mahakama isifanye kazi za utendaji wala kazi ya kutunga sheria; Serikali nayo isijishughulishe na huduma za utoaji haki wala kutunga sheria; na Bunge au Baraza la Wawakilishi lisijishughulishe na kazi ya kutoa haki wala kazi za utendaji. (ii). Kwamba mtu ambae anafanya kazi katika muhimili mmoja au mamlaka moja asiwe na nafasi ya kufanya kazi katika mamlaka nyingine kwa wakati mmoja. Yaani, Mbunge au Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi asiwe pia anahukumu kesi za watu mahakamani wala kuwa mtendaji Serikalini; Jaji au Hakimu asifanye kazi ya utendaji Serikalini wala ya utungaji wa Sheria; na mtendaji Serikalini asijishughulishe na utungaji wa Sheria wala kutoa hukumu katika kesi za watu. (iii). Kwamba, katika kufanya shughuli zake, kila mamlaka isiingilie shughuli zinazopaswa kufanya mamlaka nyingine. Haya ndio maelezo kwa ufupi kuhusu dhana ya mgawanyo wa madaraka. Hata hivyo, ni muhimu sana kuelewa kuwa kutokana na umuhimu wa lazima wa maingiliano ya kiutendaji miongoni mwa mamlaka hizi tatu za utumishi wa dola, haiwezekani tuwe na mgawanyo wa madaraka ulio thabiti kama ulivyobuniwa na waanzilishi wa dhana yenyewe na kuelezewa hapa juu. Kutokana na hali hiyo ndio inaonekana, kwa mfano, kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano ni sehemu moja ya Bunge la Tanzania, sehemu nyingine ni Wabunge wenyewe(ibara ya 62(1) ya Katiba ya Jamhuri pia angalia kifungu ya 3(1) ya Katiba ya Zanzibar kwa masharti kama hayo kwa upande wa Zanzibar). Vile vile Mawaziri na Manaibu Mawaziri wanateuliwa na Rais kutokana na Wabunge Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 39 au Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi(Ibara 55(4) ya Katiba ya Jamhuri kwa upande wa Tanzania; na kifungu 39(2) na 42(2) za Katiba ya Zanzibar, kwa upande wa Zanzibar). Katika mfano mwingine, Katiba ya Zanzibar imeipa Mahakama uwezo wa kuingilia utendaji wa mamlaka nyingine, yaani Baraza la Wawakilishi na Serikali, pale ambapo kuna ukiukwaji wa Katiba Kifungu ya 25A(1) ya Katiba ya Zanzibar ya 1984, inatoa fursa kwa mtu yeyote kufungua shauri Mahakama Kuu ya Zanzibar pale ambapo inathibitika kuwa Katiba imevunjwa, au inavunjwa, au inaelekea kuvunjwa. Na ikiwa Mahakama itaridhika na hoja ya mwombaji Mahakama Kuu inaweza kutoa amri itakayoona inafaa. Kwa kutambua hali hii ndio kifungu 5A(3) ya Katiba ya Zanzibar ime 2.2.0 Utawala wa Sheria 2.2.1 Maana ya Utawala wa Sheria Utawala wa Sheria, kama dhana, ina maana tatu kubwa:(i). Kila kitu kifanywe kwa mujibu wa sheria. Maana hii ikitafsiriwa kuhusiana na mwenendo wa Serikali inamaanisha kuwa Serikali na vyombo vyote vya umma viendeshwe kwa mujibu wa Sheria; (ii). Hakuna mtu yoyote ambae ataathirika au ataathiriwa nafsi yake au mali yake isipokuwa ni kwa mujibu wa sheria zinazosimamia au zinazozingatia haki; na (iii). Tatizo au mzozo wowote iwe ni dhidi ya mtu binafsi, Serikali au Chombo chochote cha umma unapaswa uamuliwe na Mahakama ambayo iko huru ambayo haiingiliwi katika kazi zake. 40 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Katika Katiba ya Zanzibar 1984, utawala wa sheria umewekewa misingi yake kwenye kifungu cha 5 na 12. Kifungu cha 5 kinaeleza kuwa Zanzibar itafuata mfumo wa kidemokrasia ya vyama vingi vya siasa, wenye kuheshimu utawala wa sheria. Kifungu cha 12 kinaelezea kwa kirefu juu ya usawa mbele a Sheria, na maamrisho yake yanafanana na yale ya Kifungu 13 katika Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977(kama ilivyorekebishwa mnamo 1985). 2.2.2 Usawa Mbele ya Sheria Moja katika nguzo muhimu za utawala wa sheria ni kuwepo kwa usawa mbele ya sheria. Katiba ya Jamhuri ya Muungano 1977(Ibara ya 13) na Katiba ya Zanzibar 1984(Kifungu 12) zimeweka ufafanunuzi wa kutosha juu ya tafsiri ya usawa mbele ya sheria. Vifungu vyote hivi viwili zinaelezea mambo yanayofanana, kuwa bila ya ubaguzi wowote, kulindwa na kupata haki kila mtu katika nchi hii ana haki sawa na mwingine yeyote mbele ya Sheria. Yaani bila ya kujali mtu asili yake, dini yake, rangi yake, jinsia yake n.k., kila mtu anapaswa kutendewa kadiri ambayo sheria inaelekeza mtu huyo atendewe katika mazingira yanayohusika. Mazingira hayo iwe yanahusu haki au dhima ambayo mtu anayo kwa mujibu wa sheria. Usawa mbele ya sheria pia unahitaji kuwepo na sheria zinazofaa kusimamia na kulinda haki za watu. Yaani sheria zenyewe zinazosimamia utawala wa sheria zisiwe zinaweza kutumika kwa kuhujumu haki na uhuru wa watu wenyewe. Kwa maana hiyo sheria zinazoruhusu utawala wa mabavu hazina nafasi katika dhana ya utawala wa sheria. Maamrisho ya haki na wajibu wa watu kwenye Katiba ya Jamhuri ya Muungano(Ibara ya 12 hadi 30) na Katiba ya Zanzibar(Kifungu 11 hadi 24) ni hatua muhimu sana katika kutekeleza utawala wa sheria. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 41 2.2.3 Umuhimu wa Utawala wa Sheria Moja ya nguzo muhimu za demokrasia katika nchi yoyote ni utawala wa sheria. Faida kubwa ya utawala wa sheria ni kuwafanya watu waweze kujua mipaka ya mahusiano kati yao na vyombo vya dola vinavyoongoza nchi yao pia kuweza kujua kuhusu mahusiano miongoni mwao wenyewe kwa wenyewe. Hali hii inapotokea inakuwa ni rahisi mtu kuweza kujua hatma ya mambo anayopanga kufanya, na hivyo kuweza kujiepusha na matatizo yasiyo ya lazima. Hapo tu ndio utulivu wa watu na mali zao unaweza kupatikana kitu ambacho ni nguzo muhimu katika maendeleo ya nchi yoyote. Lakini pale utawala wa sheria unapokosekana, na ikawa haki katika jamii haitendeki hata katika hali ambayo h kuonekana, kukosekana kwa haki inakuwa ni udhia mkubwa kwa watu ambao wanaamini kuwa haki zao zinavunjiwa. Udhia ukikithiri watu huwa wanajitafutia namna au mbinu zao wenyewe za kuondoa huo udhia. Mara nyingi mbinu hizi huwa hazikubaliki kwa sababu ni kinyume ya zile ambazo zimebuniwa kistaarabu na jamii(ambazo hazifuatwi). Mbinu za watu kudai haki walizonyimwa mara nyingi ni mbinu za kimapambano zenye lengo la watu kujichukulia hatua mikononi mwao. Migorogoro ya wenyewe kwa wenyewe(na hata ya baadhi ya mataifa kwa mataifa yakiwemo yale ya kujitoa muhanga dhidi ya raia wa nchi fulani) ambayo yameenea hivi sasa duniani inawezekana iwe inatokana na upotoshwaji wa haki. Katika ngazi za PDQXQJ¶XQ iko ambayo hupuuzwa na watawala. Baadae hukua na kuenea katika sehemu kubwa ya nchi. Matokeo yake wakati mwengine husababisha vita vya wenyewe kwa wenyewe. 42 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 2.3.0 Muundo na Kazi za Mihimili Mikuu Katika sehemu hii tunazungumzia muundo na kazi za Mihimili Mikuu ya nchi kwa upande wa Zanzibar. 2.3.1 Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Serikali ndio inafanya lile Tawi la Kiutendaji( Executive Branch) katika utawala wa nchi. Kazi kubwa ya muhimili huu ni kutayarisha sera za kiutawala na kiutendaji juu ya mambo mbali mbali muhimu na kuzitekeleza katika kuendesha nchi. Ndani ya Serikali zipo ngazi mbali mbali zinazojishughulisha na uundaji na utekelezaji wa sera. Katika ngazi hizi kuna Rais mwenyewe, Wizara, Idara na sehemu( Sections) tofauti. Hivi sasa Serikali ya Zanzibar imegawika katika Wizara 13. Wizara hizo ni Afisi ya Waziri Kiongozi, Wizara ya Nchi(AR) na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Wizara ya Nchi(AR) Tawala za Mikoa na Vikosi vya SMZ, Wizara ya Nchi(AR) Katiba na Utawala Bora, Wizara ya Maji ,Ujenzi, Nishati na Ardhi, Wizara ya Kazi, Maendeleo ya Vijana Wanawake na Watoto, Wizara ya Habari, Utamaduni na Michezo, Wizara ya Utalii, Biashara na Uwekezaji, Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Wizara ya Afya na Ustawi wa Jamii, Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi, Wizara ya Kilimo, Mifugo na Mazingira, na Wizara ya Fedha na Uchumi. Kitu muhimu cha kukielewa kuhusiana na Wizara za Serikali ni kuwa majina na dhamana zao huwa mara kwa mara zinabadilika kufuatana na mipango ya nchi. Ni Rais wa Zanzibar chini ya kifungu 42 cha Katiba ya Zanzibar 1984, mwenye madaraka ya kupanga Wizara za Serikali. Anaweza kubadilisha na kupanga upya Wizara na pia Baraza la Mawaziri wakati wowote. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 43 Kila Wizara huwa inapangiwa Idara zake na Rais, mara nyingi akishauriana na Waziri anaehusika. Mawaziri nao wana mamlaka ya kuanzisha vitengo tafauti chini ya Idara za Wizara zao ili kurahisisha utendaji wa shughuli walizopewa au kurahisisha utendaji wa shughuli walizopewa au kwa lengo la kutafuta ufanisi zaidi wa shughuli zao. Vitengo vya shughuli za Serikali viko vya aina tafauti. Ukiacha vitengo vya kawaida vinavyoendeshwa moja kwa moja na Idara za Serikali, kuna vitengo vyengine vinajitegemea kuitendaji ingawa utawala wake wa jumla uko chini ya Wizara au Idara fulani. Mfano wa vitengo hivyo ni Jeshi la Ulinzi ambalo liko chini ya Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Polisi ambalo nalo liko chini ya Wizara ya Mambo ya Ndani, ambao ni Wizara ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano. Kwenye Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, vitengo kama hivi ni Jeshi la Kujenga Uchumi(JKU), Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo(KMKM), Chuo cha Mafunzo, na Kikosi cha Valantia ambavyo vyote Utumishi wao unasimamiwa na Wizara ya Nchi (AR) Tawala za Mikoa na Vikosi vya SMZ. Mbali na vitengo vya aina hii pia kuna mashirikia ya umma. Haya ni mashirika yanayomilikiwa na Serikali. Yameundwa kwa shughuli maalum, na yanajitegemea kiuendeshaji. Hata hivyo mamlaka ya ujumla juu ya mashirika haya yameegemezwa kwenye Wizara fulani ya Serikali. Mfano ni Shirika la Bandari ambalo linaendeshwa chini ya Utawala wa ujumla wa Wizara ya Mawasiliano na Uchukuzi, na Shirika la Umeme ambalo liko chini ya Wizara ya Maji, Ujenzi, Nishati na Ardhi. 2.3.2 Mahakama Mahakama ni moja kati ya mihimili mikuu mitatu ya kuendesha nchi. Kazi za mahakama ni utekelezaji wa utoaji haki kwa mujibu 44 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: wa Sheria za nchi katika mashauri au kesi zinazopelekwa mbele yake na watu. Katika muundo wa Mahakama, kwa ajili ya Zanzibar, juu kabisa kuna mahakama ya rufaani ya Tanzania. Mahakama hii imeundwa chini ya ibara 117 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania 1977, na inatekeleza majukumu yake hadi Zanzibar. Kazi ya Mahakama ya Rufaa ya Tanzania ni kusikiliza na kutoa uamuzi juu ya kila rufaa inayoletwa mbele ya mahakama hiyo kutokana na hukumu au uamuzi wa namna nyingine yoyote wa Mahakama Kuu ya Jamhuri ya Muungano au wa Mahakama Kuu ya Zanzibar. Kama jina lake linavyoashiria, Mahakama ya Rufaa ya Tanzania haina mamlaka ya kusikiliza kesi kwa mara ya kwanza(original jurisdiction). Uwezo wake ni kusikiliza rufaa tu kutoka hukumu au aumuzi mwengine wa Mahakama Kuu zote(Mahakama Kuu, ya Jamhuri ya Muungano na ile ya Zanzibar). Na uamuzi wa Mahakama ya Rufaani katika jambo au suala lolote ni wa mwisho katika utaratibu wa kimahakama. Majaji wa Mahakama ya Rufaa wanateuliwa na Rais baada ya kushauriana na Jaji Mkuu wa Tanzania. Chini ya Mahakama ya Rufani ya Tanzania kuna mamlaka mbili za kimahakama. Mahakama Kuu ya Tanzania na Mahakama zilizo chini yake, na Mahakama Kuu ya Zanzibar na Mahakama zilizochini yake.Mahakama Kuu ya Tanzania imeanzishwa chini ya ibara 108 ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano na Mahakama za chini yake (ambazo ni Mahakama za Hakimu Mkaazi, Mahakama za Hakimu wa Wilaya, na Mahakama za Mwanzo) zimeanzishwa ndani ya Sheria ya Mahakama za Mahakimu ya mwaka 1984 Mahakama hizo zinatekeleza madaraka yao huko Tanzania Bara tu. Mahakama Kuu ya Zanzibar imeanzishwa chini ya kifungu 93 ya Katiba ya Zanzibar 1984. Mkuu wa Mahakama Kuu ya Zanzibar ni Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 45 Jaji Mkuu wa Zanzibar. Jaji Mkuu wa Zanzibar pamoja na Majaji wengine wa Mahakama Kuu ya Zanzibar wanateuliwa na Rais wa Zanzibar baada ya kushauriana na Tume ya Utumishi ya Mahakama ya Zanzibar. Pia Mahakama ya Kazi ambayo ni sehemu ya Mahakama Kuu. Chini ya Mahakama Kuu ya Zanzibar kuna mishazari miwili ya kimahakama ambayo ni mahakama za Mahakimu na Mahakama za Kadhi. Mahakama za Mahakimu(Zanzibar) imeanzishwa na zinafanya kazi zake kwa mujibu wa sheria ya Mahakama za Mahakimu 1985 na Sheria ya Mahakama za Kadhi 1985 ndio imeunda Mahakama za Kadhi na kuainisha kazi zake. Katika kundi la Mahakama za Mahakimu kuna Mahakama za Mkoa, Mahakama za Wilaya, na Mahakama za Mwanzo. Katika Mahakama za Kadhi kuna Mahakama ya kadhi wa Rufaa, na Mahakama za Kadhi wa Wilaya. Mahakama za Kadhi zinafanya kazi zake kwa misingi ya sheria za Kiislam. Vile vile zipo Mahakama ambazo zipo nje ya mishazari hii miwili, kwa mfano Mahakama ya Ardhi, Mahakama ya Vileo, Bodi ya Kudhibiti Kodi za Nyumba,na Mahakama ya Rufaa za kodi. Ingawa kimuundo Mahakama hizi zipo nje ya ule muundo tulioutaja lakini rufaa zinazotokana na Mahakama hizi huenda Mahakama Kuu na hivyo kuingia katika mfumo wa kawaida. Pia katika muundo huo kuna Mahakama ya Kazi ambapo hii ina uwezo sawa na Mahakama Kuu licha ya kuwepo mbali na mfumo wa kawaida wa mahakama. Rufaa ya mahakama hii huenda moja kwa moja katika Mahakama ya Rufaa ya Tanzania. Maelezo ya mpangilio huo wa Mahakama yanaweza kufupishwa kwa mchoro kama ifuatavyo hapa chini. 46 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mahakama ya Rufaa Tanzania Mahakama Kuu ya Tanzania Mahakama Kuu ya Zanzibar Mahakama ya Kazi Mahakama ya Hamkimu Mkaazi Mahakama ya Wilaya Mahakama ya Mwanzo Mahakama ya Kadhi wa Mkuu Wilaya Mahakama ya Mkoa Mahakama ya Kadhi wa Wilaya Mahakama ya Wilaya Mahakama ya Mwanzo Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 47 2.3.2.1 Uhuru wa Mahakama Tumeona hapo juu kuwa athari moja ya utawala wa sheria ni kuwepo na uhuru wa Mahakama. Maana ya uhuru wa mahakama ni kuwa na mahakama ambazo zinafanya kazi zake kwa mujibu wa sheria bila ya hofu, ushawishi au shindikizo la aina yoyote ile. Kwa ujumla dhana ya uhuru wa mahakama inajengwa kwa misingi ifuatayo:(i). Kwamba inapotokea haki ya mtu binafsi imeingiliwa, inaingiliwa au inaelekea kuingiliwa hata kama Serikali, basi mahakama iwe huru kuamua kesi hiyo bila upendeleo. Uhuru wa mahakama unahitaji maamuzi ya mahakama yasiwe yanaingiliwa au kubatilishwa na wowote kati ya mihimili mikuu ya dola. Aidha, mahakama iwe na uwezo juu ya masuala yote yanayostahiki kuamuliwa na mahakama kwa mujibu wa sheria. (ii). Kwamba, katika kuhakikisha kuwa mahakama ziko huru, Katiba ya nchi inapaswa itowe hifadhi ya kutosha kwa majaji na mahakimu kuhusu kazi zao na pia maslahi yao. Ndio sababu Katiba ya Jamhuri ya Muungano(Ibara112) na Katiba ya Zanzibar(Kifungu 95) zimeweka masharti magumu sana, tofauti na watumishi wengine wote wa umma, ya namna ya kumuondoa madarakani Jaji wa Mahakama Kuu. Pia ni Tume za Uajiri za Mahakama pekee zenye uwezo wa kuwachukulia Mahakimu hatua za nidhamu ikiwa ni pamoja na uwezo wa kuwaodoa mahakimu madarakani(ibara 113 ya Katiba ya Jamhuri, pia kifungu 103 cha Katiba ya Zanzibar). (iii). Dhana ya uhuru wa mahakama inahitaji pia kuwa maslahi ya watumishi wa mahakama yaangaliwe vizuri ili kuhakikisha kuwa mishahara na maslahi mengine yanayolipwa kwa watumishi wa mahakama ni mikubwa kwa wastani na inapatikana bila ya usumbufu. 48 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: (iv). Kwamba ni muhimu sana katika kuhakikisha uhuru wa mahakama kuwa Majaji na Mahakimu wenyewe hawafanyi upendeleo katika maamuzi yao aidha kutokana na utashi wao binafsi au kutokana na kushawishiwa au rushwa. 2.3.2.3 Umuhimu wa Uhuru wa Mahakama Umuhimu wa kuwepo na uhuru wa mahakama ni kuhakikisha kuwa mahakama zinafanya kazi zake za kusimamia utekelezaji wa utoaji haki kwa mujibu wa sheria za nchi na bila ya upendeleo wowote. Hili likiwezekana litafanya jamii iishi kufuatana na maadili ya haki kwa mujibu wa sheria. Lengo ni kuwaondeshea matatizo wananchi ili baada ya kudumu katika matatizo yanayokosa maamuzi sahihi waweze kupeleka matatizo yao mahakamani ambapo wanaamini kuwa matatizo yao yatapata maamuzi sahihi na baada ya maamuzi hayo kutumia zaidi muda wao katika shughuli za maendeleo. 2.3.2.4 Vyombo Vyenye Mamlaka ya Kimahakama Kutokana na haja ya kupata ufanisi zaidi katika usimamizi unaofanywa na idara za Serikali juu ya mambo maalum inayoyashughulikia, Sheria huwa zinatungwa ili kutoa mamlaka ya kimahakama kwa chombo au taasisi iliyomo kwenye idara ya Serikali kwa ajili ya kushughulikia matatizo yanayotokea katika sekta hiyo. Sifa moja kubwa ya chombo au taasisi ya Serikali yenye mamlaka ya kimahakama ni kuwa taasisi hiyo inapewa uwezo wa kimahakama juu ya mambo maalum ambayo Wizara au Idara inayohusika ina mamlaka nayo. Mfano wa vyombo hivyo ni: Mahakama ya Ardhi, Baraza la Kudhibiti Kodi za Nyumba. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 49 2.3.2.4.1 Mahakama ya Ardhi Mahakama ya Ardhi imeanzishwa chini ya kifungu cha 3 cha Sheria ya Mahakama ya Ardhi Namba 7 ya 1994. Mahakama hii imo ndani ya Wizara inayoshughulikia masuala ya Ardhi, na uwezo wake ni kusikiliza kesi zinazohusiana na migogoro ya ardhi. Muundo wa Mahakama ya ardhi unakamilika kwa kuwepo Mwenyekiti na washauri wawili. Mwenyekiti anateuliwa na Rais kwa kipindi cha miaka mitano, na washauri wanateuliwa na Jaji Mkuu kwa kipindi cha miaka mitano vilevile. Mwenyekiti wa Mahakama hii anachukuliwa kuwa ni mtumishi wa Idara ya Mahakama katika ngazi ya Hakimu wa Mkoa. 2.3.2.4.2 Mahakama ya Kumlinda Mlaji Hii ni Mahakama ambayo imeanzishwa chini ya kifungu cha 5(1) cha Sheria ya Kudhibiti Biashara na Kumlinda Mlaji, Sheria Namba 2 ya 1995. Mahakama imeanzishwa kama chombo cha kimahakama kilicho huru ambacho Mwenyekiti wake anateuliwa na Tume ya Uajiri wa Mahakama kutoka miongoni mwa Mahakimu wa Mkoa au watu wenye sifa za kuwa Mahakimu wa Mkoa. Kazi za mahakama hii ni kusikiliza malalamiko kuhusiana na uendeshaji wa biashara na juu ya viwango vya ubora wa bidhaa zinazouzwa ili kuhakikisha uuzaji wa bidhaa unakidhi matakwa ya kisheria. Katika uamuzi wake mahakama hii ina uwezo wa kuamuru kupatiwa taarifa inayoihitajia, kutoa faini, na kutoa amri nyinginezo za mpito au za kudumu kwa ajili ya kuzuia jambo lisifanyike. Mtu ambaye hakuridhika na uamuzi wa Mahakama hii anaweza kukata rufaa mbele ya Mahakama Kuu. 50 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 2.3.2.4.3 Mahakama ya Kudhibiti Kodi ya Nyumba Chombo hichi ambacho kina hadhi ya kimahakama na kiongozi wake ni Hakimu wa Wilaya, ni chombo ambacho kimewekwa maalum kwa ajili ya kushughulikia migogoro yote inayohusiana na mambo ya kodi ya nyumba. Hivyo mwenye nyumba au mpangaji wanapokuwa na mgogoro au mzozo kuhusu kodi ya nyumba au upangishaji hutakiwa kupeleka mgogoro huo katika chombo hiki kwa maamuzi. 2.3.2.4.4 Mahakama ya Kazi Sheria za kazi zimeanzisha Mahakama ya Kazi ambayo itakuwa ni sehemu ya Mahakama Kuu. Mahakama hii itakuwa na jukumu la kusikiliza na kuamua migogoro ya kazi itakayopelekwa, na kusajili makubaliano ya pamoja. Mtu yeyote asiyeridhika na maamuzi ya Mahakama hii anaweza kukata rufaa katika Mahakama ya Rufaa ya Tanzania. 2.3.3 Baraza la Wawakilishi Baraza la Wawakilishi ni moja kati ya mihimili Mikuu ya utawala wa nchi kwa hapa Zanzibar. Baraza hili limeanzishwa chini ya kifungu cha 63 cha Katiba ya Zanzibar 1984. Kwa mujibu wa kifungu hiki, kutakuwa na Baraza la Kutunga Sheria litakalokuwa na sehemu mbili, Rais wa Zanzibar kwa upande mmoja na Baraza la Waakilishi kwa upande wa pili. 2.3.3.1 Kazi ya Baraza la Wawakilishi Kazi za Baraza la Wawakilishi zimeelezewa chini ya kifungu 88 ya Katiba ya Zanzibar,1984. Kazi zenyewe ni:(i). Kutunga sheria pale ambapo utekelezaji wa jambo unahitajika kuwepo kwa sheria hiyo; Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 51 (ii). Kujadili shughuli za kila Wizara wakati wa vikao vyake vya kila mwaka vya Bajeti; (iii). Kuuliza masuala mbali mbali kwa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar katika vikao vyake Barazani; na (iv). Kuidhinisha na kusimamia mipango ya maendeleo ya Serikali katika njia ile ile ambayo Bajeti ya mwaka inaidhinishwa. 2.3.3.2 Wajumbe wa Baraza la Wawakilishi Kwa mujibu wa kifungu 64 ya Katiba ya Zanzibar 1984(Kama ilivyorekebishwa mnamo mwaka 2002), Wajumbe kamili wa Baraza la Wawakilishi ni 81 ambao watapatikana kama ifuatavyo:(i). Wajumbe 50 wa kuchaguliwa kutoka majimbo ya uchaguzi; (ii). Wajumbe 10 wa kuteuliwa na Rais(angalau wawili kutoka Upinzani); (iii). Wajumbe Wanawake 15 ambao huteuliwa na Tume ya uchaguzi kutoka vyama vya siasa kuzingatia uwiyano wa kushinda kwao katika uchaguzi wa Uwakilishi Majimboni; (iv). Wakuu wa Mikoa watano(5) wa Mikoa ya Zanzibar; na (v). Mwanasheria Mkuu wa Zanzibar. 2.3.3.3 Uongozi wa Baraza Uongozi katika Baraza la Wawakilishi la Zanzibar umegawika matawi mawili ambayo ni uongozi katika kuendesha vikao vya Baraza kwa upande mmoja na uongozi wa Baraza kama ofisi, kwa upande mwengine. 52 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Viongozi kwa ajili ya kuendesha vikao vya Baraza ni Spika, Naibu Spika na Mwenyekiti wa Baraza. Utaratibu wa kuwapata viongozi hawa umewekwa kwa mujibu wa masharti ya Katiba ya Zanzibar na masharti ya Kanuni za Baraza( Rules of the House). Kazi kubwa za viongozi hawa ni kusimamia majadiliano na kufanywa kwa maamuzi juu ya mambo yanayoletwa katika Baraza kwa mujibu wa Katiba, Kanuni za Baraza na sheria nyingine. Viongozi wengine wa Baraza ambao ingawa hawahusiki moja kwa moja katika kuendesha vikao vya Baraza, wanamchango mkubwa katika kufanikisha shughuli za Barazani, ni Waziri Kiongozi ambae ni Mkuu wa shughuli za Serikali ndani ya Baraza, Mkuu wa Upinzani ambae anateuliwa kwa mujibu wa Kanuni kutokana na Wawakilishi wa Vyama vya Upinzani, Mnadhimu wa Chama Tawala, na Mnadhimu wa Upinzani. Wakati Kiongozi wa shughuli za Serikali na Kiongozi wa Upinzani wanadhamana ya mwisho ya maamuzi yanayofanywa kuhusiana na mambo yanayowahusu(kama Serikali au Upinzani), wanadhimu wao ni Viongozi wa kinidhamu hasa miongoni mwa Wajumbe anaowasimamia. Katika kada ya utendaji, Katibu wa Baraza na Watendaji wa chini yake wanafanya kazi zao za kiofisi chini ya Uongozi wa Spika wa Baraza. 2.3.3.4 Kamati za Baraza la Wawakilishi Tumeona hapo juu kuwa moja ya kazi za Baraza ni kuidhinisha na kusimamia utekelezaji wa mipango ya maendeleo. Kazi za kutekeleza mipango ya maendeleo ni kazi za Serikali. Kazi hizi zinafanywa kila siku kwa namna tofauti katika Wizara za Serikali.Kutokana na namna ambavyo shughuli hizo zinafanywa sio rahisi kwa Baraza kuweza kufuatilia kwa undani utendaji huo wakati wa vikao vya Baraza. Kikubwa ambacho Baraza linaweza kukifanya wakati wa vikao ni kuwauliza mawaziri maswali kuhusu utendaji wa Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 53 Wizara zao. Bila ya shaka mawaziri wanajibu, lakini ni vigumu kwa Wajumbe waliopo ndani ya Baraza kuweza kujua ukweli uliomo ndani ya jibu lilitolewa na Waziri. Kwa ajili ya kupata ukweli na taarifa zaidi kuhusu utendaji wa Serikali ndio Baraza la Wawakilishi Zanzibar limeunda Kamati za kudumu za Baraza kwa ajili ya kazi hizo. Muundo wa Kamati za Kudumu za Baraza huwa unabadilika kulingana na mazingira ya Serikali na haja iliopo. Hata hivyo, kwa sasa Baraza la Wawakilishi Zanzibar lina Kamati zifuatazo:(i). Kamati ya Uongozi na Shughuli za Baraza; (ii). Kamati ya Fedha na Uchumi; (iii). Kamati ya Mawasiliano, Ujenzi na Mazingira; (iv). Kamati ya Maendeleo na Ustawi wa Jamii; (v). Kamati ya Katiba, Sheria na Utawala; (vi). Kamati ya Kilimo, Maliasili na Utalii; (vii). Kamati ya Kuchunguza na Kudhibiti Hesabu za Serikali na Mashirika(Public Accounts Committee- P.A.C.); na (viii). Kamati ya kufuatilia utekelezaji wa Ahadi za Serikali. Sehemu ya Pili 2.4 Sheria Mbali Mbali 2.4.1 Sheria ya Madai Sheria ya madai kama tulivyoona kabla ni Sheria binafsi. Hizi ni zile Sheria zinazozungumzia mahusiano binafsi kati ya mtu mmoja na mwengine, au kati ya mtu na kikundi cha watu chenye kutambulika kisheria, au kati ya vikundi vya watu vyenye kutambulika kisheria. 54 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Sheria za madai tunaweza kuzielezea katika makundi mawili makubwa: (i). Sheria zinazoweka masharti juu ya haki na wajibu wa watu katika hali tofauti( substantive law); na (ii). Sheria zinazoweka taratibu za kufuatwa katika uendeshaji wa kesi za madai. Mfano wa Sheria za madai zinazozingatia masharti juu ya haki na wajibu binafsi wa watu ni kama Sheria za mirathi, sheria za ndoa, Sheria ya mikataba, nk. Hapa Zanzibar mambo yanayohusu mirathi na ndoa pamoja na talaka yanasimamiwa na Sheria za Kiislam, kwa wale waislam; na mizozo yote inayohusiana na utekelezaji wa Sheria hizo huwa inasuluhiswa au kutolewa maamuzi na Mahakama za Kadhi. Kwa upande wa wale wasiokuwa waislamu masuala yao hushughulikiwa na Mahakama za kawaida. Kwa upande wa mizozo ya ardhi kama tutakavyokuja kuona baadae katika Sheria za Ardhi; hii husikilizwa katika Mahakama ya Ardhi. Mizozo inayotokana na mikataba hii husikilizwa katika Mahakama za kawaida lakini hufunguliwa kesi kama kesi za madai. Mizozo inayotokana na ukodishaji wa nyumba, hii husikilizwa na Bodi ya Kudhibiti Kodi, na kwa upande wa mizozo ya kazi au inayotokana na ajira, hii husikilizwa katika Mahakama ya Kazi. Mizozo yote hii tuliyoitaja hapa inaingia katika kesi za Madai kwani mizozo ya ardhi, kodi ya nyumba, mikataba na hata ajira mara nyingi huwa ni ya baina ya mtu na mtu. Mtu anayeona kuwa amedhulumiwa ndie anayeamua kuchukua hatua kuhusiana na mzozo au mgogoro huo. Kama tulivyokwisha kuona kwamba kabla ya kuamua ni Mahakama gani upeleke kesi yako, kwanza inabidi uangalie ni mzozo wa aina gani. Ikiwa ni moja ya mizozo iliyotajawa hapo juu mizozo hiyo Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 55 utaipeleka kwenye Mahakama hizo. Lakini ikiwa ni mizozo inayofaa kwenda Mahakama za kawaida kwa mfano masuala ya mikataba, hapa pia zipo Mahakama tofauti; yaani Mahakama ya Mwanzo, Mahakama ya Wilaya, Mahakama ya Mkoa na Mahakama Kuu. Ili uweze kujua ni mahakama gani upeleke tatizo lako inabidi uangalie thamani ya kesi au mzozo wenyewe. Mahakama Kuu imeweka utaratibu ufuatao: (i). Mahakama ya Mwanzo ± husikiliza kesi zote za mali inayohamishika isiyozidi sh. 1,000,000. na mali isiyohamishika isiyozidi sh. 5,000,000. (ii). Mahakama ya Wilaya- husikiliza kesi zote za mali inayohamishika ya zaidi ya sh. 1,000,000, lakini isiyozidi sh. 5,000,000 na mali isiyohamishika ya zaidi ya sh. 5,000,000 lakini isiyozidi sh. 10,000,000. (iii). Mahakama ya Mkoa- husikiliza kesi zote za mali inayohamishika ya zaidi ya sh. 5,000,000, lakini isiyozidi sh. 30,000,000 na mali isiyohamishika ya zaidi ya sh. 10,000,000 lakini isiyozidi sh. 50,000,000. (iv). Mahakama Kuu ± husikiliza kesi zilizo juu ya viwango vinavyosikilizwa na Mahakama ya Mkoa. 2.4.1.1 Ufunguzi wa Kesi za Madai Kwa upande wa kesi za madai, kama tulivyoeleza hapo juu kuwa hizi ni kesi zinazomhusisha mtu mmoja na mwingine. Hivyo, uamuzi wa kufungua kesi ya madai pia anao mtu mwenyewe. Kwa mfano: Juma ameingia mkataba na fundi saramala wa fundi huyo kumchongea kitanda. Juma amemlipa fundi huyo 56 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: sh. 100,000 kwa ajili ya kazi hiyo na fundi amemuahidi aje achukue kitanda baada ya mwezi mmoja. Lakini alipokwenda kuchukua kitanda amemkuta fundi hajakichonga kitanda hicho na alipodai arejeshewe pesa zake fundi huyo alikataa kutoa pesa. Hivyo ili Juma azipate pesa zake kwa kutumia njia ya Mahakama ni lazima afungue kesi ya madai dhidi ya fundi seramala. Hivyo, uamuzi wa kufungua kesi ya madai anao mwenyewe Juma. 2.4.1.2 Hatua za Ufunguaji na Uendeshaji wa Kesi za Madai Kwanza, kabisa kabla ya kufungua kesi ya madai ni lazima liwepo jambo lenye mzozo. Katika mfano uliopo hapo juu kwa vile fundi seramala amekataa kurejesha pesa alizochukua tayari mzozo upo hivyo kesi ya madai inaweza kufunguliwa. Lakini kama fundi seramala atatoa ahadi kama atakichonga kitanda baada ya wiki na kumkabidhi mwenyewe, au kumpa ahadi Juma aje achukue pesa zake baada ya wiki. Hapa patakuwa hapana mzozo hivyo kesi ya madai haiwezi kusimama. Lakini ikiwa atavunja ahadi hiyo baada ya muda aliotoa hapo utakuwa mzozo umeanza tena. Ufunguaji wa kesi ya madai huanza kwa Mdai kuwasilisha hati ya madai Mahakamani. Hati ya Madai ni maelezo anayotoa mdai kuhusu mkasa wote ulivyotokea hadi yeye kufika kuipeleka kesi Mahakamani. Mara nyingi hati ya madai huwasilishwa Mahakamani ikiambatana na uthibitisho au vielelezo au ushahidi alionao Mdai. Kwa mfano, katika mfano tuliotoa ikiwa fundi seremala alimpa Juma risiti inayoonyesha kupokea fedha hizo, hivyo katika hati ya madai Juma lazima aambatanishe risiti hiyo. Hati ya Madai baada ya kuwasilishwa mahakamani ikiwa imekamilika kwa kuwemo Wadaawa, yaani Mdai na Mdaiwa, kuwemo anuani zao ambazo zitatumika kwa upelekaji wa wito na Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 57 mambo mengine ya mahakama, kuwemo kwa maelezo ya kesi na maelezo hayo kuthibitishwa na Mdai, na pia Mdai kutia saini yake. Mdai pia hutakiwa kutayarisha nakala kadhaa za hati ya madai kwa ajili ya kumpatia Mdaiwa au ikiwa ni zaidi ya mmoja Wadaiwa, na pia nakala moja ni ya Mahakama. Kwa mfano katika kesi ya Juma, atatakiwa kutayarisha nakala tatu za hati ya Madai. Baada ya kukamilika mambo hayo Mahakama hupokea hati ya madai na nakala zake na humtaka Mdai kulipa ada ya ufunguaji kesi. Vipo viwango maalum vilivyopangwa na Mahakama kwa ajili ya kufungua kesi. Baada ya malipo kufanywa, kesi hiyo hupewa namba kwa mfano Kesi ya Madai Namba 2 ya 2007, na pia nakala moja ya hati ya madai hukabidhiwa Mdai. Hatua inayofuata ni kwa Mahakama kumpatia Mdaiwa nakala moja ya hati ya madai na huyo Mdaiwa hutakiwa kuijibu hati hiyo ya madai kwa maandishi na kuwasilisha Mahakamani majibu ya hati ya madai yakiwa na idadi ile ile ya nakala. Hapo Mdai nae hukabidhiwa majibu hayo na yeye anaweza kuyajibu tena kwa kuwasilisha Mahakamani Majibu ya Madai. Hapo hatua hii huwa imekamilika na suala linalofuata ni kwa mahakama kupanga siku ya kuanza kusikilizwa kwa kesi hiyo. Katika kusikilizwa kesi Mdai na Mdaiwa wote hupewa fursa ya kutoa maelezo yao kama yalivyo katika hati ya madai na majibu yake na pia kutoa ushahidi pamoja na vielelezo Mahakamani. Vile vile wote hupewa fursa ya kuita mashahidi wao kama wanao ili kuja kuthibitisha kesi. Kawaida yule aliyefungua kesi ndie anaeanza kutoa maelezo yake na kuwaita mashahidi wake kutoa ushahidi na wakati huo huo Mdaiwa hupewa fursa ya kuuliza maswali. Baada ya kumaliza Mdai hufunga kesi yake na kuamuachia Mdaiwa atoe maelezo yake na kuita mashahidi wake na Mdai nae hupewa fursa ya kuuliza maswali. Baada ya yote kukamilika uendeshaji wa kesi huwa nao umekamilika na masuala yote hubakia kwa Jaji au 58 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Hakimu kutegemea kesi hiyo inasikilizwa na Mahakama gani, na yeye hutakiwa kutoa hukumu. Hatua hizi hazifanyiki kwa siku moja, hutegemea ukubwa wa kesi na wingi wa mashahidi na pia shughuli za Mahakama. Mara nyingine kesi huweza kuchukua miezi sita hata miaka miwili au zaidi. Hivyo, ni jambo la kulifikiria sana kwani fedha na muda hupotea. Ikiwa mzozo wa madai unaweza kusuluhishwa nje ya Mahakama ni vyema ikafanywa hivyo, na ile inayoshinda ndio ikapelekwa mahakamani. 2.4.1.3 Ukomo wa Ufunguzi wa Kesi ya Madai Ufunguaji wa kesi ya madai nao umeekewa kikomo. Hii ina maana kwamba mtu awe muangalifu unapotokea mzozo au mgogoro asikae muda mrefu kabla ya kufungua kesi. Jambo hili pia linamlinda yule anayedaiwa pia kwamba asije akaburuzwa Mahakamani kwa kitu kilichofanyika au kupita miaka mingi iliyopita. Sheria ya Ukomo wa ufunguaji wa kesi, Sura ya 7 ya Sheria za Zanzibar ndio iliyowekwa viwango ambavyo huangaliwa kabla ya kesi kufunguliwa. Ikiwa viwango vimeshapitwa na wakati basi kesi haiwezi kufunguliwa, au ikiwa imefunguliwa bila ya kutambua kasoro hiyo. Kesi hiyo hufutwa mara kasoro hiyo inapotambulika. Sheria imeweka kuwa baadhi ya kesi ukomo wake ni mwaka mmoja, kwa mfano kudai mshahara au malipo mengine kwa ajili ya kazi, kudai kodi ya nyumba, kudai pale mwenye gari au mchukuzi anapoharibu mazao. Pia yapo makosa yaliowekewa miaka miwili kuwa ni ukomo wa kufungua kesi, kwa mfano, pale mtu aliyepewa dhamana ya kitu anapokifanya kitu hicho kuwa mali yake. Vile vile yapo makosa yaliyoekewa miaka mitatu kuwa ni ukomo wake kwa mfano kuingilia mali ya mtu, kudai mali ya wazi, kudai Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 59 pesa kwa aina yoyote ile, uvunjaji wa mikataba, kudai mahari yaliyopangwa kulipwa baadae, kudai kodi ya nyumba iliyobakia n.k. Vile vile yapo makosa ambayo ukomo wake ni miaka sita na miaka kumi na mbili. Hivyo, ni muhimu kuangalia muda huu uliowekwa kabla ya kuchukua hatua ya kufungua kesi ambayo inagharama. 2.4.2 Sheria ya Mikataba 2.4.2.1 Maana ya Mkataba Mkataba ni njia moja ambayo watu hujitungia sheria wenyewe kwa kuweka majukumu na haki zinazoongoza makubaliano yao. Mkataba hufanywa baina ya watu wawili au zaidi. Katika hali ya kawaida unapokubaliana na mtu mwengine kumfanyia jambo fulani na mtu huyo akakubali kukulipa kwa kufanya jambo hilo tunasema kwamba mmeingia kwenye makubaliano. Ikiwa makubaliano hayo yanaweza kutekelezwa kisheria tunasema kuwa huo ni mkataba. Kwa mfano, ukikubali kufanya kazi kwa mtu na mtu huyo akakubali kukulipa kwa kazi uliyofanya tunasema kwamba umeingia katika mkataba wa ajira. Wewe unayefanyakazi unakuwa mwajiriwa na yule unayemfanyia kazi na ambaye anakulipa ni mwajiri. Ili makubaliano yaweze kutekelezeka kisheria ni lazima yawepo mambo yafuatayo: (i). Wahusika wa makubaliano hayo wakubali na wawe na nia ya kuingia katika mahusiano yatakayoongozwa na sheria; (ii). Wahusika wa makubaliano hayo wawe na uwezo wa kuingia mkataba. Hapa uwezo maana yake wawe ni watu wazima wenye kuweza kutoa maamuzi na pia wawe na akili timamu, kwani mkataba na mwendawazimu ni batili kisheria; 60 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: (iii). Wahusika waingie katika makubaliano yao kwa ridhaa yao wenyewe, yaani visitumike vitisho, nguvu wala ujanja au udanganyifu; (iv). Malengo ya makubaliano hayo yawe ya halali, yaani makubaliano yasiwe na malengo yasiyokubalika kisheria kama vile kuua, kuuza bangi n.k. Vile vile na malipo nayo yawe na uhalali; yaani isiwe unalipwa kitu kisichofaa kwa mfano unapewa kazi ya kulima lakini malipo yake ni gunia la bangi; (v). Makubaliano yasiende kinyume na sera ya taifa au batili. Kwa mfano sera ya Taifa inapinga suala la uwekaji wa madanguro. Hivyo, makubaliano yoyote kwa mfano ya kufanya kazi katika danguro yatakuwa yanakwenda kinyume na sera ya Taifa na hivyo hayataongozwa na Sheria; na (vi). Makubaliano yasiwe batili. Zipo njia nyingi ambazo zinaweza kubatilisha makubaliano na hivyo yasiweze kutekelezwa kisheria. Kwa mfano kufanya makubaliano na mtoto mdogo. 2.4.2.2 Aina ya Mkataba Mkataba unaweza kuwa: (i). Kwa njia ya Maandishi; (ii). Kwa njia ya mdomo; (iii). Sehemu ya Mkataba ipo kwa maandishi na sehemu nyingine kwa mdomo; na (iv). Unatokana na vitendo vya wahusika. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 61 2.4.2.3 Masharti ya Mkataba Masharti ya mkataba ni yale maelezo yaliyomo ndani ya mkataba ambayo yanaweka wazi majukumu ambayo wahusika wa mkataba huo wanatakiwa wayatekeleze, pamoja na kuweka haki ambazo wahusika wa mkataba huo wanazo. Masharti ya Mkataba yapo yaliyo waziwazi ambayo huandikwa ndani ya mkataba wenyewe, na yapo yaliyokuwa hayaandikwi lakini yanafahamika kuwa yapo kutokana na kuwekwa katika sheria inayoongoza mambo hayo au kutokana na tabia iliyojengeka katika biashara fulani. Kwa mfano katika mkataba wa ajira hutaja mambo mengi lakini si kawaida kutajwa kwa likizo ya kawaida au likizo ya uzazi au mapumziko ya siku moja kwa wiki kwa sababu mambo haya tayari yameshawekwa katika Sheria. Au kwa mfano unapopeleka kitu mnadani kuuziwa ukifika pale hufanyi makubaliano na dalali kwamba akuzuie kitu ulichopeleka na yeye utamlipa kiasi gani, bali inaeleweka kutokana na tabia ya pahali hapo kwamba malipo ya udalali yanafanywa kwa njia fulani na kiasi fulani. Baada ya mkataba kukamilika hairuhusiwi kuingiza masharti mapya katika mkataba huo. Ikiwa Wahusika wanataka kuongeza kitu ni lazima wasitishe mkataba wa awali na wafanye mkataba mwengine. Vyenginevyo mkataba huo uwe unaruhusu kufanyiwa marekebesho. 2.4.2.4 Sifa za Mikataba Katika kuangalia sifa za mikataba, ipo mikataba ifuatayo: (i). Mkataba usiyotekelezeka ± huu ni mikataba ambao una masharti ndani yake ambayo ni lazima yatekelezwe. Hivyo, ikiwa sharti au masharti hayo hayajatekelezwa mkataba huo nao unakuwa hautekelezeki. (ii). Mkataba unaoweza kuvunjwa na mmoja ya wahusika wa mkataba na sio mhusika mwengine. Mkataba huu unakuwa ni halali lakini mmoja wao anaweza akitaka kuuvunja. Kwa 62 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: mfano ikiwa mkataba umefungwa lakini mmoja wao kalazimishwa, au hakutoa ridhaa yake. Mtu huyo anaweza kuuvunja mkataba huo. (iii). Mkataba haramu ± huu ni mkataba ambao malengo yake na malipo yake sio halali, kwa mfano mkataba wa kuuza madawa ya kulevya, au bangi. (iv). Mkataba unaokwenda kinyume na Sheria ± Mikataba hii pia huwa si halali na haiwezi kutekelezeka. Kwa mfano Sheria ya Karafuu inapiga marufuku kwa mtu yeyote kuuza karafuu kwa mtu mwengine asiyekuwa Shirika la Biashara la Zanzibar ( Zanzibar State Trading Corporation ± ZSTC). Hivyo, ukiuza kwa mtu mwengine na mtu huyo akikataa kukulipa huwezi kupeleka suala lako Mahakamani kudai. (v). Mkataba unaokwenda kinyume na Sera ya Umma. Mkataba wa aina hii ni ule unaopingana na sera ya nchi kama uwekaji wa madanguro, kuwafanyisha kazi watoto n.k. (vi). Mkataba ambao sio halali tangu awali ± huu ni mkataba ambao mtu anaingia kwa mfano na mtoto. Kwa kuwa mtoto hana uwezo wa kuingia mkataba, mkataba huo unakuwa sio halali. Mfano mwengine ni mkataba na mwandawazimu au mlevi, wote hawa hawawezi kutoa ridhaa kwa wakati huo hivyo mkataba huo nao sio halali. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 63 SURA YA TATU Sehemu ya Kwanza 3.0 Haki za Binadamu Haki za binadamu kama dhana inamaanisha matakwa, haki au madai ya msingi ambayo binadamu anastahiki kutoka mamlaka ya kuitawala.Dhana ya haki za binadamu imejengeka katika kuamini kuwa kimaumbile kila binadamu ana mambo ya msingi ambayo anapaswa kuyapata kama vile ni sehemu ya ubinadamu wake. Yaani, sifa kubwa ya kupata stahiki ya haki za binadamu ni ile ya kuwa binadamu; na kwamba binadamu alipo popote na wakati wowote anasitahiki kupata matarajio yake muhimu yanayoelezeka kwa jina 3.1 Chanzo cha Haki za Binadamu Swali linaweza kuulizwa. Ni vipi tumeweza kuzitambua haki hizo za binadamu? Jibu la msingi ni kuwa kimaumbile, kama binadamu, tuna mahitaji maalum ambayo ni muhimu kuyapata kwa ajili ustawi wetu. Miongoni mwa mahitaji hayo muhimu tunaweza kutaja chakula, mavazi, makaazi, elimu, ajira na mahusiano mema na watu wengine. Katika mkusanyiko wa mahitaji yote haya na mengineyo, yapo kuyatambua kwa kutumia maarifa au akili ambayo ni moja kati ya sifa ya msingi ya binadamu. 64 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 3.2 Sheria za Kimataifa na Haki za Binadamu Wimbi la sasa la mataifa kadhaa duniani kutilia mkazo masharti ya kisheria yanayolinda haki za binadamu asili yake ni juhudi za makusudi za Umoja wa Mataifa za kuinua thamani ya utu wa binadamu kufuatia kunyanyasika kwa binadamu kabla na wakati wa vita vikuu vya pili vya dunia. Sehemu hii itaelezea kwa ufupi kuhusu juhudi za Umoja wa Mataifa na baadhi ya Jumuiya nyingine za Kimataifa katika kuendeleza dhana ya haki za binadamu. Maelezo yanayotolewa hapa ni kwa mujibu wa Mikataba tofauti ya Kimataifa. 3.2.1 Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa 1945 Kipengele cha kwanza kabisa katika juhudi za mataifa za kukuza suala la haki za binadamu ni kile kiliopo kwenye dibaji ya Mkataba wa Umoja wa Mataifa( United Nations Charter), wa mwaka 1945 kutilia maanani suala la haki za binadamu, katika kuheshimu na kuthamini utu wa kila binadamu, katika hali sawa kati ya mwanamume na mwanamke na katika mataifa makubwa na madogo Katika ibara ya 1 ya Mkataba huu wa Umoja wa Mataifa imeelezewa pia kuwa malengo ya Umoja wa Mataifa ni pamoja na Masharti muhimu zaidi katika Mkataba huu ni yale yaliyoelezewa kwenye ibara za 55 na 56. Ibara 55 inaeleza kuwa Umoja wa Mataifa unawajibika kukuza utekelezaji wa masharti ya haki za binadamu na uhuru kwa kila binadamu bila kujali tofauti za ukabila, Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 65 wanachama zinahakikisha kuwa hatua binafsi na hatua za pamoja Ibara nyingine muhimu ni ibara ya 13 inaipa mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa( General Assembly) uwezo wa kutoa mapendekezo juu ya kukuza haki za binadamu; ibara ya 68 inalitaka Baraza Kuu la Umoja wa Mataifa( The Council) kuunda Tume kwa ajili ya ukuzaji wa haki za binadamu; na ibara ya 76 ambayo inaelezea kuwa ukuzaji wa haki za binadamu ndio lengo kuu la ushirikiano wa kimataifa. 3.2.2 Tangazo la Haki za Binadamu la 1948 Mkataba wa Kimataifa( UN Charter) ambao ulisainiwa mnamo June 1945 ulianza kutekelezwa mnamo Octoba mwaka huo huo. Hapo iliamuliwa kuwa Baraza la Kiuchumi na Kijamii la Umoja wa Mataifa( Economic and Social Council au ECOSOC) lianzishe Tume ya Haki za Binadamu ambayo itapewa kazi ya kutunga Sheria za Kimataifa juu ya Haki za Binadamu. Maamuzi hayo yaliungwa mkono na Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mnamo Februari 12, 1946. Siku nne baadae, Baraza la Kiuchumi na Kijaamii (ECOSOC) lilianza kazi hiyo, na miezi michache baadae tume ya Kimataifa ya Haki za Binadamu iliundwa na kufanya mkutano wake wa kwanza mnamo Januari 1947. Katika kutekeleza shughuli zake Tume hii ilitengeneza Tamko la Umoja wa Mataifa la Haki za binadamu( Universal Declaration of Human Rights) ambalo baada ya marekekbisho kadhaa lilikubaliwa katika Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa mnamo Disemba 10, 1948 kwa kuungwa mkono na mataifa yote 48 wanachama wa Umoja wa mataifa yaliyohudhuria mkutano huo. Mataifa 8 wanachama ndio hayakuhudhuria. 66 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Tangazo la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu lenye jumla ya Ibara 30 limeweka misingi muhimu ya haki za binadamu kama vile:(i). Haki ya usawa binadamu(ibara 1 na 2); (ii). Haki ya maisha, uhuru wa usalama(ibara 3); (iii). Haki ya mtu kutofanywa mtumwa(ibara 4); (iv). Haki ya mtu ya kutoteswa, kufanyiwa ukatili wa kupewa adhabu inayodhalilisha(ibara ya 5); (v). Haki ya Usawa mbele ya sheria(ibara 6 na 7); (vi). Haki ya mtu kupata nafuu ya kisheria ndani ya nchi yake kutokana na tendo la kuvunjiwa haki yake(ibara 8 na 10); (vii). Haki ya mtu ayeshtakiwa kutotendewa kama mwenye kosa mpaka kosa lake lithibitishwe katika kesi kwa mujibu wa sheria za nje zinazofaa(ibara 11); n.k. Kitu cha msingi kufahamika katika hatua hii ni kuwa masharti ya kisheria yaliyomo ndani ya Tangazo la Haki za Binadamu la 1948 yana lengo la kuweka vigezo maalum kuhusu masharti ya Haki za binadamu kwa ajili ya kuigwa na mataifa, lakini, Tangazo hili halikukusudiwa kuwa na nguvu za kisheria zinazolazimisha mataifa kufuata maamrisho yake. Kutokana na hali hiyo pamoja na Tangazo la Haki za binadamu kujijengea heshima kubwa kutokana na mataifa mengi wanachama na yasiyo wanachama kufuata mwelekeo wake, bado ilionekana kuwepo haja ya kupata sheria za kimataifa ambazo ni madhubuti zaidi katika kuzilamisha nchi wanachama kutekeleza masharti yake. Ili kutekeleza azma hiyo iliamuliwa kuwa iwepo mikataba ya kimatifa inayoweka masharti ya kulazimisha nchi wanachama kutekeleza masharti ya haki za binadamu na pia kuweka masharti ya namna ya kupima utekelezaji. Hatimae mikataba miwili ya kimataifa,(i) kuhusu haki za kiraia na kisiasa( International Covenant of Civil and Political Rights- ICCPR), na(ii) kuhusu haki Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 67 za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni( International Covenant on Economic, social and Cultural Rights- ICESCR). 3.2.3 Mkataba wa Kimataifa Juu ya Haki za Kiraia na Kisiasa Mkataba wa Haki za Kiraia na kisiasa ilisainiwa tarehe 16 Disemba, 1966 na kuanza kutumika mnamo tarehe 23 March 1976 na hadi kufikia 1998 mataifa 95 tayari yalikuwa yameridhia. Haki zinazolindwa kwa mujibu wa Mkataba huu zimeelezea katika ibara 22; kuanzia ibara ya 6 hadi ibara ya 27, kama ifuatavyo:(i). Haki ya kuishi(ibara 6); (ii). Haki ya kutoadhibiwa kinyama(ibara 7); (iii). Haki ya kutofanywa mtumwa na kulazimishwa kufanya kazi (ibara 8); (iv). Haki ya uhuru na usalama(ibara 9); (v). Haki ya mtu aliepo kizuizini kutoadhibiwa(ibara 10); (vi). Haki ya kutofungwa kutokana na deni(ibara 11); (vii). Haki ya mtu kwenda na kuishi atakapo(ibara 12); (viii). Haki ya wageni ya kutofukuzwa kinyume na taratibu za kisheria(ibara 13); (ix). Haki ya mtu kusikilizwa ipasavyo katika kesi(ibara 14); (x). Kinga dhidi kutumika kwa sheria ya sasa kwa makosa ya jinai yaliyopita(ibara 15); (xi). Haki ya utu wa mtu kutambuliwa kwa mujibu wa sheria (ibara 16); (xii). Haki ya faragha(ibara 17); (xiii). Uhuru wa mawazo, kuamini na kuabudu(ibara 18); (xiv). Uhuru wa maoni na kujieleza(ibara 19); (xv). Makatazo ya uchochezi wa kivita, ushongelezaji wa mataifa, ubaguzi na chuki za kidini(ibara 20); (xvi). Haki ya kuandamana katika hali ya amani(ibara 21); (xvii). Uhuru wa kuunda jumuiya(ibara 22); (xviii). Haki ya kuoa/kuolewa na kuanzisha familia(ibara 23); 68 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: (xix). (xx). (xxi). (xxii). Haki ya mtoto(ibra 24); Haki za kisiasa(ibara 25); Usawa mbele ya sheria(ibara 26); na Haki za wachache katika jamii(right of Minorities) ibara 27). 3.2.3.1 Chombo cha Utekelezaji Katika kuhakikisha kuwa masharti ya Mkataba huu yanatekelezwa na mataifa wanachama, ibara 28 ya Mkataba wa Haki za Kiraia na kisiasa imeanzisha Kamati Maalum ya Haki za Binadamu katika ngazi ya Umoja wa Mataifa. Kamati ya Haki za Binadamu ina wajumbe 18 ambao ni wawakilishi wa nchi wanachama wa mkataba wa Haki za Kiraia na kisiasa na ambao pia ni watu wenye hadhi na uwezo mkubwa katika maswala ya haki za binadamu. Wajumbe hao hupatikana kwa kura za siri zinazopigwa katika mkutano maalum ulioitishwa na Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa ajili hiyo (ibara 29 na 30). Kazi za Kamati ya Haki za Binadamu ni kupokea malalamiko kutoka kwa nchi ambayo ni mwanachama wa Mkataba wa Haki za Kiraia na kisiasa na ambayo imeukubali uwezo wa Kamati binaadamu. Masharti na taratibu za Kamati ya Haki za binadamu kuweza kufanya kazi zake imeelezwa katika ibara 41. 3.2.4 Mkataba wa Kimataifa Juu ya Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni Mkataba huu ulitiwa saini siku moja na ule mkataba wa Haki za Kiraia na kisiasa, mnamo tarehe 16 December 1966, na kuanza kufanyakazi mnamo tarehe 3 Januari 1976, baada ya kuridhiwa na mataifa 99. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 69 Mkataba huu unahusu masharti yanayolinda haki za watu zinazohusu mambo ya uchumi na hali za maisha ya watu kwa ujumla. Masharti yenye kulinda haki yamewekwa kwenye ibara 24 kuanzia ibara ya 2 hadi 25. Kwa ufupi ibara hizi zinaweka masharti kuhusu haki ya kufanya kazi, haki ya kupata ujira unaostahiki, haki ya makaazi, haki ya elimu, haki ya afya na haki zinazohusiana na mambo ya starehe. Haki zinazoelezewa hapa zimepewa jina la Generation 5LJKWV´ kwa sababu ya kuwepo zile Haki za Kiraia na Kisiasa ambazo zimepewa umuhimu wa kwanza(i.e. First Generation Rights). 3.2.4.1 Chombo cha Utekelezaji Tofauti na zile Haki za Kiraia na Kisiasa ambazo utekelezaji wake umeundiwa Kamati maalum(ie. Kamati ya Haki za binadamu), utekelezaji wa Haki za Kiuchumi, Kijamii na Kiutamaduni unasimamiwa na &RXQFLO´ . Namna ya usimamizi wa utekelezaji wake unategemea zaidi taarifa ambazo mataifa wanachama wanatakiwa kupeleka kwa Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa kwa mujibu wa ibara 16 na 17. Baada ya Katibu Mkuu huyo kupokea taarifa ya utekelezaji wa haki hizi za binadamu ndio anaituma kwa ECOSOC kwa kuzingatiwa na kuchukuliwa hatua kwa mujibu wa ibara 18, 19, 20, 21 na 22. 3.3 Mikataba ya Kikanda Mbali na mikataba miwili iliyoelezewa hapo juu kuhusu haki za binadamu na ambayo inasimamiwa na Umoja wa Mataifa, zipo juhudi kadhaa za kikanda katika Jumuiya za kimataifa zinazoshughulikia ukosaji na ulindaji wa haki za binaadamu. Kutokana na Juhudi hizo, Mikataba ifuatayo kuhusu haki za 70 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: binadamu imeweza kufanikiwa, lakini miongoni mwa hiyo tutauangalia mmoja tu: (i). The European Convention on Human Rights, 1950; (ii). The American Convention on Human Rights 1969; (iii). The Permanent Arab Commission on Human Right 1979; na (iv). 3.3.1 Mkataba wa Afrika Juu ya Haki za Binadamu na Haki za Watu wa 1981 Kufuatia kuanzishwa kwa Mikataba ya Haki za Binadamu ya Ulaya ( Europe) na Marekani, Umoja wa mataifa huru ya Africa yalifanya mikutano kadhaa mnamo 1958 na 1962 kuzungumzia bila mafanikio haja ya kuwa na Mkataba wa Afrika kuhusu haki za Binadamu. Hatimae mnamo 1969 mataifa 20 ya Afrika yalikubaliana juu ya haja ya kuwepo kwa suala hilo. Hata hivyo iilikuwa ni kwenye mkutano wa wakuu wa Nchi za Africa Monrovia mnamo July, 1979 Maamuzi hayo pia yalimtaka Katibu Mkuu wa OAU kuteua kundi la wataalamu kwa ajili ya kuandika mkataba huo. Kundi hilo la wataalamu liliifanya kazi hiyo huko Dakar mnamo mwaka huo huo wa 1979. Baada ya kuangaliwa na kurekebisha, Mkataba huo baadae ulisainiwa katika Mkutano wa Wakuu wa Nchi za Afrika waliokutana mjini Nairobi mnamo June 1981. Mkataba huo ulianza kufanya kazi mnamo Octoba 1986. Mkataba wa Afrika wa Haki za Binadamu na Watu umechanganya kwa pamoja baadhi ya haki zinazolindwa kwa mujibu wa Mkataba wa Umoja wa Mataifa wa Haki za Kiraia na kisiasa na ule wa Haki za kiuchumi, kijamii na kiutamaduni. Haki za kiraia na kisiasa zinapatikana kwenye ibara 3 hadi 16; na zile zinazohusu Haki za Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 71 kiuchumi, kijamii na kiutamaduni zipo kwenye ibara 17 na 18 katika mkataba wa Afrika. Utekelezaji wa Mkataba huu unasimamiwa na Tume ya Afrika ya Haki za Binadamu. 3.4 Haki za Binadamu ni Haki za Kisheria? Sifa moja kuu ya masharti ya ukuzaji na ulindaji wa Haki za binadamu ni kuwa ni masharti ya kimikataba ya Kimataifa. Mbali na kutoa vigezo kwa mataifa yanayohusika kuvifuata, mikataba hiyo inaweka masharti ambayo yanatakiwa kutekelezwa na mataifa wanachama kadri ya masharti yenyewe yalivyo. Kwa maana hiyo ni kuwa, kwa kiasi kikubwa, masharti hayo yanahusu mahusiano maalum kati ya nchi na nchi. Na kama tulivyoona hapo juu, utekelezaji wake hausimamiwi moja kwa moja na Mahakama za nchi wanachama. Na kwa maana hiyo, Mikataba ya Kimataifa haina nguvu za moja kwa moja za kisheria ndani ya nchi husika, isipokuwa kwa kile kiasi tu ambacho nchi inayohusika imeipa nguvu za kisheria kwa mujibu wa sheria za nchi hiyo, uzoefu ulivyo ni kuwa mataifa huwa yanachukua baadhi tu ya masharti ya haki za binadamu kutoka kwenye Mikataba ya Kimataifa na kuyaweka kivyake katika sheria za nchi. 3.5 Katiba na Historia Fupi ya Haki za Binadamu Zanzibar Mwishoni mwa miaka 1950 na mwanzoni mwa miaka 1960, wakati makoloni yanaelekea kupata uhuru, suala la kuwepo kwa masharti ya kikatiba yanayolinda haki za binadamu lilitawala mjadala. Watu ambao waliibua mijadala hiyo ni wakoloni wenyewe ambao wakati wa utawala wao suala la haki za binadamu hawakuwahi kulitaja. Ni wakati ukoloni unaelekea kumalizika ndio wakapigania masharti kuhusu haki za binadamu yawemo kwenye katiba za uhuru. Katika hili wakoloni hawakuwa wapumbavu. Ingawa utawala wa ukoloni 72 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: hapa. Pia walikuwa na mali zao nyingi. Masharti kuhusu haki za binadamu katika Katiba yalihitajika hasa kuwalinda hawa wageni na mali zao dhidi ya nguvu ya serikali mpya zisizotabirika. Tofauti na hali ilivyokuwa huko Tanzania Bara, ambapo Chama cha Tanganyika African National Union(TANU) chini ya uongozi wa Mwalimu Julius K. Nyerere ilifanikiwa kutoingiza masharti hayo kwenye Katiba ya uhuru(Katiba ya Tanganyika 1961). Katiba ya uhuru wa Zanzibar ilibeba sura nzima yenye masharti kuhusu haki za binadamu. Hata hivyo Katiba hiyo ilipigwa marufuku kufuatia mapinduzi ya Zanzibar ya tarehe 12 Januari, 1964. Mnamo tarehe 31 Januari 1964, Baraza la Mapinduzi lilitunga sheria iliyojulikana kw baada ya kushauriana na kwa ridhaa ya Baraza la Mapinduzi. Sheria hiyo yenye vifungu viwili tu ilitiwa saini na wajumbe 30 wa Baraza la Mapinduzi. Hapakuwa na Katiba nyingine ya Zanzibar kabla ya kufikia 1979. Mnamo 1979 Zanzibar, chini ya uongozi wa Mzee Aboud Jumbe iliamua kupanua wigo wa demokrasia na hivyo kupitisha Katiba ya Zanzibar ya 1979 ambayo, pamoja na mambo mengine ilianzisha Baraza la Wawakilishi kuwa ni Baraza la Kutunga Sheria. Hata hivyo Katiba hiyo ya Zanzibar 1979 haikuwa na masharti yoyote kuhusu haki za binadamu. Mnamo 1984 Baraza la Wawakilishi Zanzibar liliifuta Katiba ya Zanzibar 1979 na kupitisha Katiba ya Zanzibar 1984 ambayo ndio inatumika hadi sasa, ingawa imewahi kufanyiwa marekebisho mara kadhaa. Katiba hii ndio ina sura nzima, ambayo ni sura ya tatu, yenye kuweka masharti kuhusu haki za binadamu. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 73 3.6 Misingi ya Haki za Binadamu Haki za raia ni haki za misingi ambazo raia kama binadamu huzaliwa nazo. Kwa sababu ni binaadamu, basi kila mtu ana haki ambazo ni zake. Haki hizi ni zile ambazo raia katika jamii inayoendeshwa kwa misingi ya kidemokrasia hawezi kunyanganywa na mamlaka yeyote ile.Haki hizi zina falsafa yake ambayo asili yake ni katika Sheria za Kimataifa na ni wajibu wa Utawala wa nchi kuzitambua na kuzilinda kwa mujibu wa Sheria za nchi husika. Katika nchi nyingi zilizopiga hatua katika maendeleo ya kidemokrasia, haki hizi huwa zinalindwa ndani ya Katiba ya nchi. Hivi ndivyo ilivyo kwa Katiba ya Jamhuri ya Muungano, na pia kwa Katiba ya Zanzibar. Lengo la kuingiza masharti yanayohusu haki za raia katika Katiba ni kuhakikisha kuwa kulindwa kwa haki hizo kuna nguvu za kikatiba. Endapo kuna sheria nyingine yoyote inakwenda kinyume na haki za msingi za raia, Sheria hiyo inakuwa ni batili kwa sababu imeikiuka Katiba, na ni batili kwa kiasi kile kile inachoikiuka Katiba. Kimantiki, Vifungu 11 hadi 21 vya Katiba ya Zanzibar inazungumzia haki za msingi za raia. Badhi ya haki hizo ni kama ifuatavyo. 3.6.1 Haki za Kutambuliwa na Kuthaminiwa Dhana ya msingi juu ya haki hii ni kuwa ubinadamu wa binadamu yeyote hupatikana kwa kuzaliwa kwake kama binadamu. Baada ya kuzaliwa tu ana haki ya kutambuliwa kwake kama binadamu, na haki nyingine zote ambazo binadamu anastahiki kupata ikiwa ni pamoja na kupewa jina na kutambuliwa uraia wake. 74 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 3.6.2 Haki za Usawa Hii ni haki ya kwanza inayojitokeza katika Tamko la Umoja wa Mataifa la Haki za Binadamu. Kwamba binadamu wote wanazaliwa wakiwa sawa katika hali ya ubinadamu. Anakuwa binadamu bila ya kujali asili ya utaifa wake, kabila yake, dini yake, jinsia yake, rangi yake, wala nafasi yake katika maisha ya kijamii. Kwa sababu binadamu wote ni sawa, inatakiwa usawa wao upewe nguvu kwa mujibu wa Sheria. Ndio kifungu 11(a) ya Katika ya Zanzibar 1984 3.6.3 Haki ya Hifadhi ya Maisha Haki hii ya raia ina sehemu mbili (i). Haki ya kulinda nafsi au mwili wa kila raia dhidi ya mashambulizi yanayoweza kuathiri uhai wake; na (ii). Haki ya kulindwa maisha yake kwa kumuwekea mazingira ya kuweza kumudu maisha yake. Hii imeelezewa kuwa ni haki ya msingi kwa sababu bila ya maisha ya mtu hatuwezi kuzungumzia utu wake. 3.6.4 Haki ya Kutoteswa au Kuadhibiwa Kinyama Haki hii inalenga kuwaondolea raia uonevu kutokana na mikono au nguvu za dola, au kutoka miongoni mwa raia wenyewe kwa wenyewe.Katika Katiba ya Zanzibar 1984 masharti yanayohusiana na haki hii yamewekwa chini ya kifungu 14 ambayo inazungumzia Haki ya Uhuru wa mtu binafsi. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 75 3.6.5 Uhuru wa Maoni na Kupata Taarifa Uhuru huu una madhumuni ya kulinda haki mbili muhimu:(i). Haki ya kujieleza na kusambaza maoni kwa watu wengine; na (ii). Haki ya kupokea habari kutoka kwa wengine. Kifungu cha 18(1) cha Katiba ya Zanzibar 1984 kinaweka masharti maoni yoyote na kutoa nje mawazo yake, kutafuta, kupokea na kutoa habari na dhana kupitia chombo cho chote, bila ya kujali mipaka ya nchi na pia ana uhuru wa mawasiliano yake kutoingiliwa 3.6.6 Uhuru wa Imani na Kuabudu Kwa mujibu wa kifungu ya 19 ya Katiba ya Zanzibar 1984, kila mtu ana uhuru wa mawazo, imani ya dini na kuchagua kufuata dini yoyote ambayo anapenda. Pia kila mtu yupo huru kubadilisha dini akiona kufanya hivyo inafaa. 3.6.7 Uhuru wa Kujikusanya Haki hii inampa raia uhuru wa kujikusanya na raia wengine kwa lengo la kufanya umoja au ushikamano wowote kwa lengo lolote lenye manufaa na ambalo haliendi kinyume na sheria za nchi. Katika Katiba ya Zanzibar 1984 maelezo ya namna hiyo yapo chini ya kifungu 20(1) na(2). 3.6.8 Uhuru wa Kufanya Kazi na Kupata Ujira Kila mtu ana haki sawa ya kuweza kufanya kazi kulingana na kazi ambayo ipo na uwezo ambao anao. Kwa maana nyingine, raia hapaswi kubaguliwa katika masuala ya ajira. Pia endepo atafanya kazi, raia yeyote ana haki ya kupata ujira unaolingana na kazi yake katika mazingira yaliyopo. Pia hakutakuwepo na kazi ya 76 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: kulazimishwa. Kifungu cha 21 na 22(2) vya Katiba ya Zanzibar zinaweka masharti kuhusiana na haki hiyo. 3.6.9 Uhuru wa Mtu Kwenda Atakako Chini ya kifungu 16 cha Katiba ya Zanzibar 1984 kila mtu ana haki ya uhuru wa kwenda popote katika Zanzibar, haki ya kuishi hapo, na pia haki ya kuingia na kutoka Zanzibar. Haki zote hizi zinapaswa kutekelezwa kwa mujibu wa sheria za nchi. 3.6.10 Uhuru wa Faragha Chini ya kifungu 15(1) ya Katiba ya Zanzibar, kila mtu anastahili kuheshimiwa na kupata hifadhi kwa nafsi yake, maisha yake binafsi na ya nyumbani kwake, na pia heshima na hifadhi ya maskani yake na mawasiliano yake. Hata hivyo, kifungu 15(2) kinaelezea kuwa mamlaka ya nchi itaweka sheria inayoweka mipaka utekelezwaji wa haki hii. 3.7 Wajibu wa Raia Katiba ya Zanzibar ya 1984 inaweka wazi wajibu wa raia kwa nchi yao kuwa ni: (i). Wajibu wa kuheshimu sheria za nchi, kulinda mali za taifa na kutoingilia uhuru wa mtu mwengine; (ii). Kupiga vita aina zote za uharibifu na ubadhirifu wa mali za umma; (iii). Kulinda, kuhifadhi na kudumisha uhuru, mamlaka, ardhi na umoja wa Zanzibar; na (iv). Kulinda maliasili za Zanzibar, mali ya nchi na mali yote inayomilikiwa kwa pamoja na Wananchi. Raia pia ana wajibu wa kuheshimu mali ya mtu mwengine. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 77 Haya ni masharti ya Kifungu 22 hadi 24 vya Katiba ya Zanzibar 1984. 3.8 Katiba na Utawala Bora Utawala Bora sio tamshi la kisheria tu, lina mizizi iliyojengeka ndani ya Katiba. Tamshi hili ambalo ni maarufu sana katika zama hizi za sasa linamaanisha mambo mawili makubwa ambayo ni utawala wa kidemokrasia, ambao unaoendeshwa kwa mujibu wa Sheria. kwa sababu Katiba ya Zanzibar 1984 imeweka bayana katika wa Vyama vingi vya Siasa wenye kuheshimu utawala na Sheria, Hii ndio misingi ambayo endapo itafuatwa ipasavyo itazaa utawala ambao ni bora. Katika mtazamo wa Kikatiba, tunapokuwa na vyama vingi katika nchi, vyama hivyo vitashindana kwa sera na kuwepo na uchaguzi wa kidemokrasia., Uchaguzi wa kidemokrasia ni ule unaoendeshwa kwa uhuru na haki. Wananchi mara zote wanapendelea Serikali ambayo kutokana na sera zake ni madhubuti katika kuhakikisha umakini wa mipango na utawala wake. Lengo ni kuhakikisha kuwa kuna maendeleo endelevu katika nchi kutokana na mipango iliyoandaliwa vizuri na kutekelezwa kwa kufuata haki, usawa, amani, haki za binadamu na ushirikishwaji wa wananchi katika kuamua mambo yanayowahusu. Utawala bora ni ule unaothamini uhuru wa mawazo (ikiwa ni pamoja na uhuru wa vyombo vya habari) na uhuru wa wananchi kujiunga na vikundi vya hiari vyenye nguvu kwa maslahi ya maendeleo yao na nchi yao. 78 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 3.8.1 Misingi Muhimu ya Utawala Bora Haja ya utawala bora sio tu kutokana na matamshi mazuri ya maneno yenyewe, bali ni kutokana na umuhimu wa dhana yenyewe katika kuweka misingi muhimu ya siasa endelevu, jamii endelevu, uchumi endelevu na ustawi mzuri wa watu na hulka zao. Kwa maana hiyo athari ya utawala bora haikusudiwi tu kwenye siasa, bali zaidi kwa ajili ya kuimarisha maisha ya binadamu mmoja mmoja kihali na mali na hivyo hivyo kwa maisha ya jamii na kuyafanya yawe ni maisha endelevu. Utawala bora unapatikana pale ambapo upo utaratibu unaohakikisha kuwa nguvu na uwezo wa nchi unatumika kwa maslahi ya jamii katika mtazamo mzima wa mahusiano ya watu, vikundi vya watu na taasisi za umma katika jamii husika. Kwa ujumla mambo yafuatayo ndio yanayojenga misingi ya utawala bora: (i). Misingi mizuri ya Katiba ya nchi inayozingatia mgawanyo wa madaraka miongoni mwa mihimili mikuu ya utawala wa nchi. Msingi huu unakusudia kuhakikisha kuwa upo mgawanyo unaokubalika wa nguvu za dola miongoni mwa taasisi za nchi na kuhakikisha kuwa kila muhimili unafanya shughuli zake ipasavyo bila ya kuingilia shughuli za muhimili mwengine. (ii). Utawala wa Sheria: ili kuhakikisha kuwa nchi inaongozwa kwa misingi inayokubalika na kueleweka, ni lazima uwepo utaratibu kuwa Serikali na vyombo vyake vyote vinafanya shughuli zake kwa mujibu wa sheria, na kusimamia utekelezaji wa sheria kwa watu wote na taasisi nyingine zenye mamlaka. Pia Serikali ni lazima iweke utaratibu kwaajili ya kuhakikisha kuwa inakomesha utumiaji wa mabavu kinyume na sheria zinazokubalika. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 79 (iii). Upatikanaji wa Haki: ili uwepo utawala bora ni lazima uwepo utaratibu unaofaa na kuhakikisha kuwa utoaji wa haki unafanywa kwa njia rahisi na zinazohakikisha kuwa haki inatendeka kwenye vyombo vya utoaji haki. (iv). Taratibu za uchaguzi ni shirikishi na za kistaarabu: ziwepo taratibu zinazohakikisha ushirikishwaji wa kweli wa watu katika ngazi zenye mamlaka ya maamuzi kwa kupitia kwa wawakilishi waliowachagua katika uchaguzi huru na wa haki. Taratibu za uchaguzi ni lazima zihakikishe kuwa lengo hilo linapatikana. (v). Iwepo hali ya usalama na amani kwa ajili ya watu na mali zao. (vi). Kuwepo na kuheshimu haki za binadamu bila ya kubaguwana. (vii). Kuwepo na jamii yenye kuelewana, kuvumiliana, kuheshimiana na kushirikiana katika mambo yanayowahusu. (viii). Kuwepo na uwazi katika ngazi zote za kiutawala, kiutendaji, na katika matumizi ya fedha za umma. (ix). Kuwepo na usawa katika hali zote za kijamii, ikiwa ni pamoja na umri na jinsia. (x). Kuwepo na wananchi wanaoelewa utawala wa nchi yao unavyoendeshwa na taarifa nyingine za kijamii kwa kupitia vyombo vya habari vyenye uhuru wa kufanya kazi zao. (xi). Uwepo uwazi katika utoaji wa huduma Serikalini kwa kupitia watu wenye uwezo wa utoaji huo wa huduma na kufanya kazi zao katika misingi inayokubalika. 80 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: (xii). Kuwepo na viwango maalum juu ya mambo yanayokubalika na yasiyokubalika katika jamii, na uwepo utekelezaji wake muafaka. (xiii). Uwepo upendo wa dhati kati ya watu na nchi. Haya ni baadhi ya mambo muhimu ambayo kuwepo kwake yanajenga mazingira mazuri ya kuwepo na utawala bora. Kinyume chake au kukosekana kwake kunasababisha kuwepo na utawala mbaya. Dalili kubwa za utawala mbaya ni hizi zifuatazo: (i). Kuwepo na rushwa katika utumishi wa umma. (ii). Kutokuwepo na usalama wa kuaminika kwa maisha ya watu na mali zao. (iii). Utaratibu wa kufanya uteuzi wa watu wasiostahiki au wasioweza kufanya kazi za umma. (iv). Kutoweka kwa nidhamu inayofaa katika utendaji wa shughuli za umma. (v). Kuvurugika kwa utaratibu mzuri wa matumizi ya fedha na mali nyingine za umma. (vi). Kujenga makundi ya watu wanaokubalika na wasiokubalika na kusababisha chuki miongoni mwa wanajamii. (vii). Kuwa na uchu mkubwa wa madaraka. (viii). Kutothamini haki za binadamu na kuzivunja. (ix) Umasikini uliokithiri. (x). Elimi duni, ujinga uliokithiri na hata kutojua kusoma. (xi). Kutojali na kutoheshimu sheria za nchi. (xii). Kuporomoka kwa maadili. (xiii). Mgawanyiko wa kiuchumi usiolingana. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 81 (xiv). Kutokuwepo na njia wazi za kushauriana. (xv). Kutokuwepo na uhuru wa mahakama. (xvi). Kutokuwepo na uwiyano wa kijinsia. (xvii). Kutoweka kwa mashirikiano ya dhati baina ya baadhi ya watu na vikundi, na (xviii).Uhaba wa huduma muhimu za kijamii. Sehemu ya Pili 3.9.0 Sheria Mbali Mbali 3.9.1 Sheria za Ardhi Zipo Sheria nyingi ambazo zinasimamia masuala tafauti yanayohusiana na ardhi. Sheria hizo ni: Sheria ya Matumizi ya Ardhi, Sheria ya Uhaulishaji wa Ardhi, Sheria ya Uhaulishaji Mali, Sheria ya Usajili wa Ardhi, na Sheria ya Mahakama ya Ardhi. Yafuatayo ni maelezo kwa ufupi kuhusiana na baadhi ya sheria hizo 3.9.1.1 Sheria ya Matumizi ya Ardhi 3.9.1.1.1 Maana ya Ardhi Moja ya mambo muhimu ya kujifunza katika Sheria hii ni maana ya Kwa mtu wa kawaida, ardhi ni hii sehemu ya dunia yenye mkusanyiko wa mchanga au udongo. Lakini katika mtazamo wa kisher kifungu 2 cha sheria ya matumizi ya Ardhi 1992, ardhi inatafrisiwa kujumuisha ardhi yenyewe, pamoja na ile sehemu ya ardhi iliyofunikwa na maji pia na vitu vyote vinavyoota juu ya ardhi, yakiwemo majengo na vitu vyengine vyote vilivyoshikana na ardhi 82 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: isipokuwa miti iliyoainishwa wazi na inayomilikiwa tofauti na ardhi iliyopo. Kwa maana hii ardhi sio tu ule undogo na mchanga uliojikusanya mahali, bali ni pamoja na vitu vyote vilivyoshikamana pamoja na huo undongo na mchanga isipokuwa miti tu ambayo inajulikana wazi kuwa inamilikiwa na mtu tofauti na yule anaemiliki ardhi. 3.9.1.1.2 Umiliki wa Ardhi Kwa mujibu wa Sheria ya matumizi ya Ardhi Namba 12 ya1992, umiliki wa ardhi yote ya Zanzibar ni Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. Haki ambayo raia anaweza kupata ni haki ya kuhodhi na kutumia ardhi( Right of Occupancy). Kwa mujibu wa kifungu 7 cha Sheria ya Matumizi ya ardhi 1992, haki ya matumizi ardhi inaweza kupatikana kupitia moja kati ya njia zifuatazo:(i). Kupewa na Serikali; (ii). Kutambuliwa kwa haki ya matumizi ya ardhi kupitia maamuzi ya Mahakama ya Ardhi; (iii). Kurithi; (iv). Kununua; au (v). Hiba. 3.9.1.1.3 Masharti ya Haki za Kuhodhi na Kutumia Ardhi Yafuatayo ni masharti ya msingi ya kuhodhi na kutumia ardhi chini ya Sheria ya Matumizi ya Ardhi 1992: (i). Mwenye haki ya matumizi ya ardhi ni lazima awe Mzanzibari mwenye umri usiopungua miaka 18 (ii). Ardhi isajiliwe ndani ya miezi 6 tokea mtu anapoipata Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 83 (iii). Mwenye haki ya matumizi ya ardhi anapaswa kuitumia ardhi hiyo kama ilivyokusudiwa na Serikali (iv). Mtu mwenye haki anatakiwa kuitumia au kuiendeleza ardhi aliyopewa ndani ya miaka miwili tokea apewe; (v). Mtumiaji hawezi kupunguza au kuigawa vyengine ardhi aliyopewa; na (vi). Mwenye haki ya matumizi ya ardhi anaweza kuikodisha au kuitoa kwa njia ya hiba ardhi aliyopewa kwa kufuata masharti yaliyowekwa kisheria, pia anaweza kurithiwa. 3.9.1.1.4 Kukatishwa kwa Haki za Matumizi ya Ardhi Tumeona kuwa haki ya kuhodhi na kutumia ardhi ni haki yenye kuendelea kwa mtu anaepewa, na inaweza hata kurithiwa. Hata hivyo mambo yafuatayo yanaweza kusababisha mtu aliepewa haki ya kuhodhi na kutumia ardhi aondolewe au akatishiwe haki hiyo na Serikali. Mambo yenyewe ni haya yafuatayo:(i). Kuondoshewa Haki kwa Maslahi ya Taifa Chini ya kifungu 56 cha Sheria ya Matumizi ya Ardhi 1992, Serikali inaweza kumuondoshea mtu yeyote haki aliyopewa ya kuhodhi na kutumia ardhi ikiwa kufanya hivyo kuna maslahi na Taifa. Kwa mfano endapo ardhi hiyo inahitaji kujengwa njia, hospitali, shule, n.k. Hata hivyo masharti yafuatayo ni lazima yakidhiwe ili haki ya mtu ya kuhodhi na kutumia ardhi iondolewe kwa maslahi ya Taifa. Masharti yenyewe ni: (a). Haja ya kuchukuliwa ardhi kwa maslahi ya taifa lazima ithibitishwe mbele ya Mahakama ya Ardhi(i.e. Land Tribunal), na (b). Mwenye kuondoshewa haki alipwe fidia kwa thamani halisi ya vitu vyake vilivyomo katika ardhi hiyo. 84 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: (ii). Endapo Mwenye Kupewa Haki sio Mzanzibari. Endapo mtu alipewa haki ya kuhodhi na kutumia ardhi sio Mzanzibari, basi Waziri anaehusika anaweza kumuondoshea haki hiyo wakati wowote(Angalia kifungu 57(a) cha Sheria Namba 2 ya 1992). (iii). Endapo Mmilikaji Anajaribu kuhaulisha haki yake kwa asiyekuwa Mzanzibari. Waziri anaehusika pia anaweza wakati wowote kumuondoshea mtu haki ya kuhodhi na kutumia ardhi endapo mtu huyo anajaribu kuhaulisha haki hiyo kwa mtu mwengine ambae sio Mzanzibari(Angalia kifungu 57(b)). (iv). Endapo Mmilikaji ameshindwa kuitumia ardhi. Endapo mtu mwenye haki ya kuhodhi na kutumia sehemu ya ardhi ameshindwa kuitumia ardhi hiyo kwa muda wa miaka miwili tokea apewe, au anaitumia ardhi hiyo kinyume na alivyoruhusiwa, au ameikimbia au kuitelekeza ardhi hiyo kwa kipindi cha miezi 18 au zaidi mfululizo, basi Waziri anaehusika anaweza(kwa kufuata utaratibu maalum) kumuondolea mtu huyo haki ya kuhodhi na kumiliki ardhi. 3.9.2 Sheria za Uhaulishaji Ardhi Zipo sheria mbili zinazozingatia masharti ya msingi uhaulishaji wa haki za ardhi, Sheria hizi ni: (a). Sheria ya Uhaulishaji wa Mali(sura 150); na (b). Sheria ya Uhaulishaji Ardhi(Namba 8) ya 1994. kuhusu 3.9.2.1 Sheria ya Uhaulishaji Mali Sura 150 Hii ni Sheria mama katika Sheria zinazozingatia uhaulishaji wa ardhi( transfer of property) kwa Zanzibar. Sheria hii ndio inaelezea ni haki gani inayohusiana na ardhi inaweza kuhaulishwa, nani Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 85 anaweza kuhaulisha na kuhaulishiwa, haki za muhaulishaji na muhaulishiwaji, na aina za uhaulishaji. 3.9.2.1.1 Kipi Kinahaulishika Kifungu cha 6 cha Sheria ya Uhaulishaji Mali, Sura 150, kinaeleza kuwa mali(au milki) ya aina yoyote inaweza kuhaulishwa isipokuwa tu zile mali ambazo uhaulishawaji wake unazuiliwa ama na Sheria ya Uhaulishaji Mali(Sura 150), au Sheria nyingine yoyote. Kimsingi ni kuwa haki yoyote ambayo mtu anayo(kama miliki) katika mali yoyote, basi haki hiyo inaweza kuhaulishwa, isipokuwa kama tu kuna sheria iliyozuia uhaushaji wa mali hiyo(iwe ni sura 150 yenyewe au sheria nyengine yoyote). Mfano wa mali(au haki) ambazo haziwezi kuhaulishika ni:(a). Uwezekano wa mtu kurithi mali wakati anaetegemewa kurithiwa yupo hai; (b). Haki ya mtu aliekodisha ya kukabidhiwa mali yake kutokana na kuvunjwa masharti ya kodi; (c). Uhuru wa kutumia ardhi ya mtu mwengine kwa ajili ya njia (kupita) au huduma nyingine muhimu, n.k. 3.9.2.1.2 Nani Anaweza Kuhaulisha/ Kuhaulishiwa Tendo la kuhaulisha ni tendo la kimkataba kwa hivyo mtu mwenye uwezo wa kuhaulisha ni yule mtu ambae: (i). Ana uwezo( capacity) ya kuingia katika mkataba; na (ii). Anayo haki(milki) ya kuhaulisha. 86 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Tayari tumezungumza hapa juu ni kitu gani kinahaulishika. Suala la uwezo wa kuingia katika Mkataba ni suala ambalo linazingatiwa katika sheria ya mikataba(Sura 149) sheria za Zanzibar. Kifungu 11 kufanya mkataba endapo ni mtu mzima kwa mujibu wa sheria inayohusika na ana akili timamu, na hajazuiliwa kufanya mikataba na sheria nyingine yoyote. ´ Yaani endapo mtu ana umri wa kuitwa mtu mzima kwa mujibu wa sheria inayotumika ana akili timamu, na hajazuiliwa kuingia katika mikataba kwa mujibu wa sheria nyingine yoyote, basi mtu huyo anao uwezo wa kuingia katika mkataba, ikiwa ni pamoja na mkataba wa kuhaulisha. Na kwa hivyo mtu huyo anaweza kuhaulisha ikiwa hicho cha kuhaulisha anacho. 3.9.2.1.3 Aina za Uhaulishaji Sheria ya Uhaulishaji Mali(sura 150) yanayoelezea uhaulishaji kwa njia zifuatazo: (i). Kuuza( sale); (ii). Kukodisha( lease); (iii). Kuweka dhamana( Mortgager); na (iv). Hiba( Gift). inaweka masharti 3.9.2.1.4 Haki/ Wajibu wa Muhaulishaji/ Muhaulishiwa Sheria ya uhaulishaji Mali(Sura 150) inaweka masharti pia kuhusu haki za muhaulishaji na muhaulishiwa kufuatia tendo la uhaulishaji. Haki hizi na wajibu zinategemea aina yenyewe ya uhaulishaji. Tunaweza kuzizungumza kama haki na wajibu wa muuzaji na mnunuzi, mkodishaji na mkodishwaji mweka dhamana( mortgagor) na muwekewa dhamana( mortgage) na mtoaji hiba na mpokeaji. Maelezo ya haki na wajibu katika haki zote hizo kwa urefu yanaelezewa kwenye makala( document) nyingine. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 87 3.9.2.2 Sheria ya Uhaulishaji Ardhi Namba 8 ya 1994 Sheria hii ni ya karibuni ukilinganisha na sura 150 lengo la sheria hii ni kuweka utaratibu wa kuhaulisha mali isiyoondosheka(ardhi) hapa Zanzibar. Masharti ya msingi ya sheria hii yanahusu uundwaji wa ji Ardhi, na masharti kwamba hakutakuwepo na uhaulishaji wowote wa ardhi(na hasa ardhi ya eka) au ukodishaji wa muda mrefu au mkataba wa ukodishaji wa muda mrefu utakaofanywa ndani ya Zanzibar mpaka iwe uhaulishaji au ukodishaji huo umefanyiwa mapitio na kuidhinishwa na Bodi ya Uhaulishaji Ardhi. Ukodishaji wa muda mrefu, kwa mujibu wa Sheria hii ni ule unafanywa kwa muda wa miaka mitatu au zaidi. Kwa mujibu wa kifungu 5(1) cha Sheria hii, muhaulishaji au mkodishaji mwenyewe anapaswa kuomba idhini au ridhaa ya Bodi juu ya uhaulishaji anaotaka kufanya. Pia kifungu hicho cha 5(1) hadi(3) kimeweka utaratibu maalum wa namna ya kufanya maombi hayo. 3.9.2.2.1 Bodi ya Uhaulishaji Ardhi Kwa mujibu wa kifungu 9(1) cha Sheria ya Uhaulishwaji Ardhi 1994, kutakuwa na Bodi ya Uhaulishaji Ardhi yenye Wajumbe wafuatao: (a). Mwenyekiti ambae atateuliwa na Rais; (b). Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Ardhi na Mazingira ambae atakuwa Katibu wa Bodi; (c). Naibu Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Ardhi na Maingira, ambae atakuwa Katibu wa Kamati Ndogo; (d). Mkurugenzi wa Ardhi; (e). Mrajis wa Ardhi; (f). Mkuu wa Idara ya Ardhi, Pemba; (g). Naibu Mrajis wa Ardhi, Pemba; 88 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: (h). Wajumbe wengine watano, angalau wawili kutoka Pemba, ambao watateuliwa; na Waziri anaehusika na masuala ya ardhi. 3.9.2.2.2 Utaratibu wa Kuomba Ridhaa ya Bodi Utaratibu wa kupeleka maombi ya ridhaa au idhini ya Bodi kuhusu uhaulishaji au ukodishaji wa muda mrefu umewekwa chini ya kifungu 5 cha Sheria hii Namba 8 ya 1994. Utaratibu wenyewe ni kwamba ombi kwanza linapelekwa kwa Mkuu wa Wilaya katika Wilaya ambayo ardhi inayohusika ipo. Mkuu wa Wilaya, baada ya kutoa maoni yake atalipeleka ombi hilo kwa Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Ardhi(Unguja) au Naibu Katibu Mtendaji wa Kamisheni a Ardhi(Pemba), Katibu Mtendaji wa Kamisheni ya Ardhi(Unguja) au Naibu wake(Pemba), kadiri ya mahali ambapo ardhi hiyo ipo kati ya Unguja au Pamba atalipeleka ombi hilo kwenye Bodi kwa ajili ya kufanyiwa maamuzi. 3.9.2.2.3 Masharti ya Ombi Ombi la idhini au ridhaa ya kuhaulisha au kukodisha ardhi lazima lionyeshe taarifa zifuatazo:(a). Jina la Muhaulishaji /Mkodishaji, (b). Jina la Muhaulishiwaji/ Mkodishwaji, (c). Utambulisho wa Muhaulisha na Muhaulishwaji au wa Mkodishaji na Mkodishwaji, (d). Mahali ambapo ardhi yenyewe ipo(pamoja na nambari zake za utambulisho), (e). Sababu za kuhaulisha au kukodisha, (f). Masharti ya Uhaulishaji au Ukodishaji, (g). Uraia wa Muhaulishiwaji au Mkodishwaji, Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 89 (h). Bei au thamani kwa ajili ya uhaulishaji au kodi, (i). Tarehe ya kuzaliwa Muhaulishaji au Muhaulishiwaji au Mkodishaji au Mkodishwaji, na (j). Taarifa nyingine yoyote inayofaa. 3.9.2.2.4 Sababu za Kutotoa Idhini/ Ridhaa ya Kuhaulisha Endapo imeombwa idhini au ridhaa ya mtu kuhaulisha ardhi, Bodi inaweza isitoe ridhaa hiyo katika hali zifuatazo:(a). Endapo Bodi itaridhika kuwa uhaulishaji huo unaweza kusababisha kumnyima ardhi Mhaulishaji kwa ajili ya matumizi ya lazima yake mwenyewe na warithi wake, (b). Endapo Bodi itaridhika kuwa uhaulishaji huo hauna maslahi kwa Muhaulishaji, (c). Endapo Bodi itaona kuwa uhaulishaji huo una athari ya dhamana, (d). Endapo Bodi itaona kuwa Mhaulishiwaji ana lengo la kuitumia vibaya ardhi inayohaulishwa, (e). Endapo Bodi imeridhika kuwa uhaulishaji utaleta matokeo au haki ambayo haiwezi kuandikishwa kwa mujibu wa sheria kusajili ardhi, au (f). Endapo Bodi ina amini kuwa uhaulishaji huo haukubaliki. 3.9.3 Sheria ya Usajili wa Ardhi Usajili wa ardhi unasimamiwa na Sheria ya Usajili wa Ardhi (Namba 10) ya 1990. Chini ya kifungu 5 cha sheria ya Usajili wa Ardhi, Waziri anayehusika na maswali ya ardhi anaweza kuanzisha mamlaka ya Usajili wa ardhi( Land Registration District) kwa ajili ya eneo lolote ambalo atalitangaza kwenye gazeti rasmi. Katika kila Mamlaka ya Usajili wa Ardhi ambayo Waziri ataianzisha, shughuli 90 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: za usajili wa ardhi ndio zitafanyika. Usajili wenyewe utafanywa kwa kuweka mambo yafuatayo:(a). Regista la Ardhi(kwa mujibu wa sheria hii) (b). Regista la Ramani, (c). Majarida( files) yenye kuweka kumbukumbu zinazohusiana na ardhi iliyoandikishwa, (d). Daftari lenye arodha ya maombi ya usajili kama yanavyopokelewa, (e). Index ya wamiliki ardhi, kodi au dhamana( mortgage) inayoonyesha idadi ya vikataa vya ardhi ambavyo mtu anavyo, (f). Orodha ya ramani za ardhi zilizobadilishwa kwa amri ya Msajili wa Ardhi na kwa ridhaa ya watu walio athirika na ubadilishaji huo, na (g). Regista la watu waliotumika uwakala katika hatua za uhaulishaji. Usajili utafanywa katika hatua mbili. Katika hatua ya kwanza ya usajili, kwa kila sehemu ya ardhi inayosajiliwa, patatayarishwa regista kwa mujibu wa kifungu cha 12(2). Katika regista hilo yatakuwemo maelezo juu ya umiliki wa ardhi inayoandikishwa, vikwazo ambavyo vipo dhidi ya mmiliki wa ardhi hiyo(mfano kama ardhi nidhamana kwa ajili ya mkopo). Mrajis wa Ardhi atasaini kuhakikisha ithibati ya kumbukumbu hizo. Usajili katika hatua nyingine zozote utafanywa kwa kuingiza taarifa mpya ndani ya regista liliopo la ardhi(Angalia kifungu 14(1) na(2) Chini ya kifungu 15 Mrajis anaweza kufuta ili kutoka kwenye regista kumbukumbu zozote ambazo hazina kazi tena kimsingi. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 91 3.9.3.1 Umuhimu wa Kusajili Ardhi Kwa mujibu wa kifungu 8(2) cha Sheria ya Matumizi ya Ardhi (Namba 12) ya 1992, haki yoyote ambayo mtu amepata kuhusiana na ardhi hapa Zanzibar haitakuwa na nguvu za kisheria mpaka haki hiyo iwe imesajiliwa kwa mujibu wa sheria ya Usajili wa Ardhi. Nacho kifungu 27(a) cha Sheria ya Usajili wa Ardhi(Namba 10) ya 1990 kinaeleza kuwa mtu ambae umiliki wake wa ardhi umesajiliwa rasmi atakuwa na haki zote za kuitumia ardhi hiyo dhidi ya watu wengine wote isipokuwa Serikali tu. 92 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: SURA YA NNE Sehemu ya Kwanza 4.0 Sheria Mbali Mbali 4.1 Sheria ya Mzanzibari Sheria ya Mzanzibari Namba 5 ya 1985 imepitishwa kwa madhumuni ya kuweka wazi nani Mzanzibari ili aweze kupata haki zake zote kama Mzanzibari. Sheria hii ilianza kutumika tarehe 12 Januari 1985. 4.1.1 Nani Mzanzibari? Uzanzibari si uraia bali ni utambulisho wa kuwa mtu fulani ni mzanzibari, uraia ni wa Tanzania. Hivyo, ili mtu yeyote awe Mzanzibari kwanza ni lazima awe Mtanzania, na atakapoupoteza uraia wa Tanzania basi pia atasita kuwa Mzanzibari. Zipo aina nne za kumtambua nani Mzanzibari, aina hizo ni: (a). Ni mtu yeyote ambaye ni raia wa Tanzania ambaye amekuwa akiishi Zanzibar kabla na hadi tarehe 12 Januari 1964; (b). Ni mtu yeyote ambaye kuanzia tarehe 26 Aprili 1964 ni raia wa Tanzania na amezaliwa Zanzibar na wazazi wake wote au baba yake au mama yake ni Mzanzibari; (c). Ni mtu yeyote ambaye ni raia wa Tanzania na kabla ya tarehe 26 Aprili 1964 alikuwa Mzanzibari; (d). Ni mtu yeyote ambaye ni raia wa Tanzania na wazazi wake wote au baba au mama ni Mzanzibari. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 93 4.1.2 Uzanzibari wa Kuomba Mtu yeyote ambaye ni raia wa Tanzania na ana sifa zifuatazo anaweza kuomba Uzanzibari. Sifa hizo ni: (a). Awe ameishi Zanzibar kwa kipindi cha miaka 10 mfululizo; (b). Ana elimu ya kutosha ya kuandika na kusoma kiswahili; (c). Ana tabia nzuri; (d). Ameingia Zanzibar kihalali na anatii Sheria zilizopo Zanzibar na kanuni zake; (e). Ni mtu mzima, na (f). Ana nia ya kuendelea kuishi Zanzibar. Ingawa hapa imeelezwa kwamba mtu mwenye sifa zilizotajwa hapo juu anaweza kuomba kuwa Mzanzibari, lakini hadi leo haujawekwa utaratibu wa jinsi gani maombi hayo yafanywe katika ofisi gani na kwa namna gani. Lakini mtu aliyepata Uzanzibari kwa kuomba atasita kuwa Mzanzibari ikiwa atapoteza uraia wa Tanzania au ikiwa mujibu wa taratibu zitakazowekwa. Kila Mzanzibari mwenye umri wa miaka 18 na zaidi ana haki ya kujiandikisha na kupewa kitambulisho cha Uzanzibari kitakachotolewa na Mkurugenzi wa Vitambulisho vya Wazanzibari Wakaazi. 4.2 Sheria ya Usajili wa Wazanzibari Wakaazi Sheria ya Usajili wa Wazanzibari Wakaazi Namba 7 ya 2005, imeanzisha afisi ya Uandikishaji wa vitambulisho vya Wazanzibari wakaazi ambayo inaoongozwa na Mkurugenzi aliyeteuliwa na Rais. Ili mtu aweze kuandikishwa na kupewa kitambulisho ni lazima awe 94 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mzanzibari ambaye anaishi kwa kudumu Zanzibar na ambaye ana umri wa miaka 18 na zaidi. Uandikishaji huu ni lazima kwa Wazanzibari na Mkurugenzi atakapotoa tangazo la uandikishaji Wazanzibari watapaswa kufuata maelekezo yake na kufika sehemu waliyopangiwa kwa uandikishaji. Kwa wale Wazanzibari waliopo nje ya nchi Sheria hii ilipoanza kutumika au waliokuwa hawajatimia umri wa miaka 18 watapaswa kufika ofisi ya usajili kwa madhumuni ya kujiandikisha ndani ya mwezi mmoja baada ya kurudi Zanzibar au kutimia umri wa miaka 18. Baada ya kuandikisha, walioandikisha watapewa vitambulisho baada ya kulipa ada iliyowekwa. Watu hao watatakiwa wavitunze vizuri vitambulisho hivyo na endapo kitambulisho kitapotea mtu aliyepoteza atatakiwa apeleke mara moja taarifa ya kupotea kwa Sheha wa Shehia yake na baadae kituo cha polisi kilicho karibu naye. Baada ya uchunguzi kufanywa afisa uandikishaji atampa kitambulisho chengine. Mzanzibari yeyote anaweza akatakiwa akionyeshe kitambulisho hicho kwa Mamlaka yoyote wakati akitaka kujiandikisha kupiga kura, kuomba leseni, ruhusa au hati yoyote, na akishindwa kuonyesha kitambulisho hicho Mamlaka husika inaweza ikaacha kushughulikia maombi yake. Vile vile Mkurugenzi wa Vitambulisho, Afisa yeyote wa polisi au uhamiaji wanaweza wakati wowote kumtaka mtu aonyeshe kitambulisho cha Uzanzibari. Mkurugenzi chini ya Sheria hii ana uwezo wa kukataa kutoa kitambulisho au anaweza kukifuta kitambulisho kilichotolewa kwa mtu yeyote ikiwa mtu huyo si mkaazi wa kudumu wa Zanzibar. Ikiwa mtu huyo hatoridhika na uamuzi wa Afisa uandikishaji anaweza kukata rufaa kwa Mkurugenzi, na ikiwa hakuridhika na uamuzi wa Mkurugenzi anaweza kukata rufaa kwa Waziri anayeshughulikia Tawala za Mikoa ambaye uamuzi wake ni wa mwisho. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 95 Sheria hii pia imeweka wazi kuwa ni makosa kwa mtu yeyote: (a). kushindwa kujiandikisha; (b). kutoa maelezo ya uongo; (c). (d). kuandika, kubadilisha au kufuta kwenye kitambulisho kitu chochote; (e). kutoa maelezo ya uongo kuwa hajajiandikisha kwa nia ya kumdanganya muandikishaji, au (f). kujaribu kupata kitambulisho cha pili. Mtu yeyote atakayepatikana na makosa haya atatozwa faini isiyopungua shilingi laki moja au kifungo kisichozidi mwaka mmoja au vyote viwili. 4.3 Sheria ya Uchaguzi Shughuli za uchaguzi Zanzibar zinaongozwa na Sheria ya uchaguzi Namba 11 ya1984. Sheria hii imeshafanyiwa marekebisho mara 7 hadi hivi sasa ili kuweza kukidhi mahitaji ya mabadiliko yaliyotokea ya kisiasa, kiuchumi na kijamii. Msimamizi wa Sheria hii ni Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar, ambayo ndio inayoratibu mchakato mzima wa uchaguzi. Utaratibu wa uchaguzi unajumuisha hatua kuu 8 ambazo ni: kugawa majimbo ya uchaguzi, uandikishaji wapiga kura, uteuzi wa wagombea, kampeni za uchaguzi, upigaji kura, kuhesabu kura, kujumlisha kura na kutangaza matokeo. 4.3.1 Mgawanyo wa Majimbo Hili ni jambo muhimu kwani linaiwezesha Tume ya uchaguzi na Wadau wengine kufahamu pahali ambapo wapiga kura watajiandikisha na kupiga kura na pia kugombea uwakilishi, ubunge 96 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: na udiwani. Kwa hivi sasa Zanzibar ina majimbo 50; 32 yapo Unguja na 18 yapo Pemba. 4.3.2 Uandikishaji Wapiga Kura Kujiandikisha kupiga kura ni haki ya Kikatiba ya kila raia. Ili mtu awe mpiga kura anatakiwa awe na sifa zifuatazo: (a). awe ni Mzanzibari mwenye umri usiopungua miaka 18; (b). awe na akili timamu; (c). asiwe na utii kwa nchi nyengine yeyote mbali na Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; (d). awe hajazuiwa kujiandikisha kuwa mpiga kura kutokana na makosa ya rushwa katika uchaguzi; (e). asiwe anatumikia kifungo cha zaidi ya miezi 6; (f). awe ni mkaazi wa kawaida wa jimbo au shehia anayojiandikisha. Ili kuondoa usumbufu wa wananchi kujiandikisha kila uchaguzi unapokaribia Tume ya Uchaguzi imeanzisha Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ambalo limeanza kutumika katika uchaguzi wa 2005. Tume italiendeleza na kulitunza daftari hilo kwa ajili ya chaguzi nyingine zinazofuata. 4.3.3 Uteuzi wa Wagombea Urais, Uwakilishi, na Udiwani Uteuzi wa wagombea ni hatua muhimu katika uchaguzi. Tume ya uchaguzi ndio inayopanga siku ya uteuzi na yenye mamlaka ya kuthibitisha uteuzi wa wagombea wa urais, na kwa upande wa wagombea wa uwakilishi, na udiwani Wasimamizi wa Uchaguzi ndio wanaothibitisha uteuzi. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 97 Ili mtu aweze kugombea urais anatakiwa awe na sifa zifuatazo: (a). awe Mzanzibari wa kuzaliwa; (b). awe na umri usiopunguwa miaka 40; (c). anazo sifa za kumuwezesha kuchaguliwa kuwa mjumbe wa Baraza la Wawakilishi, na ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa kilichosajiliwa rasmi kwa mujibu wa Sheria ya vyama vya Siasa ya 1992. Kwa yule anayetaka kugombea uwakilishi, anatakiwa awe na sifa zifuatazo: (a). awe ni Mzanzibari aliyetimia umri wa miaka 21; (b). awe amejiandikisha au ana sifa za kujiandikisha katika jimbo la uchaguzi kama mpiga kura katika uchaguzi wa wawakilishi; (c). awe anaweza kusoma na isipokuwa kama hana uwezo wa kuona au magonjwa mengine ya kiwiliwili, anasema lugha ya Kiswahili; (d). awe ni mwanachama wa Chama cha siasa kilichosajiliwa na ni mgombea na aliyependekezwa na chama cha siasa kilichosajiliwa rasmi kwa mujibu wa Sheria ya vyama vya Siasa ya 1992. (e). Awe ni mtu ambaye hakuzuiliwa kugombea uchaguzi kwa mujibu wa Sheria. Mtu hatofaa kuchaguliwa kuwa mjumbe wa Baraza la Wawakilishi ikiwa: (a). ana uraia wa nchi nyingine; (b). amethibitishwa kwa mujibu wa Sheria kuwa ni mgonjwa wa akili; (c). si mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama, au 98 Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: (d). ametumikia kifungo cha zaidi ya miezi 6 kwa kosa la jinai au kosa la uchaguzi linalohusu uaminifu ndani ya miaka mitano kabla ya uchaguzi; Kwa yule anayetaka kugombea udiwani, anatakiwa awe na sifa zifuatazo: (a). awe ni Mzanzibar aliyetimia umri wa miaka 21; (b). awe amejiandikisha au ana sifa za kujiandikisha katika jimbo la uchaguzi kama mpiga kura na hakuzuiliwa kugombea uchaguzi kwa mujibu wa Sheria. (c). awe ni mkaazi wa kawaida wa eneo linalohusika; (d). awe anaweza kusoma na kuandika kiswahili na kiingereza; (e). awe ni mwanachama na mgombea aliyependekezwa na chama cha siasa kilichosajiliwa rasmi kwa mujibu wa Sheria ya vyama vya Siasa ya 1992; na (f). Awe anajishughulisha na kazi halali. Mtu hatofaa kuchaguliwa kuwa diwani ikiwa: (a). ana uraia wa nchi nyingine; (b). amewekwa kizuizini kwa mujibu wa Sheria ya jinai kwa muda unaozidi miezi 6; (c). amesafirishwa kwa lazima kisheria na iwapo amekaa huko kwa zaidi ya miezi 6; (d). amethibitishwa kwa mujibu wa Sheria kuwa ni mgonjwa wa akili; (e). ikiwa mtu huyo ana maslahi yeyote katika mkataba wa Serikali wa aina yoyote uliyowekwa miiko maalum kwa mujibu wa Sheria na iwapo amekiuka miiko hiyo; (f). iwapo amezuiliwa kuwa diwani kwa mujibu wa Sheria. Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: 99 (g). ikiwa mtu huyo amezuilika kupiga kura kutokana na makosa ya uchaguzi. 4.3.4 Kampeni za Uchaguzi Kampeni ni kipindi kinachotumiwa na wagombea wa vyama vya siasa kujinadi na kujilabu na kutangaza sera katika mikutano ya hadhara ya kampeni za uchaguzi. Kipindi chote baada ya uteuzi wa wagombea hadi siku moja kabla ya upigaji kura ni kipindi cha kampeni. Yapo mambo muhimu yanayopaswa kuandaliwa kwa ajili ya kampeni. Tume ya uchaguzi inatakiwa iandae ratiba ya kampeni ili kuondoa na kuepusha migongano ya vyama katika eneo moja. Sheria imeweka kuwa ni kosa kufanya kampeni katika sehemu za ibada na taasisi za taaluma. Katika uchaguzi hasa wakati wa kampeni hutokea migogoro mingi kutoka pande zenye itikadi tofauti ya kisiasa. Hivyo Tume inatakiwa iandae maadili ya uchaguzi ili kuepusha au kupunguza migogoro hiyo. Ili kampeni ziende vizuri ni lazima uwanja wa kampeni uwe sawa kwa vyama vyote. Hivyo, ni makosa kwa chama kimoja kutumia fursa ilizonazo kwa faida ya kuendeleza kampeni zake, kwa mfano kutumia gari za Serikali, vyombo vya habari kuzipa uzito habari za chama fulani, vyombo vya dola kupendelea chama fulani n.k. 4.3.5 Upigaji Kura Tume ya uchaguzi ndiyo yenye mamlaka ya kupanga siku ya kupiga kura ambayo inatakiwa iwe si chini ya siku 60 na si zaidi ya siku 90 tokea wagombea walipoteuliwa. Upigaji kura hufanyika katika vituo vya kupigia kura vilivyopangwa na Tume. Katika kila kituo hutengenezwa eneo la faragha ambalo mpiga kura hutumia kupiga kura yake kwa siri bila ya kuonekana na wengine. Tume pia inawajibu wa kutangaza muda wa kuanza na kumaliza kupiga kura. 100 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Watu wafuatao wanaruhusiwa kuwepo katika kituo cha kupiga kura: (a). msimamizi wa kituo au msaidizi msimamizi wa kituo; (b). mwenye kuhesabu; (c). wakala wa upigaji kura; (d). mtu anayemsaidia mpiga kura mwenye ulemavu; (e). askari polisi na askari wa aina nyengine ikibidi kwa ajili ya kuweka usalama katika kituo cha upigaji kura; (f). mgombea; (g). msimamizi wa uchaguzi au msaidizi wa uchaguzi; (h). mjumbe wa Tume au Afisa uchaguzi; (i). waangalizi walioruhusiwa kwa maandishi na Tume. 4.3.6 Kuhesabu Kura Baada ya zoezi la kupiga kura kukamilika, kura huhesabiwa hapo hapo kituoni. Isipokuwa kutokana na sababu za kiusalama, msimamizi wa kituo baada ya kushauriana na mawakala anaweza kuhamisha shughuli za kuhesabu kura pahala pengine ndani ya jimbo husika. 4.3.7 Kujumlisha Kura Tume ya Uchaguzi itajumlisha kura zote za Rais wa Zanzibar baada ya kupokea kutoka katika majimbo yote ya uchaguzi. Wasimamizi wa uchaguzi kwa mujibu wa Sheria watajumlisha kura za wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani. Vyama vya siasa vinatakiwa vifahamishwe na mapema kuhusu tarehe, pahala na saa ya kuanza kujumlisha kura ili waweze kushuhudia kazi hiyo. 4.3.8 Kutangaza Matokeo Matokeo ya uchaguzi kwa kila uchaguzi yatatangazwa na kubandikwa pahala ambapo ujumlishaji utafanyika. Baada ya kura zote zilizopigwa katika jimbo kuhesabiwa, msimamizi atawasilisha Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 101 kwa Tume na kwa Mgombea au wakala wa mgombea akieleza: jumla ya kura zote zilizopigwa katika uchaguzi wa Rais, jumla ya kura zilizopigwa katika uchaguzi wa wawakilishi na udiwani, idadi ya kura alizopata kila mgombea, kama ni mgombea pekee kura alizopata mgombea huyo. Baadaye Tume itajumlisha jumla ya kura zote za kila mgombea urais zilizothibitishwa kutoka katika majimbo yote ya uchaguzi. Mgombea urais atatangazwa kuwa mshindi ikiwa atapata kura nyingi zaidi halali zilizopigwa kuliko wagombea wenzake. Na iwapo wagombea wawili waliopata kura nyingi watapata kura sawa basi uchaguzi utarudiwa tena. Sheria inaeleza kwamba ni makosa kwa mtu yeyote kutangaza matokeo kabla ya kutangazwa na Tume ya Uchaguzi na adhabu yake ni faini ya shilingi milioni tano au kifungo kisichopunguwa miaka mitano au vyote viwili. Sehemu ya Pili 4.4.0 Sheria za Idara Maalum za SMZ Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kutumia uwezo aliopewa na Katiba ya Zanzibar ya mwaka 1984 ameanzisha Idara maalum za Serikali za Mapinduzi ya Zanzibar (SMZ) zikiwa na malengo mbali mbali. Idara hizo ni Kikosi cha Valantia kilichoanzishwa kwa Sheria Namba 5 ya 2004, Kikosi Maalum cha Kuzuia Magendo kilichoanzishwa kwa Sheria Namba 1 ya 2003, Jeshi la Kujenga Uchumi lililoanzishwa kwa Sheria Namba 6 ya 2003, Kikosi cha Zimamoto kilichoanzishwa kwa Sheria Namba 7 ya 1999, na Chuo cha Mafunzo kilichoanzishwa na Sheria Namba 1 ya 1980. 102 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 4.4.1 Kikosi cha Valantia Sheria Namba 5 ya 2004 imeanzisha Kikosi cha Valantia(KVZ) ambacho ni sehemu ya Idara Maalum za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar. KVZ kwa mujibu wa Sheria ina majukumu yafuatayo: (a). kushirikiana na vikosi vya ulinzi na usalama vya Tanzania; (b). kupigana na janga lolote litakaloikumba jamii; (c). kulinda mali za Serikali; (d). kufanya kazi za kijeshi kwa madhumuni ya kuzuia hali inayohatarisha ulinzi na usalama; (e). kuweka amani na usalama ndani ya nchi; (f). kufanya kazi yoyote watakayopewa na Rais au Waziri anayehusika na Valantia. KVZ ina watumishi wa aina mbili: wale walioajiriwa na wale wanaojitolea. Watumishi walioajiriwa wanaweza kuajiriwa wakiwa na umri baina ya miaka 18 na 35, na wanaweza kuwa na cheo chochote kwa mujibu wa kanuni za Valantia au wanaweza kuwa watumishi wa Serikali ambao wanaongozwa na Kanuni za utumishi Serikalini. Wale watumishi wanaojitolea ni Wazanzibari ambao wamejiandikisha kufanya kazi ya kujitolea katika Valantia. 4.4.1.1 Uwezo na Haki za Valantia Katika kutekeleza majukumu yao Valantia wana uwezo wa kumkamata mtu na kumpekua kwa mujibu wa Sheria ikiwa wanasababu za kuamini kuwa mtu huyo amevunja Sheria yoyote. Pia Valantia wana haki ya kupata mafunzo ya ulinzi na usalama katika Taasisi yoyote Zanzibar, Tanzania au nje ya Tanzania. Vile vile Valantia wana haki ya kutumia silaha ndogo ndogo ikiwa ni lazima kufanya hivyo. Valantia wanaweza kuamrishwa na Rais wa Zanzibar wafanye kazi pamoja na Jeshi la Wananchi wa Tanzania au Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 103 Polisi, au Idara maalum za SMZ, na wanapofanya kazi hizo watapokea amri kutoka kwa jeshi, polisi au Idara maalum. Valantia pia wana haki ya kupandishwa cheo na haki ya kulipwa mshahara kwa mujibu wa taratibu zilizowekwa na Tume ya Utumishi ya Idara Maalum. Pale Valantia wanapofanya makosa watapewa adhabu kwa mujibu wa kanuni. Wanaweza kupewa adhabu ya karipio, karipio kali, adhabu ndogo, faini isiyozidi nusu ya mshahara, kushushwa cheo, kifungo kisichozidi siku 14 au kuachishwa kazi. Sheria imeweka wazi kwamba Valantia anaweza kuachishwa kazi ikiwa atagoma au atatumia nguvu kwa afisa yoyote, atatumia lugha ya kudhalilisha kwa afisa huyo, atakataa amri halali, ataiba au kushiriki katika wizi au kuondoka kazini bila ya ruhusa kwa siku zaidi ya 21. Sheria pia imeanzisha Mahakama ya Valantia kwa ajili ya kusikiliza kesi zinazotokea katika kikosi hichi. Kwa upande mwengine Sheria imekataza Valantia yoyote kushiriki katika shughuli za kisiasa na yeyote atakayepatikana na kosa hili ataachishwa kazi. 4.4.2 Kikosi cha Kuzuia Magendo Kikosi hiki cha kuzuia magendo kimeanzishwa kikiwa na lengo kuu la kuzuia magendo na hivyo kimepewa uwezo wa kutumia silaha mbali mbali katika kutekeleza majukumu yao. Kazi zao mara nyingi zinafanyika katika eneo la baharini. Mbali ya jukumu la kuzuia magendo KMKM imepewa majukumu mengine kama yafuatayo: (a). kuhakikisha usalama upo katika bahari ya Zanzibar; (b). kulinda mali asili za baharini; (c). kulinda na kukinga usalama wa nchi kutokana na majasusi na watu wenye nia mbaya wanaokuja kwa kupitia baharini; 104 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria (d). kulinda misafara ya vyombo vya Serikali wakati wa vita au hali ya hatari; (e). kusafirisha vikosi vyengine; (f). kushirikiana na Jeshi la Wananchi wa Tanzania; (g). kushughulikia uhalifu unaofanywa baharini ikiwa ni pamoja na usafirishaji wa madawa ya kulevya na uharamia; (h). kutafuta na kufanya uokozi baharini na kulinda mazingira ya baharini; (i). kuisaidia Serikali wakati wa hali ya hatari. Katika kutekeleza majukumu yao afisa wa KMKM wana uwezo wa kufanya upekuzi, kuzuia na kukamata chombo cha baharini, chombo kilichomo ndani ya chombo hicho au chombo kilichopo gatini au chombo wanachokishutumu kuhusika na magendo na usafirishaji wa mazao ya biashara. Baada ya kufanya upekuzi au kukamata mali, mazao au watu wanaohusika KMKM wanatakiwa waipeleke mali hiyo au watu kwa mamlaka nyengine inayohusika ili hatua za kisheria zichukuliwe. Afisa wa KMKM amepewa kinga ya kutoshitakiwa kwa kutekeleza majukumu yake ikiwa ametekeleza hayo baada ya kupewa amri halali na ametumia nguvu inayowiana na tukio lenyewe. KMKM inaongozwa na Mkuu wa KMKM ambaye ameteuliwa na Rais, lakini Waziri anayehusika na Idara Maalum anao uwezo wa kutoa maelekezo kwa KMKM. Mtu yeyote anaweza kujiunga na KMKM kama ilivyowekwa na kanuni ambazo zimekubaliwa na Tume ya Utumishi ya Idara Maalum. Kila mtu aliyeajiriwa na KMKM atapaswa kula kiapo cha utii, na atapewa mafunzo ya baharini na ya kwenye vyombo. Upandishwaji wa vyeo unafanywa na Rais baada ya kupokea mapendekezo kutoka kwa Tume. Ushushaji wa vyeo pia unafanywa kwa kufuata taratibu za kijeshi na mpaka Rais akubali ushushwaji huo. Ikiwa afisa yoyote wa KMKM Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 105 amefanyiwa uonevu au hakutendewa haki anaweza kuyapeleka malalamiko yake kwa Mkuu wa KMKM kwa kufuata utaratibu uliowekwa. Sheria pia imeanzisha Mahakama ya KMKM ambayo inasikiliza kesi za maafisa wa KMKM na Mahakama za kawaida hazina uwezo wa kusikiliza kesi hizo. Pia yamewekwa makosa kadhaa na adhabu zake; yapo makosa ya kiutendaji wa kazi za kila siku, kutotii amri halali zilizotolewa na maafisa wa KMKM, kufanya uasi, kukimbia kazini, kuondoka bila ya ruhusa n.k. Pale afisa wa KMKM anapofanya lolote kati ya makosa hayo anaweza kupewa moja wapo ya adhabu zifuatazo: kifungo, kuachishwa kazi, kuwekwa ndani, kushushwa cheo, kutozwa faini, kupewa karipio, pamoja na adhabu nyengine ndogo ndogo. Rais ana uwezo wa kuwapa amri KMKM wajiunge na Jeshi la Wananchi wa Tanzania wakati wa vita, machafuko au hali ya hatari, na KMKM watakapojiunga na Jeshi watafuata Sheria inayowaongoza majeshi. Pia Rais anaweza kuwatumia KMKM nje ya Zanzibar. 4.4.3 Jeshi la Kujenga Uchumi Jeshi la Kujenga Uchumi(JKU) lilianzishwa mwaka 1979 likiwa na lengo la kutoa mafunzo kwa vijana wa Kizanzibari ili waitumikie vyema nchi yao na pia waajiriwe na JKU. Mafunzo wanayopewa vijana hao ni: (a). misingi ya uchumi na jinsi ya kuitumia katika kilimo, viwanda vidogo vidogo, uvuvi na mafunzo mengine ya amali; (b). elimu ya uraia; (c). shughuli za kijamii na kiutamaduni; na (d). ulinzi wa nchi. 106 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Vijana wanaoajiriwa na JKU wana majukumu mbalimbali, miongoni mwao ni: (a). kushirikiana na Jeshi la Wananchi wa Tanzania katika ulinzi na kuweka amani nchini; (b). kutoa huduma za ulinzi kwa Taasisi za umma, au za binafsi ambazo ni muhimu kiuchumi, au kiusalama; (c). kujiunga na vikosi vyengine ya ulinzi na usalama. Katika kutekeleza majukumu yao JKU wana uwezo na haki ya kutumia silaha. JKU inaongozwa na Mkuu wa JKU ambaye anateuliwa na Rais. Wafanyakazi wengine wa JKU ni wale walioajiriwa kwa masharti ya kudumu, watu wanaojitolea, na wale wanaohamishiwa JKU kutoka sehemu nyengine. JKU imegawika katika idara na vitengo mbali mbali, hivyo mtu yeyote anayejiunga anaweza kupelekwa katika kitengo chochote kulingana na uwezo wake. Pia anatakiwa awe tayari kufanya kazi popote ndani au nje ya Zanzibar. Watu wanaojiunga na JKU wanalipwa mishahara na marupurupu kwa kiwango na kwa masharti yaliyowekwa na Tume ya Utumishi ya Idara Maalum na Kanuni za JKU. Kwa upande wa nidhamu na adhabu zinazoweza kutolewa ni kama ilivyo katika Idara mbili zilizotangulia. Sheria pia imeanzisha Mahakama ya JKU na zipo Mahakama ya Jumla, Mahakama ya Maofisa Waongozaji, na Mahakama ya Nidhamu. Makosa yote yanayosikilizwa na Mahakama hizi yawe yametendeka si zaidi ya mwaka mmoja uliopita. Lakini Mahakama za kawaida hazina uwezo wa kusikiliza kesi za makosa ya JKU. Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 107 4.4.4 Kikosi cha Zimamoto na Uokozi Kikosi cha Zimamoto na Uokozi kama zilivyo Idara Maalum zilizotangulia imeundwa ikiwa na jukumu kuu la kuzima moto na kufanya uokozi unaotokana na moto; ukiwa wa mali au maisha. Majukumu mengine waliyonayo ni: (a). utayarishaji wa sera ya usalama wa moto; (b). kuishauri Serikali katika utekelezaji wa sera hiyo; (c). kujishughulisha na uwekaji wa viwango vya kimataifa katika kudhibiti moto katika viwanja vya ndenge; (d). kufanya uchunguzi kutafuta vyanzo vya ajali za moto; (e). kutoa mafunzo ya uzimaji moto na uokozi. Kikosi hiki kinaongozwa na Kamishna anayeteuliwa na Rais na chini yake wapo maafisa wa Zimamoto, askari wa kawaida. Wafanyakazi wa Idara hii wanajukumu la kufanya kazi popote kwenye visiwa vya Unguja na Pemba, au nchi za jirani kutoa msaada wa kibinadamu kama ambavyo Waziri anayeshughulikia Idara hii atakavyoamrisha. Katika utekelezaji wa majukumu yao wafanyakazi wa Idara hii wanaweza baada ya kuruhusiwa kwa maandishi na Kamishna kuingia katika jengo lolote ili kuhakikisha masharti ya Sheria hii yanafuatwa, kupata maelezo kuhusiana na uzimaji moto kama muundo wa jengo, upatikanaji wa maji n.k., kuangalia kama ipo hatari yoyote ya moto. Ruhusa hii ya kuingia kwenye majengo ni kwa yale majengo yanayotumika kwa mkusanyiko wa umma, burudani, viwanda, karakana au sehemu za kazi au biashara. Katika majengo mengine kabla ya kuingia wanatakiwa watoe notisi ya maandishi ya masaa 24 kwa mkazi wa jengo hilo. 108 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Wafanyakazi wa Idara hii kama walivyo wa Idara nyengine wanapaswa kutii Sheria na kutii amri zote halali wanazopewa, na yeyote asiyetii Sheria au amri anazopewa atachukuliwa hatua za kinidhamu kwa mujibu wa Kanuni za Zimamoto au kuachishwa kazi. 4.4.5 Chuo Cha Mafunzo Chuo cha Mafunzo Zanzibar kimeanzishwa kwa malengo makuu mawili; kwanza; kuwashughulikia watu wote wanaofanya makosa ya jinai kwa kuwarekebisha tabia zao ili baadae waweze kuwa raia wema wa nchi yao, na pili ni kutoa mafunzo ya amali katika nyanja zifuatazo: (a). kilimo na mifugo; (b). uchongaji; (c). ujenzi wa nyumba na uashi; (d). ufundi wa mashine; (e). ushonaji wa nguo; na (f). utengenezaji wa viatu. Chuo cha Mafunzo kinaongozwa na Kamishna na Naibu Kamishna ambao wanateuliwa na Rais, na kila kituo cha chuo cha mafunzo kinaongozwa na afisa mdhamini anayeteuliwa na Kamishna. Kama zilivyo Idara nyengine Maalum, pia chuo cha mafunzo kina utaratibu wake wa kinidhamu na makosa ya kinidhamu pamoja na adhabu zinazoweza kutolewa kwa maafisa wanaofanya makosa. Utaratibu wake kwa kiasi kikubwa unafanana na ule wa Idara Maalum tulizozitaja hapo juu. Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 109 4.4.5.1 Masuala ya Afya Katika kila kituo cha chuo cha mafunzo anatakiwa awepo daktari au afisa wa tiba atakayeteuliwa na Mkurugenzi wa Tiba, na afisa huyu atakuwa na jukumu la kuwaangalia wanafunzi wote, na kuangalia hali ya usafi katika kituo na atapeleka taarifa kwa Kamishna au afisa mdhamini kuhusiana na mambo yote ambayo anayaona yanafaa kushughulikiwa kwa misingi ya kiafya. Pia afisa wa tiba atakuwa akiwachunguza wanafunzi wote kabla ya kuingia chuoni na kabla ya kutoka na ataweka kumbukumbu za hali ya afya ya wanafunzi. Vile vile atakuwa akiwachunguza kila siku wale wanafunzi walioko hospitali au walioko katika kifungo cha peke yao au wale wanaoumwa. Afisa wa tiba pia ana uwezo wa kutoa amri kwamba mwanafunzi yoyote asifanyishwe kazi au afanyishwe kazi nyepesi. Vile vile afisa wa tiba atakuwa mdhamini wa daftari la wagonjwa na daftari la vifo. 4.4.5.2 Wakaguzi wa Chuo Waziri anayehusika na chuo cha mafunzo ana uwezo wa kuteua watu ambao watakuwa wakivitembelea vituo vya chuo cha mafunzo kila baada ya kipindi ili kuangalia hali halisi ya vituo hivyo, pamoja na wanafunzi waliokuwemo, kuangalia viwango vya vyakula na wingi wa chakula anachopewa mwanafunzi, kusikiliza malamiko yao, na kuhakikisha kwamba masharti ya Sheria hii na kanuni zilizoweka zinafuatwa. Miongoni mwa Wakaguzi hao watakuwemo wanawake ambao watakagua vituo ambavyo wanawake wapo, kwani mkaguzi mwanamme hawezi kwenda sehemu ya wanawake na Mkaguzi mwanamke hawezi kwenda sehemu ya wanaume. Watu wafuatao ni waangalizi wa chuo kutokana na nyadhifa zao: (a). Mjumbe wa Baraza la Mapinduzi; 110 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria (b). Mjumbe wa Baraza la Wawakilishi na Mbunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania; (c). Jaji wa Mahakama Kuu; (d). Mwanasheria Mkuu; (e). Mkuu wa Mkoa kwa vituo vilivyomo kwenye mkoa wake. Vile vile itakuwepo Kamati ya Wakaguzi ambayo itajumuisha wakaguzi wote waliotajwa hapo juu. Jaji Mkuu ndiye atakayekuwa Mwenyekiti wa Kamati hiyo. Majukumu ya Kamati ni kuandaa ukaguzi wa vituo, na kujadili mambo yote yanayohusiana na uongozi wa chuo na kupeleka ripoti kwa Rais. 4.4.5.3 Upokeaji wa Wanafunzi na Nidhamu Ili mwanafunzi aweze kupokelewa chuo cha mafunzo ni lazima akipelekwa awe na hati ya kumuweka rumande au hati au amri ya kumuweka ndani au hati ya kifungo. Mtoto wa mwanafunzi wa kike pia anaweza kupokelewa chuoni ikiwa mtoto huyo ananyonya na hajatimia miezi 18. Akitimiza miezi 18 mtoto huyo atapaswa kuondoka chuoni hapo. Wanafunzi wanaopokelewa chuoni ni lazima watenganishwe, wanaume na wanawake wawekwe sehemu tofauti, watoto na watu wazima wawekwe sehemu tofauti, na pia wale waliofungwa na wale walioko rumande watenganishwe. Afisa mdhamini anatakiwa ahakikishe kwamba wanafunzi wote wanapatiwa chanjo ndani ya siku 14 tokea walipopokelewa. Kwa upande wa nidhamu, Sheria imeweka mambo mengi sana ambayo wanafunzi hawatakiwi kuyafanya wakiwepo chuoni. Mambo hayo ni kama: kutogombana na wanafunzi wengine, kutotoa malalamiko yasiyo na msingi, kutokataa kuchukuliwa alama za vidole, kutoa tuhuma za uondo dhidi ya afisa yoyote au mwanafunzi; Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 111 kuharibu chakula au kikitupa bila ya ruhusa, kukataa kula, n.k. Ikiwa mwanafunzi atafanya miongoni mwa makosa hayo afisa mdhamini ana uwezo wa kusikiliza na kuamua makosa. Katika kusikiliza kesi hiyo mwanafunzi atapewa fursa ya kusikiliza kosa na ushahidi dhidi yake na yeye kutoa utetezi wake. Afisa anaweza kutoa adhabu zifuatazo: (a). kupewa chakula cha kifungoni kwa muda usiozidi siku 4; (b). kupewa kifungo cha peke yake; pamoja na/bila ya kupewa chakula cha kifungoni kwa muda usiozidi saa 48; (c). kukatwa kwa siku zake zinazopaswa kupunguzwa zisiozidi 7; (d). adhabu ya viboko; (e). kupewa kazi ya ziada isiyozidi saa moja kwa siku kwa muda usiozidi siku 7; na (f). Kuunganisha adhabu yoyote kati ya hizi. Lakini kabla mwanafunzi hajaanza kutumikia adhabu hizi ni lazima ithibitishwe na afisa wa tiba kwamba mwanafunzi huyo anaweza kutumikia adhabu hizo. Ikiwa hawezi kutumikia adhabu hizi afisa aliyetowa adhabu atampangia adhabu nyengine. Ingawa adhabu ya viboko hivi sasa imeshafutwa katika Sheria ya mwenendo wa makosa ya Jinai. Sheria ya chuo cha mafunzo bado inayo adhabu hiyo ambayo hutolewa kwa mwanafunzi aliye kifungoni ambaye ameasi au ameshawishi watu waasi, au ametumia nguvu dhidi ya afisa wa chuo au mwanafunzi mwengine. Hata hivyo adhabu hii haitotolewa kwa mwanafunzi wa kike au wa kiume anayesubiri kifo au mwenye umri wa zaidi ya miaka 45. Adhabu hii ya viboko pia haitozidi viboko 12, na kabla ya mwanafunzi kupigwa viboko ni lazima afisa wa tiba athibitishe kwamba anaweza kutumikia adhabu hiyo. 112 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Mwanafunzi aliyepatikana na kosa ikiwa atapenda anaweza kuipeleka kesi yake kwa Kamishna kwa kufanyiwa mapitio. Afisa mdhamini anatakiwa amueleze mwanafunzi haki hii. 4.4.5.4 Haki za Wanafunzi Wanafunzi walioko chuo cha mafunzo wana haki zifuatazo: (a). haki ya kuthaminiwa kwa dini yake, na kupata sehemu ya kuabudu; (b). haki ya kutembelewa na ndugu na marafiki mara moja kila mwezi; (c). haki ya kupokea barua na kuandika na kutuma barua moja kila mwezi; (d). haki ya kumuelezea mkaguzi wa chuo jambo lolote analoliona ni muhimu kulieleza; (e). haki ya kupewa kazi au mafunzo; (f). haki ya kutibiwa anapoumwa; (g). haki ya wanafunzi wanawake kushughulikiwa na maafisa wanawake na wanaume kushughulikiwa na maafisa wanaume; (h). haki ya kupewa nguo za chuoni, vitanda na mashuka isipokuwa kwa wanafunzi wa rumande. Kwa wanafunzi waliopo rumande wana haki ya kuwasiliana na jamaa zao na marafiki kwa mujibu wa kanuni. Wanaweza kujishugulikia wenyewe kwa kununua vitu wao wenyewe katika muda muafaka kama vyakula, vifaa vya kulalia, nguo pamoja na vitu vyengine muhimu. Ikiwa hawezi kupata vitu hivyo yeye mwenyewe basi atapewa vitu vya kawaida vya chuoni. Kwa baadhi ya wanafunzi pia ipo haki ya adhabu yao kufanyiwa mapitio. Wanafunzi hao ni wanafunzi watoto na watu wazima ambao adhabu zao hazijawekewa kiwango.(Mapitio hayo yanaweza kufanywa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 113 baada ya kumaliza mwaka mmoja), na wanafunzi watu wazima ambao wanaotumikia miaka 8 mapitio yanafanywa baada ya kutumikia miaka 4. 4.4.6 Tume ya Utumishi ya Idara Maalum Ingawa Idara hizi zote tano zinazo Sheria zao, lakini masuala yote yanayohusiana na ajira, upandishaji na ushushaji vyeo, mishahara, uteuzi, na hatua za kinidhamu yanaamuliwa kwa mujibu wa Sheria ya Tume ya Utumishi ya Idara Maalum Namba 7 ya 1986. Katika kutekeleza majukumu yake Tume inaweza kumtaka mtumishi yeyote wa Serikali au Idara Maalum afike mbele yake kwa kutoa maelezo kuhusiana na suala lolote linalozingatiwa na Tume. Hivyo, ikiwa mtu hakutendewa haki na Idara yake au hakuridhika na maamuzi yaliyotolewa katika Idara yake anaweza kupeleka malalamiko yake mbele ya Tume hii. Mtu yeyote pia asiyeridhika na maamuzi ya Tume hii anaweza kukata rufaa kwa Waziri Kiongozi. 114 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria SURA YA TANO 5.0 Sheria Mbali Mbali 5.1 Sheria za Kazi Katika Sura hii tutaziangalia Sheria za Kazi zinazotumika Zanzibar. Sheria hizi ni zile zinazomuongoza mfanyakazi kuanzia anapoomba na kufanikiwa kupata ajira hadi anapofikia umri wa kustaafu. Sheria hizi pia zimeweka majukumu ya waajiri na waajiriwa katika sehemu za kazi na zinaongoza mahusiano ya mwajiri na mwajiriwa kwa ujumla. Sheria hizi za kazi zipo tano, nazo ni: Sheria ya Ajira Namba 11 ya 2005, Sheria ya Mahusiano Kazini Namba 1 ya 2005, Sheria ya Afya na Usalama Kazini Namba 8 ya 2005, Sheria ya Fidia ya Wafanyakazi Namba 15 ya 1986 na Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Namba 2 ya 2005. Katika sehemu hii tutayaangalia mambo muhimu yaliyomo ndani ya Sheria hizi. 5.2 Sheria ya Ajira 5.2.1 Mkataba wa Ajira Katika hali ya kawaida unapokubaliana na mtu mwengine kumfanyia jambo fulani na mtu huyo akakubali kukulipa kwa kufanya jambo hilo tunasema kwamba mmeingia kwenye mkataba. Hivyo, ukikubali kufanya kazi kwa mtu na mtu huyo akakubali kukulipa kwa kazi uliyofanya tunasema kwamba umeingia katika mkataba wa ajira. Wewe unayefanyakazi unakuwa mwajiriwa na yule unayemfanyia kazi na ambaye anakulipa ni mwajiri. Mikataba ya ajira mara nyingi inakuwa na masharti kadhaa ambayo yanaitwa masharti ya ajira. Masharti haya yapo yalio waziwazi kwa Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 115 mfano pahala pa kufanyia kazi, mshahara, aina ya kazi, masaa ya kazi n.k. vilevile yapo masharti ambayo hayatajwi lakini yanaeleweka kuwa yapo, kwa mfano uchukuaji wa likizo, mapumziko katika wiki n.k. Mikataba ya ajira ipo ya aina 4: mikataba ya kudumu, mikataba ya baadhi ya wakati, mikataba ya kutwa, na mikataba ya muda maalum. Mikataba pia inaweza kuwa ya maandishi au ya maneno tu. Lakini Sheria inataka mikataba ya ajira inayoanzia miezi sita iwe ya maandishi, na imeweka kuwa ni kosa kwa mtu yeyote kumuajiri mwengine kama mfanyakazi wa kutwa kwa kazi inayohitaji uajiri wa kudumu. Mkataba wa ajira kabla ya kuanza kutumika unapaswa kuthibitishwa na afisa wa kazi ambaye jukumu lake kubwa ni kuhakikisha kwamba mwajiriwa ameyafahamu masharti ya mkataba na hayapingani na Sheria. Pia afisa huyo anapaswa kuhakikisha kwamba mwajiriwa anayo ripoti ya uchunguzi wa afya inayothibitisha kwamba mwajiriwa huyo anaweza kufanya kazi atakayoajiriwa. Mkataba wa kazi pia unaweza kuhaulishwa kwa muajiri mwengine lakini mwajiriwa lazima kwanza aridhie, asiporidhia itachukuliwa kuwa mkataba umemalizika na mwajiriwa atapaswa kulipwa haki zake anazostahiki chini ya mkataba. Ikiwa ataridhia haki zake zitakwenda kwa mwajiri mpya. Vile vile mkataba wa ajira unaweza kukatishwa ikiwa: (a). muda wa mkataba umemaliza; (b). mwajiriwa amefariki; (c). mwajiri amefariki na biashara imesita; (d). itakapothibitishwa na madaktari kwamba mwajiriwa hawezi kumudu kazi; 116 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria (e). mwajiriwa anapofukuzwa kazi kutokana na tabia mbaya au kutokana na kutofaa kwenye kazi hiyo; (f). mwajiriwa anapokataa kuhamishwa kwenda kwa mwajiri mwengine; (g). pale taasisi inaposita kufanya kazi kwa kipindi kinachozidi miezi 3; na (h). pale mwajiri au kampuni yake inapofilisika. 5.2.2 Matumizi ya Sheria na Haki za Msingi Sheria hii inatumika kwa wafanyakazi wote walioajiriwa katika sekta ya umma(Serikali) na Sekta binafsi, lakini haitumiki kwa askari wa vikosi ya ulinzi, polisi na usalama, wafanyakazi wa Idara maalum za SMZ(JKU, KMKM, Mafunzo, Valantia na Zimamoto), manahodha wa meli na mabaharia(wao wanatumia Sheria ya Usafiri Baharini 2006), na aina au ngazi ya maafisa wa umma ambao watatajwa na Waziri. Sheria hii imeweka haki za msingi zinazohusiana na masuala ya ajira. Haki hizo ni: (a). kutofanyishwa kazi ya shurti; (b). kutobaguliwa katika kazi; (c). kutowafanyisha kazi watoto; (d). kutowaajiri vijana wanaosoma, na kwa wasiosoma kutowaajiri katika ajira mbaya; (e). kukataza udhalilishaji wa kijinsia. Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 117 5.2.3 Viwango na Haki za Waajiriwa Sheria hii imeweka viwango maalum katika masuala ya ajira. Viwango hivyo ni: Saa za kazi ± saa za kazi zisizidi 8 kwa siku au 42 kwa wiki. Ikiwa ni kazi za zamu saa zinaweza kuzidi 8, lakini wastani usizidi saa 48 kwa wiki. Lakini mwajiri kwa makubaliano na mwajiriwa anaweza kumruhusu mwajiriwa kufanyakazi muda wa ziada lakini si zaidi ya saa 10 ya muda wa ziada kwa wiki na si zaidi ya saa 12 kwa siku yoyote ile. Siku ya mapumziko ± mwajiriwa hatakiwi kufanya kazi kwa zaidi ya siku 6 mfululizo bila ya kupewa siku 1 ya mapumziko. 5.2.4 Haki za Waajiriwa Waajiriwa wanaweza kuwa na haki zifuatazo kulingana na aina ya ajira pamoja na makubaliano waliyofanya na mwajiri. Haki hizo ni: (a). Haki ya kupata usafiri na makaazi; (b). Haki ya kupata posho ya chakula; (c). Haki ya kupata gharama za dawa na matibabu; (d). Haki ya kupata nauli ya safari; (e). Haki ya kurejeshwa nyumbani baada ya kumaliza mkataba wa ajira; (f). Haki ya kulipwa fidia mwajiriwa anapofariki au kuumia; (g). Haki ya kupewa vifaa vya kufanyia kazi; (h). Haki ya kupewa cheti cha utendaji baada ya kumaliza mkataba wa ajira; 118 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria (i). Haki ya likizo: likizo ya uzazi, likizo ya maradhi, likizo bila ya malipo, likizo ya kawaida na likizo ya dharura; na (j). Haki kwa ajili ya makundi maalum. 5.2.5 Hatua za Kinidhamu na Adhabu Sheria hii imeweka misingi imara ya hatua za kinidhamu zinazoweza kuchukuliwa dhidi ya mwajiriwa, pamoja na adhabu zinazoweza kutolewa na muajiri kwa mwajiriwa. Mwajiri anaweza kutoa adhabu za kinidhamu kwa mwajiriwa yoyote kwa utovu wa nidhamu, uzembe au kushindwa kutekeleza wajibu wake chini ya mkataba wa ajira. Lakini adhabu zitakazotolewa kwa waajiriwa lazima zifuate utaratibu uliowekwa na Jadweli iliyomo kwenye Sheria hii. 5.2.6 Usimamizi wa Sheria Kamisheni ya Kazi ndio inayosimamia Sheria hii kwa mambo yote yanayotokea katika sekta binafsi na sekta ya umma. Kamisheni ya Kazi inaongozwa na Kamishna kwa Unguja na Afisa Mkuu wa Kazi kwa Pemba. Pia katika kila Mkoa yupo Afisa wa Kazi wa Mkoa, na katika kila Wilaya yupo Afisa wa Kazi wa Wilaya. Hawa hushughulikia masuala ya kazi katika sehemu zao, na chini yao wapo maafisa wa kazi. Hivyo, linapotokea tatizo katika sehemu ya kazi hao ni watu wa mwanzo wa kupelekewa malalamiko. Sheria imewapa uwezo wa kuchunguza na kushughulikia malalamiko kwa njia ya usuluhishi, masikilizano au kwa utaratibu wowote watakaoona unafaa na kukubalika na pande zote mbili. Lakini endapo atashindwa kulipatia ufumbuzi tatizo hilo ndani ya siku 21 anatakiwa aliwasilishe tatizo hilo kwa Kamishna au Afisa Mkuu kwa Pemba ambaye Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 119 ataliwasilisha jambo hilo katika Mahakama ya Kazi kwa kutolewa maamuzi. 5.3 Sheria ya Mahusiano Kazini Ili maendeleo yaweze kupatikana mahusiano mazuri katika sehemu ya kazi ni jambo la lazima. Sheria hii imeweka utaratibu wa mahusiano baina ya waajiriwa na waajiri. Waajiriwa wanaweza kujikusanya pamoja na kuunda vyama vyao na baadae kukaa na mwajiri au jumuiya ya waajiri kuzungumza masuala yanayohusu kazi na kuweka utaratibu watakaoona unafaa. 5.3.1 Haki za Msingi Sheria imeweka haki za msingi kwa pande zote mbili yaani waajiri na waajiriwa. Kwa upande wa waajiriwa haki zao za msingi ni kushiriki katika uundaji wa chama cha wafanyakazi au jumuiya ya vyama vya wafanyakazi; na kuwa mwanachama wa chama cha wafanyakazi ambapo ataweza kugombea uongozi, kuchagua viongozi na kushiriki katika shughuli halali za chama hicho. Haitokuwa halali kwa mwajiri yoyote kukatisha mkataba wa ajira au kumbagua mwajiriwa kwa namna yoyote ile kwa sababu tu anashiriki katika shughuli za chama cha wafanyakazi. Kwa upande wa waajiri nao wana haki ya kushiriki katika uundaji wa chama cha waajiri au kuwa mwanachama wa jumuiya ya waajiri na kushiriki katika shughuli zote zinazohusiana na jumuiya hiyo. Vile vile mwajiri anatakiwa aruhusu shughuli za chama cha wafanyakazi katika sehemu ya kazi na chama hicho kinaweza kufungua tawi sehemu hiyo na kufanya mikutano halali ya tawi. 120 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 5.3.2 Mapatano na Makubaliano ya Pamoja Waajiriwa wote ambao hawamo katika safu ya uongozi wana haki ya kufanya mapatano ya pamoja na mwajiri au jumuiya ya waajiri kwa kupitia vyama vyao vya wafanyakazi. Makubaliano yanaweza kufanywa katika mambo yafuatayo: (a). kuweka mazingira ya kazi na masharti ya ajira; (b). kuratibu mahusiano baina ya waajiri na waajiriwa; (c). kuratibu mahusiano baina ya waajiri au jumuiya zao na vyama vya wafanyakazi; na (d). kuratibu mambo yoyote yanayoruhusiwa na Sheria na ambayo yanaonekana na wahusika kuwa ni muhimu. Chama kinachowawakilisha waajiriwa wa sehemu fulani ya kazi ndicho chenye haki ya kufanya mapatano. Lakini mapatano yanaweza kufanywa katika ngazi tofauti kama sehemu moja ya kazi, kiwanda kizima au sekta nzima, au katika ngazi ya taifa. Baada ya kufanyika mapatano na wahusika kukubaliana, makubaliano hayo yatazibana pande zote mbili, na makubaliano hayo yatawasilishwa Mahakamani kwa kusajiliwa na nakala kupelekwa Kamisheni ya Kazi. 5.3.3 Migogoro ya Kazi Kutokea kwa migogoro katika sehemu ya kazi ni kitu kisichoweza kuepukwa. Sheria imeweka utaratibu wa hatua za kuchukuliwa migogoro inapotokea. Unapotokea mgogoro wa maslani na sio wa haki, waajiriwa wanaweza wakagoma na mwajiri anaweza akawafungia nje ya sehemu ya kazi. Lakini kabla ya kufikia hatua hii, inatakiwa hatua zote muhimu za kutatua mgogoro ziwe zimeshachukuliwa na mwajiri na mwajiriwa na kushindwa. Lakini Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 121 kabla ya kuchukua hatua hiyo wanatakiwa watoe notisi ya saa 48 ya maandishi kabla ya mgomo au kufungiwa nje kwa waajiriwa. Baadhi ya waajiriwa hawaruhusiwi kushiriki katika migomo. Waajiriwa hawa ni wale walio katika nafasi ya uongozi na wale waajiriwa wanaotoa huduma za lazima kama umeme, maji, afya, wazima moto n.k. Sheria pia imeanzisha kitengo cha kushughulikia migogoro ya kazi ambacho kipo chini ya Kamisheni ya Kazi. Hivyo, mgogoro wowote wa kazi unapotokea au unapodhaniwa kuwa unaweza kutokea kwanza lazima upelekwe kwenye kitengo hichi ambacho kitashughulikia mgogoro huo kwa kumteua mpatanishi atakayewapatanisha wahusika. Endapo mpatanishi atashindwa kutatua mgogoro huo, wahusika wanaweza kukubaliana kuupeleka kwa wasuluhishi. Lakini ikiwa wataamua kutoupeleka mgogoro huo kwa wasuluhishi wahusika watakuwa na haki ya kugoma kwa upande wa waajiriwa na mwajiri naye atakuwa na haki ya kuwafungia nje. Kunapokuwa na mgogoro wa haki na mpatanishi ameshindwa kupatanisha, mgogoro huo lazima uende kwa wasuluhishi. Lakini ikiwa mgogoro unahusiana na Katiba au ufafanuzi wa Sheria, mgogoro huo lazima upelekwe Mahakama ya Kazi. 5.4 Sheria ya Usalama na Afya Kazini Usalama na afya kazini ni mambo muhimu katika masuala ya kazi. Ili mwajiriwa aweze kuzalisha katika sehemu yake ya kazi ni lazima awe na afya nzuri na sehemu anayofanya kazi iwe na usalama wa kutosha. Sheria hii imeweka masharti bora zaidi yatakayowafanya waajiri wazingatie usalama na afya za waajiriwa. Masharti hayo ni pamoja na: 122 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria (a). usajili wa sehemu zote za kazi pamoja na mitambo na zana zinazotumika katika uzalishaji au kutoa huduma; (b). matumizi ya vifaa vya kinga za ajali na maradhi yanayotokana na ajira; (c). utoaji taarifa za ajali na maradhi yanayotokana na ajira; (d). kuundwa kwa chombo cha kusimamia afya na usalama; (e). ukaguzi wa usalama na afya katika sehemu za kazi. 5.4.1 Usimamizi wa Usalama na Afya Sheria hii imeanzisha kurugenzi ya usalama na afya kazini ambayo inaongozwa na Mkurugenzi na itakuwa chini ya Kamisheni ya Kazi. Pia Waziri atateua wakaguzi ambao watakuwa na uwezo wa kuingia na kukagua sehemu yoyote ya kazi wanayoitilia mashaka. Ikiwa Mkaguzi atazuiliwa kuingia anaweza kutumia afisa wa polisi katika kuingia sehemu hiyo. Katika ukaguzi wake anaweza kukagua daftari, cheti, notisi, hati, mitambo, mashine pamoja na kitu chochote kilichopo sehemu hiyo ya kazi. Pale Mkurugenzi anapofanya maamuzi yake na ikiwa mtu yoyote hakuridhika na maamuzi hayo mtu huyo anaweza kukata rufaa kwenye Kamati ya Usalama na Afya Kazini. 5.4.2 Uteuzi wa Wawakilishi wa Usalama na Afya Kazini Mwajiri aliyeajiri waajiriwa 10 au zaidi anatakiwa ndani ya miezi 4 kuanzia tarehe ya kutumika kwa Sheria hii au baada ya kuanza shughuli zake au kuanzia pale waajiriwa watakapofikia 10 kuteua kwa maandishi wawakilishi wa usalama na afya kazini hapo. Wawakilishi hao watafanya shughuli hiyo kwa muda utakaotajwa na mwajiri kwa utaratibu uliowekwa na mwajiri na waajiriwa wake au wawakilishi hao. Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 123 Kazi za wawakilishi hawa ni: (a). kuangalia ufanisi wa hatua za usalama na afya; (b). kutambua hatari au ajali zinazoweza kuzuka katika sehemu za kazi; (c). kushirikiana na mwajiri katika kuchunguza vyanzo vya ajali kazini; (d). kuchunguza malalamiko ya mwajiriwa yoyote kuhusiana na afya na usalama wake kazini; (e). kuwasilisha malalamiko kwa mwajiri na pale wanaposhindwa kuyatatua, kuyapeleka kwa mkaguzi; (f). kukagua hati zozote ambazo mwajiri anatakiwa kuweka kwa mujibu wa Sheria hii kwa kadri ya umuhimu unaohitajika katika kufanya kazi zake; (g). kuongozana na mkaguzi katika ukaguzi; (h). kushiriki katika tathmini ya ndani ya usalama na afya; (i). kutoa ripoti kwa mkaguzi kuhusu ajali, makoseo ya ajali, majeraha, magonjwa, vifo na kutofuatwa kwa Sheria. 5.4.3 Masharti ya Usalama, Afya na Ustawi Sheria inataka majengo ya sehemu za kazi yawe madhubuti. Jengo liwe katika hali itayowalinda waajiriwa kutokana na hali ya hewa, mapaa yasiyovuja, lisiwe na unyevunyevu unaoweza kuliathiri jengo lenyewe au afya za wafanyakazi, na liwe katika hali ya kuwawezesha watu wenye ulemavu waweze kuingia kwa urahisi. Hatua madhubuti zichukuliwe kadri inavyowezekana kuzuia waajiriwa kuathirika na kelele wanapokuwa kazini. Mwajiri anawajibu wa kuweka maji ya kunywa yaliyo safi. Kila sehemu ya kazi iwe na vyoo vya kutosha kwa ajili ya waajiriwa na 124 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria viwe safi pamoja na kuwa na taa. Pia patenganishwe kati ya vyoo vya wanawake na wanaume na kwa wastani kila choo kimoja kihudumie si zaidi ya watu 25. Pawe na vyombo vya kunawia kutegemeana na aina ya kazi. Iwepo sehemu ya kutosha na inayofaa kuweka nguo ambazo hazivaliwi wakati wa kufanya kazi na sehemu hiyo itenganishwe baina ya wanaume na wanawake. Aidha mwajiri anapaswa kuweka kisanduku cha huduma ya kwanza kikiwa na vifaa vya huduma hiyo na kitunzwe na mtu aliyepata mafunzo ya huduma ya kwanza. Mwajiriwa anapoumia na kuhitaji matibabu zaidi uwepo usafiri wa uhakika wa kumfikisha hospitali. Masharti mengine ni kuwepo kwa vikalio kwa waajiriwa wanaosimama, kuondoa vumbi au moshi iwapo kazi inayofanywa inatoa vumbi au moshi au uchafu mwengine wa aina ya kiasi ambacho kinaweza kuleta madhara au kero kwa waajiriwa. Endapo waajiriwa wanafanya kazi inayowakaribisha na kitu chochote chenye kudhuru au katika mazingira ya hatari muajiri anapaswa kuwapatia vifaa maalum vya kinga. Kazi kama vile za uchomaji na uunganishaji vyuma hatua madhubuti zichukuliwe kuwakinga na mwangaza. Kwa waajiri waliojiajiri wenyewe wana wajibu wa kuhakikisha kwamba watu wanaokuja katika sehemu zao za kazi hawapati madhara ya usalama au afya zao. Kila baada ya muda waajiriwa wanatakiwa wachunguzwe afya zao na madaktari wenye sifa ambao wataidhinishwa na Mkurugenzi. Gharama za uchunguzi zitalipwa na mwajiri. Madaktari nao wana wajibu wa kuficha siri za matokeo ya uchunguzi huo. Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 125 5.4.4 Haki na Wajibu wa Waajiriwa Mwajiriwa anapokuwa kazini ana wajibu ufuatao: (a). kuchukua hadhari kwa usalama na afya yake binafsi na watu wengine ambao wanaweza kuathirika na utendaji kazi wake; (b). kushirikiana na wenzake kama inavyohitajika kuwezesha wenzake kutimiza wajibu au masharti wanayotakiwa kuyatimiza; (c). kuripoti hali ya hatari; (d). kutoharibu kwa makusudi au kwa uzembe kitu kilichowekwa kwa ajili ya afya, usalama au ustawi kutokana na masharti ya Sheria hii. Kila penye wajibu pia pana haki. Mwajiriwa ana haki zifuatazo: (a). haki ya kukimbia hatari. Mwajiriwa anahaki ya kuondoka sehemu ya kazi endapo anaamini kwamba hatari inaweza kutokea na kusababisha hasara kwa maisha au afya. Mwajiriwa huyo hatochukuliwa hatua za kinidhamu ikiwa hatari hiyo itathibitishwa na Mkurugenzi. (b). Haki ya kutoadhibiwa kutokana na tendo lolote alilolifanya katika kutekeleza masharti ya Sheria hii. 5.5 Sheria ya Fidia ya Wafanyakazi Mwajiriwa anapokuwa kazini anaweza kupata madhara ambayo yanaweza kupelekea kupoteza maisha au kupata maumivu yatakayomfanya asiweze kufanya kazi tena, au maumivu yatakayopunguza uwezo wake wa kufanya kazi. Sheria imeweka utaratibu wa kumlipa fidia mwajiriwa huyu anapoumia. Lakini pia imeweka masharti kwamba maumivu yawe yanatokana na kazi 126 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria anayoifanya au akiwa ndani ya kazi hiyo. Mwajiriwa hatolipwa fidia ikiwa madhara yenyewe yamemfanya asifanye kazi kwa kipindi cha chini ya siku 3, au ikiwa itathibitika kwamba madhara hayo yamesababishwa na vitendo vya makusudi vya mwajiriwa, au ikiwa madhara au kifo ni matokeo ya maumivu ambayo mwajiriwa kwa kujua kwamba ni maelezo ya uongo alieleza kwa maandishi kuwa hana maumivu na hajapata kuumia. Ingawa Sheria hii imeweka fidia anayopaswa kulipwa mfanyakazi anapoumia, lakini haimzuii mfanyakazi huyo kwenda Mahakamani kufungua kesi ya madai endapo maumivu yake yamesababishwa na uzembe au kitendo cha makusudi cha muajiri au mtu mwengine ambaye muajiri ndiye mwenye dhamana. Lakini endapo mfanyakazi ataamua kufungua kesi ya madai na hukumu kutolewa hatoweza tena kufungua madai chini ya Sheria hii kuhusiana na maumivu yale yale. Hali kadhalika hukumu itakayotolewa chini ya Sheria hii pia itamzuia mfanyakazi huyo kufungua kesi ya madai kwa maumivu yale yale. Hivyo, ni kusema kuwa mfanyakazi anatakiwa achague sehemu moja ya kupeleka madai. 5.5.1 Fidia Kutokana na Maumivu Endapo madhara yatakayomtokea mfanyakazi akiwa kazini yatasababisha kifo, na ikiwa mfanyakazi aliyefariki ameacha warithi kiwango cha fidia atakayolipwa ni sawa na kipato chake cha miezi 36, gharama za mazishi ambazo zisizopungua thuluthi moja ya gharama zote. Lakini endapo madhara yaliyotokea yamemsababisha asiweze kufanyakazi tena kiwango cha fidia atakacholipwa kitakuwa ni sawa na kipato cha miezi 48 au shilingi milioni tano, chochote kilichokuwa kikubwa. Lakini ikiwa madhara yaliyompata mfanyakazi huyo ni kwamba ni lazima wakati wote apate msaada wa mtu mwengine, ataongezwa fidia anayolipwa kwa robo ya kiwango anachopaswa kulipwa. Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 127 Endapo madhara yaliyotokea yamemsabisha mfanyakazi asiweze kufanya kazi kwa ukamilifu, kiwango cha fidia atakacholipwa kitakuwa ni asilimia itakayowekwa na daktari ya kipato cha miezi 48. Katika kupanga viwango vya asilimia chini ya Sheria hii daktari ataongozwa na asilimia zilizowekwa katika Jadweli ya Kwanza ya Sheria hii. Endapo madhara yaliyotokea yamemsabisha mfanyakazi asiweze kufanya kazi kwa muda ikiwa kwa ukamilifu, au kutoweza kabisa, kiwango cha fidia atakacholipwa kitakuwa ni malipo ya vipindi kama watakavyokubaliana na muajiri au Mahkama itakavyoamrisha au malipo ya pamoja yatakayofanyiwa hesabu kwa kuzingatia muda atakaokuwa hawezi kufanya kazi na kubadilika kwa hali ya kutoweza kufanya kazi. Malipo hayo ya vipindi yatakuwa ni nusu ya malipo ya mwezi ambayo yataangalia kipato chake kabla ya ajali na kutoa kipato anachopata baada ya ajali au anachoweza kupata katika kazi anayoiweza kuifanya. Lakini malipo haya ya vipindi hayatozidi miezi 96. Katika kupanga malipo haya ya vipindi au malipo ya pamoja, malipo yaliyokwisha fanywa, marupurupu au faida nyengine ikiwemo chakula, mafuta, au makaazi yatakatwa kutoka katika kiwango hicho. 5.5.2 Fidia kwa Wachumaji Karafuu Katika kuwaangalia wachumaji karafuu, Serikali inawachakulia kama ni wafanyakazi walioajiriwa na Serikali kufanya kazi hiyo ya uchumaji karafuu. Hivyo wachumaji karafuu wanapopata madhara kutokana na ajali inayotokana na kazi hiyo au ndani ya kazi hiyo, muajiri wao ambaye ni Serikali anapaswa kuwalipa fidia kwa mujibu wa Sheria hii. Mshahara wa wafanyakazi hawa unachukuliwa kuwa ni mshahara wa kima cha chini uliowekwa na Serikali. 128 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kama ilivyo kwa wafanyakazi wengine nao pia hawatolipwa fidia ikiwa madhara yenyewe yamemfanya mfanyakazi asifanye kazi kwa kipindi cha chini ya siku tatu, au ikiwa itathibitika kwamba madhara hayo yamesababishwa na vitendo vya makusudi vya mfanyakazi, au ikiwa madhara au kifo ni matokeo ya madhara aliyojitia yeye mwenyewe kwa makusudi. Lakini ikiwa vitendo hivyo vya makusudi vimepelekea kifo au kushindwa kufanya kazi tena Mahakama inaweza kutoa fidia baada ya kuzingatia mazingira ya tukio hilo. 5.5.3 Fidia kwa Wanamichezo Kwa upande wa wanamichezo Sheria hii inawachukulia kama ni wafanyakazi na mtu aliyewaajiri ndio muajiri wao, lakini vyama au vikundi vya michezo havihesabiwi kama ni muajiri. Wanamichezo wanapopatwa na madhara nao pia wanapaswa kulipwa fidia kama waajiriwa wengine. 5.5.4 Madai ya Fidia Watu wanaopaswa kudai fidia ni waajiriwa walioumia au ikiwa ajali imesababisha kifo watu wanaomtegemea mwajiriwa aliyefariki. Madai ya fidia hayatosimama mpaka kwanza notisi ya ajali itolewe mapema iwezekanavyo katika fomu iliyoainishwa kwa niaba ya mfanyakazi aliyeumia, na kabla ya mfanyakazi hajaondoka kwenye ajira ambayo ameumia. Kwa upande wa mwajiri ikiwa ajali iliyotokea inapaswa kulipwa fidia, naye anatakiwa kutoa notisi ya ajali katika fomu iliyoainishwa kwa Mkurugenzi wa Ustawi wa Jamii au Naibu wake haraka iwezekanavyo na kabla mfanyakazi aliyeumia hajaondoka kwenye ajira ambayo ameumia. Ikiwa kifo kimetokea ndani ya ajira na muajiri amepelekewa notisi kwa niaba ya mfanyakazi au anayo taarifa, naye anatakiwa atoe notisi kwa Mkaguzi wa Afya au afisa mwengine aliyeruhusiwa haraka iwezekanavyo, na notisi hiyo itaeleza mazingira ya kifo cha mwajiriwa kama mwajiri anayajuwa. Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 129 Mara baada ya mfanyakazi kutoa notisi ya ajali muajiri anatakiwa haraka iwezekanavyo aandae utaratibu wa mfanyakazi huyo kuchunguzwa afya yake na daktari kwa gharama za mwajiri. Ikiwa mfanyakazi atashindwa kwenda kufanyiwa uchunguzi, haki yake ya fidia itasimamishwa mpaka uchunguzi ufanywe. Haki hii ikisimamishwa maana yake ni kuwa hatolipwa kitu kwa siku ilizosimamishwa, na ikiwa ameshindwa kwenda kufanyiwa uchunguzi na kipindi cha siku 15 kimepita, hapana fidia atakayolipwa mpaka Mahkama iridhike kwamba kulikuwa na sababu ya msingi ya kutofika huko. Lakini mwajiriwa anayo haki ya kwenda kwenye uchunguzi huo pamoja na daktari wake atakayemlipia mwenyewe. Ikiwa mwajiriwa aliyepata madhara atashindwa kufanyakazi kwa muda, muajiri ataandaa mpango kwa ajili ya mwajiriwa huyo kupata matibabu ya kawaida kwa daktari wa mwajiri au daktari wa mwajiriwa aliyekubaliwa na mwajiri kwa gharama za mwajiri. Lakini ikiwa mwajiriwa atashindwa kwenda kwa daktari, au baada ya kwenda kwa daktari amepuuza maelekezo ya daktari, na itathibitika kwamba kupuuza huko hakukuwa na msingi na matokeo yake maumivu yamezidi. Kuzidi huko kwa maumivu hakutotiwa maanani na itachukuliwa kama mwajiriwa amekwenda kwa daktari na amefuata maelekezo ipasavyo. Vile vile ikiwa kupuuza huko kufuata maelekezo ya daktari kumesababisha kifo, kifo hicho hakitochukuliwa kuwa kimesababishwa na madhara hayo na hapana fidia atakayolipwa mwajiriwa huyo. Madai yote chini ya Sheria hii ikiwa mwajiri na mwajiriwa wameshindwa kukubaliana kwa maandishi yataamuliwa na Mahakama ya Mkoa. 130 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 5.5.5 Maradhi Yanayotokana na Ajira Jadweli la pili la Sheria hii limeorodhesha maradhi mbali mbali ambayo yanapatikana kutokana na mtu kufanya kazi ya aina fulani. Hivyo, ikiwa daktari atatoa cheti kuthibitisha kwamba mwajiriwa amepata maradhi hayo na yamempunguzia uwezo wake wa kufanya kazi au yamemsababishia kifo na maradhi hayo ameyapata ndani ya miezi 24 kabla ya kushindwa kufanya kazi au kifo. Mwajiriwa huyo au akiwa amefariki wanaomtegemea watapaswa kudai fidia chini ya Sheria hii kama kwamba matokeo hayo yamesababishwa na ajali. Mahakama baada ya kusikiliza kesi na ikiwa imeridhika kwamba tuhuma zilizomo ndani ya cheti ni sahihi, mwajiriwa au wanaomtegemea watapaswa kupata fidia chini ya Sheria hii. Fidia hiyo italipwa na mwajiri aliyemuajiri mwisho mwajiriwa huyo katika kipindi cha miezi 24 isipokuwa kama mwajiri huyo atathibitisha kwamba maradhi hayo hakuyapata wakati akifanya kazi kwake. Ikiwa mwajiri atasema hivyo anaweza kumuunganisha muajiri mwingine wa awali katika kesi hiyo na ikithibitika kwamba hayo maradhi ya mfanyakazi ameyapata kwa huyo mwajiri mwengine, mwajiri huyo atapaswa kulipa fidia. 5.6 Sheria ya Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Baada ya mwajiriwa kufanyakazi na kufikia umri wa kustaafu kwa hiari(miaka 55) au kustaafu kwa lazima(miaka 60) suala linalofuata ni kupata mafao yake chini ya Sheria hii. Msimamizi wa Sheria hii ni Bodi iliyoundwa chini ya Sheria hii ambayo ina jukumu la kuhakikisha kuwa wanachama wa mfuko, na warithi wa mwanachama wanapata mafao yao mara tu yanapohitajika. Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 131 5.6.1 Michango Katika Mfuko Kila mwanachama anatakiwa kuchangia asilimia 5 ya mshahara wake wa mwezi na mwajiri atamkata mwajiriwa malipo hayo na kuyawasilisha mfuko wa hifadhi ya jamii pamoja na mchango wa mwajiri ambao ni asilimia 10 ya mshahahara wa mwajiriwa. Michango hii italipwa katika mfuko ndani ya siku 15 kutoka tarehe uliolipwa mshahara. Kwa upande wa watu waliojiajiri wenyewe Waziri kwa kushauriana na Bodi anaweza kutunga kanuni kwa ajili ya michango kuwekwa na watu waliojiajiri wenyewe. Mwajiri yoyote atakapoacha kukata michango hiyo, au atakapokata michango hiyo lakini akashindwa kuiwasilisha katika mfuko ndani ya siku 15, basi mwajiri huyo atawajibika kulipa adhabu ya asilimia 5 ya michango hiyo kwa kila mwezi au sehemu ya mwezi kuanzia tarehe ambayo alipaswa awasilishe malipo hayo. Aidha kiwango chochote kinachodaiwa na hakijalipwa kwa miezi mitatu tokea kilipotakiwa kulipwa, kitatozwa riba ya asilimia 5. 5.6.2 Mafao Yanayotolewa na Mfuko Mfuko unatoa mafao yafuatayo: (a). Mafao ya uzeeni yanayojumuisha pamoja na pensheni na kiinua mgongo; (b). Mafao ya warithi; (c). Mafao ya uzazi; (d). Mafao ya ulemavu; (e). Mafao ya matibabu; na (f). Mafao mengine yoyote yatakayothibitishwa na Bodi. 132 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Ingawa mafao haya yote yametajwa lakini hadi leo hayajaanzwa kulipwa, mafao yanayolipwa ni ya uzeeni, yanayojumuisha pensheni na kiinua mgongo. Mafao mengine yanayolipwa ni yale yanayopaswa kulipwa kwa warithi pale mwanachama anapofariki kabla ya kustaafu au baada ya kustaafu lakini kabla ya kulipwa mafao yake. Warithi wa marehemu watastahiki kulipwa kiinua mgongo. Kila mwanachama wa mfuko anastahiki kupata pensheni na kiinua mgongo baada ya kustaafu kwa kufikia umri wa kustaafu au kutokana na sababu za kiafya ambapo Bodi imeridhika kwamba mwajiriwa hawezi kabisa kufanya kazi. Lakini pia mwanachama hatolipwa pensheni na kiinua mgongo ikiwa: (a). Muda wake wa michango ni chini ya miezi 60; (b). Akiwa katika majaribio ya kazi, mpaka pale atakapothibitishwa kazini; (c). Pale mwanachama anapokuwa hayupo kazini kutokana na likizo bila ya malipo. Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 133 VITABU VILIVYOCHAGULIWA VYA MAREJEO A History of Zanzibar: A Study in Constitutional Development 1934-1964, kimeandikwa na Samuel G. Ayang, Nairobi: Kenya Literature Bureau, 1970. Adhabu ya Kifo Katika Uislam, Kimeandikwa na Sheikh Muhiddin Ahmed Khamis Zanzibar: Kituo Cha Huduma za Sheria Zanzibar(2008). Babu: I Saw the Future and it Works ± Essays Celebrating the Life of Comrade Abdulrahman Mohamed Babu 1924-1996, Kimehaririwa na Prof. Haroub Othman, Dar es Salaam: E&D Publishers, 2001. Comparative Democracy and Cultural Wisdom: Africanity, Islam and the West, kimenadikwa na Prof. Ali A. Mazrui. Conflicts and Harmony in Zanzibar ± Memoirs, imeandikwa na Ali Muhsin Al Barwani, Dubai, 2002. Constitutional and Legal System of Tanzania: A Civics Sourcebook, Kimehaririwa na Prof. Issa G. Shivji na Wenzake, Dar es Salaam: Mkuki na Nyota Publishers(2004). Environment, Aid and Politics in Zanzibar, Kimeandikwa na Chachge S.L. Chachage, Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press(1996) Limited, 2000. Fundamental Rights and Freedoms in Tanzania, Kimehaririwa na Prof. Chris Maina Peter na Prof. Ibrahim Hamisi Juma, Dar es Salaam: Mkuki na Nyota Publishers(1998). Human Rights Protection and Enforcement in Tanzania, Kimeandikwa na Prof. Haroub Othman, Dar es Salaam: The National Assembly, 1997. IFES International Observer Report: The October 29, 2000 General Elections in Zanzibar, Ripoti hii imetayarishwa na International Foundation for Election Systems(IFES), Washington, D.C.: IFES, 2000. 134 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya 1977. Katiba ya Zanzibar ya 1984. Kitabu cha Kiada kwa Mahakimu wa Mahakama za Mwanzo, Kimetolewa na Tume ya Haki na Amani(TEC), Dar es Salaam(2001). Law& Justice in Tanzania: Quarter of a Century of the Court of Appeal of Tanzania, Kimehaririwa na Prof. Chris Maina Peter na Bi. Helen Kijo-Bisimba, Dar es Salaam: Mkuki na Nyota(2007) Liberalisation and Politics, Kimehaririwa na Prof. Haroub Othman na Rwekaza Mukandala), Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press, 1994. Maadili Mema Msingi wa Uongozi: Mfano wa Nyalali, kimetolewa na Christian Professionals of Tanzania(CPT), 2003. Mufti Act of Zanzibar: The Fundamental Rights and Freedoms of Muslims on the Isles, kimeandikwa na Prof. Chris Maina Peter(2008). Perspective on Legal Aid and Access to Justice in Zanzibar, kimehaririwa na Prof. Haroub Othman and Prof. Chris Maina Peter(2003). =DQ]LEDU , kimeandikwa na Dr. Hamudi Ismail Majamba(2008). Possibility and Rationale of Establishing Kadhi Courts in Tanzania Mainland, kimeandikwa na Dr. Hamudi Ismail Majamba(2008). Racism, Racial Discrimination, Xenophobia and Related Intolerances in Tanzania, kimendikwa na Prof. Chris Maina Peter, Harare: Association of African Political Scientists(2002). Reflections on Leadership in Africa: Essays in Honour of Mwalimu Julius Nyerere, Kimehaririwa na Prof. Haroub Othman, Brussels: VUB Press, 2000. Revolution in Zanzibar, kimeandikwa na John Okello, Nairobi: East African Publishing House, 1967. Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 135 7DOH , kimeandikwa na Balozi Don Petterson, Boulder Colorado: Westview Press, 2002. Suppressing Dissent: The Crackdown on Muslims in Zanzibar, kimeandikwa na Nafeez Mosaddeq Ahmed, Wembly, United Kingdom: Islamic Human Rights Commission, 2001. Tanzania at Cross-roads: The Conflict of the Union, Its Reasons and Its Consequences, Kimetayarishwa na Wolfgang Fengler, Munich: University of Augsburg, 1995. Tanzania Human Rights Report 2008, Kimetolewa na Legal and Human Rights Centre and Zanzibar Legal Services Centre, 2009. Tanzania: Democracy in Transition, Kimehaririwa na Prof. Haroub Othman na Immanuel Bavu na Michael Okema), Dar es Salaam University Press, 1990. Tanzania: The Bullets Were Raining ± The January 2001 Attacks on Peaceful Demonstrators in Zanzibar, Kimeandikwa na African Watch, New York: African Watch, 2002. The Democratisation Process in Zanzibar: A Retarded Transition, kimeandikwa na Mohamed Ali Bakari, Hamburg: Institute of African Affairs, 2001. The Development of the Constitution in Zanzibar, kimehaririwa na Prof. Haroub Othman; Chris Maina Peter and Ms, Immi Sikand(2006). The Elections in Zanzibar, United Republic of Tanzania 29 October 2000: The Report of the Commonwealth Observer Group, Ripoti hii imetayarishwa na Commonwealth Secretariat, London: Commonwealth Secretariat, 2001. The Independence of the Judiciary and the Rule of Law: Strengthening Constitutional Activism in East Africa, Kimehaririwa na Prof. Frederick W. Jjuuko, Kampala: Kituo Cha Katiba, 2005. The Judiciary in Zanzibar, kimehaririewa na Prof. Chris Maina Peter and Ms. Immi Sikand(2006). 136 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Constitutions, kimeandikwa na Prof. Issa G. Shivji, Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press, 1990. The Partner-ship: Tanganyika Zanzibar Union- 30 Turbulent Years, kimeandikwa na Aboud Jumbe, Dar es Salaam: Amana Publishers, 1994. The Political Economy of Land Reforms in Zanzibar: Before and After the Revolution, kimeandikwa na Ibrahim F. Shao, Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press, 1992. The Political Plight of Zanzibar, kimehaririwa na T.L. Maliyamkono, Dar es Salaam: Tema Publishing Company Ltd., 2000. The Right to Choose a Leader: Reflections on the 1995 Tanzanian General Elections, kimehaririwa na Cuthbert K. Omari, Dar es Salaam: Dar es Salaam University Press(1996) Limited, 1997, p. 128. The State in Tanzania: Who Controls it and Whose Interests Does it Serve? Kimeandikwa na Prof. Haroub Othman, Dar es Salaam University Press, 1980. The Zanzibar Revolution and Its Aftermath, kimeandikwa na A. Clayton, London: C. Hurst& Co, 1976. Utawala wa Katiba na Sheria, Utulivu wa Siasa Zanzibar: Muafaka na Utafutwaji wa Mwelekeo Mpya, kimehaririwa na Joseph OlokaOnyango na Maria Nassali, Kampala: Kituo Cha Katiba(2003). Zanzibar- The 1964 Revolution: Achievements and Prospects, kimeandikwa na Omari R. Mapuri, Dar es Salaam: TEMA Publishers Company Lted., 1996. Zanzibar ± Wave of Violence: A Fact Finding Report on Police Brutality and Election Mismanagement in Zanzibar, Ripoti hii imetayarishwa na International Federation for Human Rights na Legal and Human Rights Centre, Paris and Dar es Salaam: FIDH and LHRC, 2001. Zanzibar and the Union Question, kimehaririwa na Prof. Haroub Othman and Chris Maina Peter(2006). Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 137 Zanzibar Politics: A Proper Perspective, kimeandikwa na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, Zanzibar: Government Printer, 2000. Zanzibar: Background to the Revolution, kimeandikwa na Michael F. Lofchie, Princeton: Princeton University Press, 1965. Zanzibar: Overcoming the Challenges of Poverty Reduction, Kimehaririwa na Prof. Humphrey P.B. Moshi na Ammon V.Y Mbelle, Dar es Salaam na Zanzibar: Research and Consultancy Centre(2008). Zanzibar: The Rise and Fall of an Independent State 1895 ± 1964, kimendikwa na Suleiman Said Shahbal, Dubai, 2002. Zanzibar: Tradition and Revolution, kimeandikwa na Esmond Bradley Martin, London: Hamish Hamilton, 1978. Kimeandikwa na Prof. Haroub Othman, Dar es Salaam: Institute of Development Studies(1993). 138 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria USAWA MBELE YA SHERIA Moja ya haki muhimu ya binadamu ni usawa mbele ya sheria. Haki hii ina maana kwamba ni lazima pawe na usawa kwa wale wote wanaokutana mbele ya sheria. Usawa mbele ya sheria una maana nyingi. Hii ni pamoja na kuweza kuwezeshwa, inapohitajika, inapofikia wakati wa kujitetea. Haki hii ni muhimu kwa sababu siyo kila mtu anao uwezo wa kutoa uwezo wa kujitetea au kutoa maelezo yake inapobidi. Mheshimiwa Jaji Dennning wa Mahakama ya Rufaa ya Uingereza alielezea vizuri kabisa majanga ambayo yanaweza kutokea pale ambapo mtu wa kawaida ± hata akiwa msomi, anapokutana na Sheria. Katika kesi ya Pett v. Greyhound Racing Association Ltd (1969) Jaji Denning alieleza kwamba mara nyingi sana katika Mahakama za kawaida mtuhumiwa wa makosa ya jinai anapoambiwa amuulize maswali shahidi anayetoa ushahidi dhidi yake huzubaa. Na badala ya kuuliza maswali anaanza kutoa maelezo au hadithi ambazo hazimsaidii katika kesi yake. Haya yote yanatokea kwa sababu mtuhumiwa huyu hana fursa ya kupata ushauri mzuri kutoka kwa mtaalamu wa sheria. Mtaalamu huyu ni wakili. Lakini, wote tunafahamu kwamba siyo kila mtuhumiwa au mtu mwenye matatizo ya Sheria anao uwezo wa kuweka wakili wa kumsadia katika kesi yake. Hivyo, uwezo au nafasi yake ya kupata haki inakuwa kidogo sana. Kutokana na hali halisi, inapendekezwa katika nchi nyingi kwamba kuna haja ya kutafuta na kuruhusu watu wenye uwezo lakini wasio mawakili kuweza kuwashauri watuhumiwa au wadaawa wengine katika kesi zao. Makundi makubwa ya hawa watu yanazidi kujitokeza. Hawa ni Wasaidizi wa Sheria. Katika nchi tofauti wanapewa majina tofauti. Haya ni pamoja na Paralegals, barefoot Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 139 lawyers hutoa huduma ambayo katika hali halisi haiwezi kutolewa na wakili wa kawaida. Kwa upande wa Zanzibar tatizo la kutokuwa na mawakili na wanasheria wa kutosha tumeliona. Hivyo, Kituo cha Huduma za Sheria kimeamua kuwa na Wasaidizi wake wa Sheria. Idadi yao kwa sasa ni 54 kwa Unguja na Pemba. Hawa wamechukuliwa kutoka kila jimbo la uchaguzi(mmjoja kila jimbo) na wengine wanatoka katika Vikosi Maalum vya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar( Special Forces of the Revolutionary Government of Zanzibar). Kazi kubwa ya wasaidizi hawa wa sheria ni kupeleka huduma za kisheria kwa wananchi huko walipo na hasa sehemu zilizo nje ya miji mkubwa. Hivi sasa wasaidizi hawa wa sheria wanapewa umuhimu mkubwa katika mkakati wa Kituo wa kutoa huduma bora zaidi kwa Wazanzibari wote mahali walipo. Hivyo, Kituo kina mpango mkakati wa kuwaelimisha wasaidizi hawa wa sheria vizuri ili wawe mabingwa wa sheria kwa muda mfupi. Mwongozo huu wa sheria ni moja ya juhudi za Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar katika kuwaelimisha wasaidizi wetu wa sheria. Ni matumaini yetu kwamba utawanufaisha na kuwafanya waweze kufanya kazi zao kwa ufanisi zaidi. 140 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria AZIMIO LA ULIMWENGU JUU YA HAKI ZA BINADAMU(1984) Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 141 142 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 143 144 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 145 146 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 147 148 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 149 150 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 151 152 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 153 154 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 155 156 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 157 158 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 159 HAKI ZA BINADAMU KATIKA KATIBA YA JAMHURI YA MUUNGANO WA TANZANIA YA 1977 160 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 161 162 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 163 164 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 165 166 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 167 168 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 169 170 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 171 172 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 173 174 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 175 176 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 177 178 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 179 HAKI ZA BINADAMU KATIKA KATIBA YA ZANZIBAR YA 1984 180 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 181 182 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 183 184 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 185 186 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 187 188 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 189 190 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 191 MWONGOZO WA HAKI ZA BINADAMU KWA MUJIBU WA KATIBA YA ZANZIBAR YA 1984 SEPTEMBER, 2008 192 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 193 194 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 195 196 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 197 198 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 199 200 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 201 202 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 203 204 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 205 206 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 207 208 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 209 210 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 211 212 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 213 214 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 215 216 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 217 218 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 219 220 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 221 222 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 223 224 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 225 226 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 227 228 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 229 230 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 231 232 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 233 234 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 235 236 Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria Kituo cha Huduma za Sheria Zanzibar: Mwongozo wa Sheria Mbali Mbali za Zanzibar kwa Ajili ya Wasaidizi wa Sheria 237